< Ecclesiastes 3 >

1 All things have their time, and all things under heaven continue during their interval.
Kwa kuwa kila kitu na wakati wake, na majira kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 A time to be born, and a time to die. A time to plant, and a time to pull up what was planted.
Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kung'oa yaliyopandwa,
3 A time to kill, and a time to heal. A time to tear down, and a time to build up.
wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomo na wakati wa kujenga.
4 A time to weep, and a time to laugh. A time to mourn, and a time to dance.
Kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati kucheza,
5 A time to scatter stones, and a time to gather. A time to embrace, and a time to be far from embraces.
wakati wa kutupa mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia watu wengine wakati wa kutokumbatia.
6 A time to gain, and a time to lose. A time to keep, and a time to cast away.
Kuna wakati wa kutafuta vitu na wakati wa kutotafuta, wakati wa kutunza vitu na wakati wa kuvitupa,
7 A time to rend, and a time to sew. A time to be silent, and a time to speak.
wakati kuchana mavazi na wakati wa kuyashona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza.
8 A time of love, and a time of hatred. A time of war, and a time of peace.
Kuna wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
9 What more does a man have from his labor?
Ni faida gani mfanyakazi aipatayo katika kazi yake?
10 I have seen the affliction that God has given to the sons of men, in order that they may be occupied by it.
Nimeona kazi ambayo Mungu amewapa wanadamu kuitimiza.
11 He has made all things good in their time, and he has handed over the world to their disputes, so that man may not discover the work which God made from the beginning, even until the end.
Mungu amefanya kila kitu kufaa kwa wakati wake. Pia ameweka umilele ndani ya mioyo yao. Lakini mwanadamu hawezi kuelewa matendo ambayo Mungu ameyafanya, tangu mwanzo wao hadi mwisho.
12 And I realize that there is nothing better than to rejoice, and to do well in this life.
Ninajua kuwa hakuna kilicho bora kwa mtu yeyote kuliko kufurahi na kutenda mema maadamu anaishi-
13 For this is a gift from God: when each man eats and drinks, and sees the good results of his labor.
na kwamba kila mmoja anapaswa ale na kunywa na anapaswa kuelewa jinsi ya kufurahia mazuri ambayo yanatoka katika kazi zake zote. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu.
14 I have learned that all the works which God has made continue on, in perpetuity. We are not able to add anything, nor to take anything away, from those things which God has made in order that he may be feared.
Ninajua kwamba chochote afanyacho Mungu kinadumu milele. Hakuna kinaweza kuongezwa au kuondolea, kwa sababu Mungu ndiye aliyekifanya, ili kwamba watu wamsogelee kwa heshima.
15 What has been made, the same continues. What is in the future, has already existed. And God restores what has passed away.
Chochote kilichopo kimekwisha kuwepo; chochote kitakachokuwepo kimekwisha kuwepo. Mungu huwafanya wanadamu kutafuka vitu vilivyjificha.
16 I saw under the sun: instead of judgment, impiety, and instead of justice, iniquity.
Na nimeona kwamba chini ya jua ubaya upo mahali palipopaswa kuwa na haki, na sehemu ya haki mara nyingi ina ubaya.
17 And I said in my heart: “God will judge the just and the impious, and then the time for each matter shall be.”
Nikasema moyoni mwangu, “Mungu atahukumu mwenye haki na mbaya kwa wakati muafaka kwa kila jambo na kila tendo.
18 I said in my heart, about the sons of men, that God would test them, and reveal them to be like wild animals.
Nikasema moyoni mwangu, “Mungu huwajaribu wanadamu kuwaonyesha kwamba wao ni kama wanyama.”
19 For this reason, the passing away of man and of beasts is one, and the condition of both is equal. For as a man dies, so also do they die. All things breathe similarly, and man has nothing more than beast; for all these are subject to vanity.
Kwa kuwa mwisho watoto wa wanadamu na mwisho wa wanyama ni sawa. Kifo cha mmoja ni sawa na kifo cha mwingine. Wote wana pumzi sawa. Hakuna faida kwa mwanadamu zaidi ya wanyama. Kwa kuwa hakuna kila kitu isipokuwa pumzi?
20 And all things continue on to one place; for from the earth they were made, and unto the earth they shall return together.
Kila kitu kinaenda sehemu moja. Kila kitu kinatoka mavumbini, na kila kitu kinarudi katika mavumbini.
21 Who knows if the spirit of the sons of Adam ascend upward, and if the spirit of the beasts descend downward?
Ni nani ajuaye kama roho ya mwanadamu inaenda juu na roho ya wanyama inaenda chini ya nchi?
22 And I have discovered nothing to be better than for a man to rejoice in his work: for this is his portion. And who shall add to him, so that he may know the things that will occur after him?
kwa hiyo tena nikatambua kwamba hakuna lililo jema kwa yeyote zaidi ya kufurahia kazi yake, kwa kuwa hilo ndilo jukumu lake. Ni nani awezaye kumleta tena kuona kinachotokea baada yake?

< Ecclesiastes 3 >