< Exodus 26 >
1 “Truly, thus shall you make the tabernacle: You shall make ten curtains of fine twisted linen, and hyacinth as well as purple, and twice-dyed scarlet, with diverse embroidery.
Lazima ufanye hiyo maskani iwe na mapazia kumi ifanye ya nguo ya kitani nzuri ya kusokota, pamoja na nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, pamoja na makerubi. Kazi ya fundi stadi.
2 The length of one curtain shall have twenty-eight cubits. The width shall be four cubits. The entire set of curtains shall be of one measure.
Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa ishirini na nane, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Mapazia yote yatakuwa ya kipimo kimoja.
3 Five curtains shall be joined to one another, and the other five shall be similarly coupled together.
Mapazia matano yataungwa pamoja, na mapazia matano mengine yataungwa pamoja.
4 You shall make loops of hyacinth on the sides at the edges of the curtains, so that they will be able to be joined to one another.
Lazima ufanye tanzi za rangi ya samawati upande wa mwisho wa pazia moja katika ule upindo wa fungu lake. Vivyo hivyo utafanya upande wa mwisho wa ile pazia iliyo, katika fungu la pili.
5 A curtain shall have fifty loops on each of two sides, inserted in such a manner that loop may come against loop, and one can be fitted to the other.
Fanya matanzi hamsini katika pazia moja, na matanzi hamsini katika upande wa mwisho wa ile pazia iliyo katika kuungana kwa pili.
6 You shall also make fifty rings of gold, with which the veils of the curtains are to be joined, so that it shall be one tabernacle.
Fanya hivi ili hizo tanzi zielekeana. Kisha ufanye vifungo hamsini vya dhahabu, na kuunganisha hayo mapazia pamoja kwa vile vifungo na hiyo maskani itakuwa ni moja.
7 You shall also make eleven haircloth canopies to cover the roof of the tabernacle.
Lazima ufanye mapazia ya nywele za mbuzi yawe hema juu ya maskani. Lazima ufanye mapazia kumi na moja.
8 The length of one canopy shall hold thirty cubits, and the width, four. The measure of all the canopies shall be equal.
Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa thelathini, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Hayo mapazia kumi na moja yatakuwa ya kipimo kimoja.
9 Five of these you shall join by themselves, and six of these you shall couple to one another, in such a manner as to double the sixth canopy at the front of the roof.
Lazima utaunganisha mapazia matano mbali, na mapazia sita mbali, na lile pazia la sita utalikunja hapo upande wa mbele wa ile hema.
10 You shall also make fifty loops along the edge of one canopy, so that it may be able to be joined with the other, and fifty loops along the edge of the other canopy, so that it may be coupled with the other.
Ufanye tanzi hamsini upande wa mwisho wa pazia lile lililo la mwisho katika hayo yaliyounganywa pamoja, na tanzi hamsini upande wa mwisho wa lile pazia lililo nje katika hayo ya pili yaliyounganywa pamoja.
11 You shall also make fifty brass buckles, with which the loops may be joined, so that there may be one covering out of all.
Kisha ufanye vifungo hamsini vya shaba, na kuvitia vile vifungo katika zile tanzi, na kuiunganya ile hema pamoja, ili iwe hema moja.
12 Then what will be left over of the canopies which are prepared for the roof, that is, one canopy which is in excess, from half of it you shall cover the back of the tabernacle.
Kipande kile kilichosalia, kile kiangukacho, cha yale mapazia ya hema, itaanguka huko upande wa nyuma wa maskani.
13 And one cubit will hang down on one side, and another on the other side, which is more than the length of the curtains, protecting both sides of the tabernacle.
Lazima kuwe na dhiraa moja upande mmoja, na ile dhiraa moja upande wa pili - ya urefu wa mapazia ya hema uliosalia, zitaanguka katika ubavu wa maskani upande huu na upande huu, ili kuifunika.
14 You shall also make another covering for the roof from the skins of rams, dyed-red, and above that again, another covering of violet-colored skins.
Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
15 You shall also make the standing panels of the tabernacle from setim wood.
Nawe lazima ufanye hizo fremu za maskani za mti wa mjohoro.
16 Of these, each shall have ten cubits in length, and in width, one and one half.
Kila fremu utakuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wake kila ubao utakuwa dhiraa moja na nusu.
17 At the sides of the panels, there shall be made two dovetails, by which one panel may be connected to another panel; and in this way all the panels shall be prepared.
Kila fremu itakuwa na ndimi mbili, zenye kuunganishwa huu na huu. Ndivyo utakavyozifanya mbao zote za maskani.
18 Of these, twenty shall be at the meridian, which lies toward the south.
Kisha ufanye zile mbao za maskani, mbao ishirini kwa upande wa kusini kuelekea kusini.
