< Ezekiel 44 >

1 And he turned me back, toward the way of the gate of the outer sanctuary, which looked toward the east. And it was closed.
Kisha yule mtu akanirudisha hata lango la nje la patakatifu linaloelekea mashariki; lilikuwa limefungwa kwa kukazwa.
2 And the Lord said to me: “This gate will be closed; it will not be opened. And man shall not cross through it. For the Lord, the God of Israel, has entered through it, and it shall be closed
Yahwe akanambia, “Hili lango litakuwa limefungwa; halitafunguliwa. Hakuna mtu atakaye pitia hapo, kwa kuwa Yahwe, Mungu wa Israeli ameingia kwa hilo, hivyo lilikuwa limefungwa kwa kukazwa.
3 to the prince. The prince himself will sit at it, so that he may eat bread before the Lord; he will enter by the way of the vestibule of the gate, and he will depart by the same way.”
Mtawala wa Israeli atakaa katika hilo kula chakula mbele ya Yahwe. Ataingia kwa njia ya varanda na kutoka kwa njia hiyo hiyo.”
4 And he led me in, along the way of the north gate, in the sight of the house. And I saw, and behold, the glory of the Lord filled the house of the Lord. And I fell upon my face.
Kisha akaniletea kwa njia ya lango la kaskazini linaloelekea kwenye nyumba. Hivyo nikaona na kutazama, utukufu wa Yahwe umejaa kwenye nyumba ya Yahwe, nikaanguka kifudifudi.
5 And the Lord said to me: “Son of man, set within your heart, and see with your eyes, and hear with your ears all that I am speaking to you about all the ceremonies of the house of the Lord and about all its laws. And set your heart upon the ways of the temple, along all the exits of the sanctuary.
Kisha Yahwe akanambia, “Mwanadamu, andaa moyo wako na tazama kwa macho yako na sikiliza kwa masikio yako kwa yote yale nikuambiayo, kwa amri zote za nyumba ya Yahwe na maagizo yote. Fikiri kuhusu malango ya nyumba na na matokeo ya malango.
6 And you shall say to the house of Israel, which provokes me: Thus says the Lord God: Let all your wicked deeds be sufficient for you, O house of Israel.
Kisha waambie wale walioasi, nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Acheni matendo yenu maovu kwenu, nyumba ya Israeli-
7 For you bring in foreign sons, uncircumcised in heart and uncircumcised in flesh, so that they may be in my sanctuary and may defile my house. And you offer my bread, the fat, and the blood, yet you have broken my covenant by all your wicked deeds.
ambayo mmewaleta wageni pamoja na wasiotahiriwa mioyo na wasiotahiriwa mwili kuwa katika patakatifu pangu, kuikufuru nyumba yangu, wakati mlipokuwa mnanitolea chakula, mafuta na damu-mmevunja agano langu kwa matendo yenu maovu.
8 And you have not observed the precepts of my sanctuary, yet you have stationed observers of my vigil in my sanctuary for yourselves.
Hamkumaliza kazi zenu zinazohusiana na vitu vitakatifu, lakini mmewateua wengine kuchukua kazi zenu, na mmewatuma kupaangalia mahali patakatifu pangu.
9 Thus says the Lord God: Any foreigner, any foreign son who is in the midst of the sons of Israel, who is uncircumcised in heart and uncircumcised in flesh, shall not enter into my sanctuary.
Bwana Yahe asema hivi: hakuna mgeni, ambaye hajatahiriwa kwenye moyo wake na mwili, kutoka yeyote wa hao waishio miongoni mwa watu wa Israeli, awezaye kuingia patakatifu pangu.
10 And as for the Levites, they have withdrawn far away from me, in the errors of the sons of Israel, and they have gone astray from me after their idols, and they have borne their iniquity.
Kisha Walawi wakaenda mbali nami-wakapotea mbali nami, kwenda kwenye sanamu zao-lakini watalipa kwa ajili ya dhambi yao.
11 They will be caretakers in my sanctuary, and doorkeepers at the gates of the house, and ministers to the house. They will slay the holocausts and the victims of the people. And they will stand before them, so that they may minister to them.
Wao ni watumishi katika patakatifu pangu, waangalizi wa malango ya nyumba na kutumika kwenye nyumba na kuchinja sadaka za kuteketezwa na dhabihu za watu, na watasimama mbele za watu na kuwatumikia.
12 But because they ministered to them in the sight their idols, and they became a stumbling block of iniquity to the house of Israel, for this reason, I have lifted up my hand against them, says the Lord God, and they will bear their iniquity.
Lakini kwa sababu wamefanya dhabihu mbele ya sanamu zao, wamekuwa kikwazo kwa dhambi ya nyumba ya Israeli. Kwa hiyo nitainua mkono wangu kuapa kiapo dhidi yao-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-watabeba adhabu yao.
13 And they shall not draw near to me, so as to exercise the priesthood for me, and they shall not approach to any of my holy things, which are near the Holy of Holies. Instead, they will bear their shame and their wicked deeds, which they committed.
Hawatakuja karibu nami kufanya kama makuhani au kukaribiakila vitu vyangu vitakatifu, vitu vitakatifu sana. Badala yake, watabeba lawama zao na hatia zao kwa ajili ya matendo yao ya karaha waliyoyafanya.
14 And I will make them doorkeepers of the house, for all its ministries and for all that will be done within it.
Lakini nitawaweka kama watunzaji wa kazi katika nyumba, kwa kazi zote na kila kitu kitakachofanyika ndani yake.
