< Deuteronomy 33 >

1 This is the blessing, with which Moses, the man of God, blessed the sons of Israel before his death.
Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
2 And he said: “The Lord went forth from Sinai, and he arose for us from Seir. He appeared from Mount Paran, and thousands of holy ones were with him. The fiery law was in his right hand.
Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
3 He loved the people; all the holy ones are in his hand. And those who approach his feet shall receive from his doctrine.
Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
4 Moses instructed us in the law, the inheritance of the multitude of Jacob.
Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
5 The king shall have great righteousness, at the gathering of the princes of the people with the tribes of Israel.
Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
6 Let Ruben live, and not die, and may he be small in number.”
Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
7 This is the blessing of Judah. “Hear, O Lord, the voice of Judah, and lead him to his people. His hands shall fight for him, and he shall be his helper against his adversaries.”
Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
8 Likewise, to Levi he said: “Your perfection and your doctrine are for your holy man, whom you have proven by temptation, and whom you have judged at the Waters of Contradiction.
Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
9 He has said to his father and to his mother, ‘I do not know you,’ and to his brothers, ‘I will disregard you.’ And they have not known their own sons. Such as these have kept your word and have observed your covenant:
Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
10 your judgments, O Jacob, and your law, O Israel. They shall place incense before your fury and a holocaust upon your altar.
Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
11 O Lord, bless his strength, and receive the works of his hands. Strike the backs of his enemies, and do not let those who hate him rise up.”
Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
12 And to Benjamin he said: “The most beloved of the Lord will live confidently in him. He shall remain all day long, as if in a bridal chamber, and he shall rest amid her arms.”
Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
13 Likewise, to Joseph he said: “His land shall be from the blessing of the Lord, from the fruits of heaven, and from the dew, and from the abyss which lies below,
Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
14 from the fruits of the crops under the sun and the moon,
Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
15 from the heights of the ancient mountains, from the fruits of the everlasting hills,
kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
16 and from the fruits of the earth with all its plenitude. May the blessing of him who appeared in the bush, settle upon the head of Joseph, and upon the top of the head of the Nazarite among his brothers.
Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
17 His excellence is like that of a first-born bull. His horns are like the horns of a rhinoceros; he shall brandish these against the Gentiles, even to the ends of the earth. These are the multitudes of Ephraim, and these the thousands of Manasseh.”
Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
18 And to Zebulun he said: “Rejoice, O Zebulun, in your departure, and Issachar, in your tabernacles.
Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
19 They shall summon the peoples to the mountain. There, they shall immolate the victims of justice, who feed on the flood of the sea, as if on milk, and on the hidden treasures of the sands.”
Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
20 And to Gad he said: “Blessed is Gad in his breadth. He has rested like a lion, and he has seized the arm and the top of the head.
Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
21 And he has seen his own pre-eminence, which his teacher has stored up as his portion. He was with the princes of the people, and he accomplished the justices of the Lord, and his judgment with Israel.”
Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
22 Likewise, to Dan he said: “Dan is a young lion. He shall flow plentifully from Bashan.”
Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
23 And to Naphtali he said: “Naphtali shall enjoy abundance, and he shall be full of the blessings of the Lord. He shall possess the sea and the Meridian.”
Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
24 Likewise, to Asher he said: “Let Asher be blessed with sons. Let him be pleasing to his brothers, and let him dip his foot in oil.
Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
25 His shoe shall be of iron and of brass. As were the days of your youth, so also shall be your old age.
Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
26 There is no other god like the God of the most righteous one. He who rides upon the heavens is your helper. His magnificence scatters the clouds.
Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
27 His habitation is above, and the everlasting arms are below. He shall cast out the enemy before your face, and he shall say: ‘Be utterly broken!’
Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
28 Israel shall live in confidence and alone, as the eye of Jacob in a land of grain and of wine; and the heavens shall be misty with dew.
Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
29 Blessed are you, O Israel. Who is like you, the people who are saved by the Lord? He is the shield of your assistance and the sword of your glory. Your enemies will refuse to acknowledge you, and so you shall tread upon their necks.”
Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.

< Deuteronomy 33 >