< Ezekiel 25 >

1 And the word of the Lord came to me, saying:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 “Son of man, set your face against the sons of Ammon, and you shall prophesy about them.
“Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
3 And you shall say to the sons of Ammon: Listen to the word of the Lord God: Thus says the Lord God: Because you have said, ‘Well, well!’ over my sanctuary, when it was profaned, and over the land of Israel, when it was desolated, and over the house of Judah, when they were led into captivity,
Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
4 therefore, I will deliver you to the sons of the East, as an inheritance. And they will arrange their fences within you, and they will place their tents within you. They will eat your crops, and they will drink your milk.
kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
5 And I will make Rabbah into the habitation of camels, and the sons of Ammon into the resting place of cattle. And you shall know that I am the Lord.
Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
6 For thus says the Lord God: Because you have clapped your hands and stomped your foot, and have rejoiced with all your heart against the land of Israel,
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
7 therefore, behold, I will extend my hand over you, and I will deliver you as a spoil of the Gentiles. And I will destroy you from the peoples, and I will perish you from the lands, and I will crush you. And you shall know that I am the Lord.
Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
8 Thus says the Lord God: Because Moab and Seir have said, ‘Behold, the house of Judah is like all the Gentiles!’
Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
9 therefore, behold, I will open the shoulder of Moab from the cities, from his cities, I say, and from his borders, the famous cities of the land of Beth-Jesimoth, and Baal-meon, and Kiriathaim,
Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
10 with the sons of Ammon, to the sons of the East, and I will give it to them as an inheritance, so that there may no longer be a remembrance of the sons of Ammon among the Gentiles.
kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
11 And I will execute judgments in Moab. And they shall know that I am the Lord.
Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
12 Thus says the Lord God: Because Idumea has taken vengeance, so as to vindicate herself against the sons of Judah, and has sinned grievously, and has sought revenge against them,
Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
13 therefore, thus says the Lord God: I will extend my hand over Idumea, and I will take from it both man and beast, and I will make it desolate from the south. And those who are in Dedan will fall by the sword.
Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
14 And I will issue my vengeance upon Idumea, by the hand of my people, Israel. And they shall act in Idumea in accord with my wrath and my fury. And they shall know my vengeance, says the Lord God.
Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
15 Thus says the Lord God: Because the Philistines have taken vengeance, and have revenged themselves with all their soul, destroying, and fulfilling ancient hostilities,
Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
16 because of this, thus says the Lord God: Behold, I will extend my hand over the Philistines, and I will destroy those who destroy, and I will perish the remnant of the maritime regions.
Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
17 And I will execute great vengeance against them, reproving them in fury. And they shall know that I am the Lord, when I will send my vengeance upon them.”
Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'

< Ezekiel 25 >