15 But the priests and the Levites who are the sons of Zadok, who observed the ceremonies of my sanctuary when the sons of Israel went astray from me, these shall draw near to me, so that they may minister for me. And they shall stand in my sight, so that they may offer to me the fat and the blood, says the Lord God.
Kisha makuhani walawi, hao wana wa Zadoki ambao waliokamilisha kazi ya patakatifu pangu wakati wana wa Israeli walipotea mbali nami-watakuja karibu nami kuniambudu. Watasimama mbele yangu kunitolea mafuta na damu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
16 They shall enter into my sanctuary, and they shall draw near to my table, so that they may minister for me, and so that they may observe my ceremonies.
Watakuja hata patakatifu pangu; wataikaribia meza yangu kuniabudu na kukamilisha kazi zao kwangu.
17 And when they enter the gates of the inner court, they shall be clothed with linen garments. Neither shall anything woolen be placed over them, when they minister within the gates of the inner and the outer court.
Hivyo itakuwa kwamba watakapokuja kwenye malango ya ua wa ndani, watatakiwa kuvaa mavazi ya kitani, kwa kuwa hawatakuja na sufu ndani ya lango la ua wa ndani na nyumba yake.
18 They shall have linen bands on their heads, and linen undergarments over their loins, and they shall not be girded so as to sweat.
Kutakuwa na vilemba juu ya vichwa vyao na kitani ndani ya viuno vyao. Ndani wasivae nguo ambayo itawafanya watoke jasho.
19 And when they go forth to the outer court to the people, they shall strip off their vestments, in which they ministered, and they shall place them in the storeroom of the sanctuary, and they shall clothe themselves with other garments. And they shall not sanctify the people in their vestments.
Wakati watakapotoka nje ya ua wa nje, hata kwenye ua wa ndani ili kwenda kwa watu, watavua nguo zao walizokuwa wamezivaa kisha wakatumika; watazivua na kuziweka chini katika chumba kitakatifu, hivyo wasiwafanye wengine watakatifu kwa kugusana na nguo zao maalumu.
20 Now they shall not shave their heads, and they shall not grow long hair. Instead, they shall trim the hair of their heads.
Hawatanyoa vichwa vyao wala kuruhusu nywele zao kuwa ndefu, watapunguza nywele za vichwa vyao.
21 And no priest shall drink wine, when he will be entering into the inner court.
Hakuna kuhani atakaye ruhusiwa kunywa mvinyo wakati atakapoingia kwenye uwa wa ndani,
22 And they shall not take as wife a widow or one who has been divorced. Instead, they shall take virgins from the offspring of the house of Israel. But they may also take a widow, if she is the widow of a priest.
hakuna kuchukua mjane au mwanamke aliyetalikiwa kama mke kwa ajili yake, lakini mwali kutoka safu ya nyumba ya Israeli au mjane aliyekuwa ameolewa na kuhani aliyepita.
23 And they shall teach my people the difference between holy and defiled, and they shall distinguish for them between clean and unclean.
Kwa kuwa watawafundisha watu wangu tofauti kati ya utakatifu na kukufuru; watawafanya kujua uchafu kutoka usafi.
24 And when there has been a controversy, they shall stand in my judgments, and they shall judge. They shall observe my laws and my precepts, in all my solemnities, and they shall sanctify my Sabbaths.
Katika kubishana watasimama kwenye hukumu pamoja na amri yangu; watakuwa waadilifu. Watashika sheria yangu na amri zangu katika sikukuu, na watasherekea siku yangu ya Sabato.
25 And they shall not enter to a dead person, lest they be defiled, except to father or mother, or son or daughter, or brother, or to a sister who does not have another man. By these, they may become unclean.
Hawataenda kwa mtu aliyekufa ili wasiwe najisi, vinginevyo awe ni baba au mama yao, mwana wa kiume au binti, kaka au dada ambaye hajawahi kulala na mtu; vinginevyo, watakuwa najisi.
26 And after he will have been cleansed, they shall number for him seven days.
Baada ya kuhani kuwa najisi, watahesabu mda wa siku saba kwa ajili yake.
27 And on the day when he enters into the sanctuary, to the inner court, so that he may minister to me in the sanctuary, he shall make an offering because of his offense, says the Lord God.
Katika siku atakayoingia mahali patakatifu, ndani kwenye uzio kutumika katika mahali patakatifu, ataleta sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
28 And there shall be no inheritance for them. I am their inheritance. And you shall not give them any possession in Israel. For I am their possession.
Hapa patakuwa urithi wao: Mimi ndiyo urithi wao, na usiwapatie mali katika Israeli; nitakuwa mali yao!
29 They shall eat the victim both for sin and for offenses. And every vowed offering in Israel shall be theirs.
Watakula chakula cha sadaka, sadaka za dhambi, sadaka za hatia, na kila kitakachotolewa kwa ajili ya Yahwe katika Israeli, vitakuwa vyao.
30 And the first-fruits of all the firstborn, and all the libations out of all that is offered, shall belong to the priests. And you shall give the first-fruits of your foods to the priest, so that he may return a blessing to your house.
Malimbuko ya kwanza ya vitu na kila sadaka, kila kitu kitokanacho na sadaka zenu vitakuwa mali ya makuhani, mtatoa sadaka ya chakula kizuri kwa makuhani ili kwamba baraka iweze kukaa katika nyumba zenu.
31 The priests shall not consume anything which has died on its own, or which was seized by a beast, whether from the fowl or the cattle.”
Makuhani hawatakula mzoga au mnyama aliyeraruliwa, iwe ni ndege au mnyama.

< Ezekiel 44 >