19 For these, you shall cast forty bases of silver, so that two bases will lie under each panel at its two corners.
Lazima nawe ufanye vitako arubaini vya fedha chini ya zile fremu ishirini. Vitako viwili chini ya fremu moja, kupokea zile ndimi zake mbili, na vitako viwili chini ya fremu nyingine kupokea zile ndimi zake mbili.
20 Likewise, at the second side of the tabernacle, which lies to the north, there shall be twenty panels,
Kwa upande wa pili wa maskani, upande wa kaskazini, mbao ishirini
21 having forty bases of silver; two bases shall support each panel.
na vitako vyake vya fedha arubaini. Lazima kuwe na vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya fremu nyingine.
22 Truly, toward the western part of the tabernacle, you shall make six panels,
Ufanye fremu sita kwa ajili ya upande wa nyuma wa maskani kuelekea magharibi.
23 and again another two, which will be raised at the corners, behind the back of the tabernacle.
Tena ufanye fremu mbili kwa ajili ya hizo pembe za maskani zilizo upande wa nyuma.
24 And these shall be joined together from bottom to top, and one joint shall retain them all. Likewise, two of the panels, which will be set at the corners, shall be served by similar joints.
Hizi fremu zitakuwa zimetengana upande wa chini, lakini zimeshinkana kwa juu ya duara moja.
25 And together these will be eight panels, and their bases of silver, sixteen, counting two bases for each panel.
Fremu zitakuwa ni nane, na vitako vyake vya fedha. Vitako kumi na sita, vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya ubao wa pili.
26 You shall also make five bars of setim wood, to connect the panels on one side of the tabernacle,
Lazima ufanye mataruma ya mti wa mshita- mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa maskani,
27 and five others on the other side, and the same number toward the western part.
na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa maskani ulio nyuma kuelekea magharibi.
28 These shall be set along the middle of the panels, from one end all the way to the other end.
Na hilo taruma la katikati lililo katikati ya zile fremu, litapenya toka mwisho huu hata mwisho huu.
29 Likewise, the panels themselves you shall overlay with gold, and you shall establish rings of gold in them, by which the bars of the panels may be connected. These you shall cover with layers of gold.
lazima uzifunuke hizo fremu kwa dhahabu. Nawe lazima ufanye maduara yake ya za dhahabu, kuwa kama vishikizo, na hayo mataruma utayafunika dhahabu.
30 And you shall raise the tabernacle according to the example which was shown to you on the mountain.
Nawe utaisimamisha hiyo maskani sawasawa na mfano wake uliooneshwa mlimani.
31 You shall also make a veil of hyacinth, and purple, and twice-dyed scarlet, and fine twisted linen, wrought with a diversity of continuous and beautiful embroidery.
Nawe fanya pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na nguo za kitani nzuri zenye kusokotwa, litafumwa na kutiwa makerubi, kazi ya fundi stadi.
32 And you shall suspend it before four columns of setim wood, which themselves certainly shall be overlaid with gold, and have heads of gold, but bases of silver.
Kisha litungike katika nguzo nne za mti wa mshita zilizofunikwa dhahabu, vifungo vyake vitakuwa vya dhahabu, katika vitako vya fedha vinne.
33 Then the veil shall be inserted through the rings. Beyond the veil, you shall place the ark of the testimony, where both the Sanctuary and the Sanctuary of Sanctuaries shall be divided.
Nawe tungika lile pazia chini ya vile vifungo, nawe lete lile sanduku la ushuhuda. Lile pazia litawagawanyia kati ya patakatifu, na mahali patakatifu sana.
34 And you shall place the propitiatory over the ark of the testimony, in the Holy of Holies.
Nawe lazima utaweka kiti cha rehema juu ya lile sanduku la ushuhuda ndani ya mahali pale patakatifu sana. Na ile meza utaiweka nje ya pazia.
35 And the table shall be outside the veil. And opposite the table shall be the lampstand, in the meridian of the tabernacle. For the table shall stand at the north side.
Lazima uweke kinara cha taa kuikabili ile meza upande wa maskani wa kuelekea kusini. Lile meza utaiweka upande wa kaskazini.
36 You shall also make a tent at the entrance of the tabernacle from hyacinth, and purple, and twice-dyed scarlet, and fine twisted linen, wrought with embroidery.
Kisha utafanya kisitiri kwa mlango wa hema, cha nyuzi za rangi ya buluu, zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji wa taraza.
37 And you shall overlay with gold five columns of setim wood, over which the tent shall be drawn. The heads of these shall be of gold, and the bases of brass.”
Nawe fanya nguzo tano za mti wa mshita kwa kile kisitiri, na kuzifunika dhahabu; kulabu zake zitakuwa za dhahabu. Nawe utasubu vitako vya shaba vitano kwa ajili yake.