< Deuteronomy 25 >
1 “If there is a case between persons, and they apply to the judges, they shall give the palm of justice to the one whom they perceive to be just, and they shall condemn of impiety the one who is impious.
Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia.
2 But if they see that the one who has sinned is worthy of stripes, they shall prostrate him and cause him to be beaten before them. According to the measure of the sin, so shall the measure of the stripes be.
Kama mtu mwenye hatia anastahili kuchapwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili achapwe mbele yake idadi ya viboko kulingana na kosa lake,
3 Even so, these shall not exceed the number of forty. Otherwise, your brother may depart, having been wounded shamefully before your eyes.
lakini kamwe asichapwe zaidi ya viboko arobaini. Ikiwa atachapwa zaidi ya viboko arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.
4 You shall not muzzle an ox as it is treading out your crops in the field.
Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.
5 When brothers are living together, and one of them dies without children, the wife of the deceased shall not marry another. Instead, his brother shall take her, and he shall raise up offspring for his brother.
Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake.
6 And the first son from her, he shall call by his brother’s name, so that his name will not be abolished from Israel.
Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.
7 But if he is not willing to take his brother’s wife, who by law must go to him, the woman shall go to the gate of the city, and she shall call upon those greater by birth, and she shall say: ‘The brother of my husband is not willing to raise up his brother’s name in Israel; nor will he join with me.’
Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.”
8 And immediately, they shall summon him to be sent, and they shall question him. If he responds, ‘I am not willing to accept her as a wife,’
Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,”
9 then the woman shall approach him in the sight of the elders, and she shall remove his shoe from his foot, and she shall spit in his face, and she shall say: ‘So shall it be done to the man who was not willing to build up his brother’s house.’
mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.”
10 And his name shall be called in Israel: The House of the Unshod.
Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.
11 If two men have a conflict between themselves, and one begins to do violence to the other, and if the other’s wife, wanting to rescue her husband from the hand of the stronger one, extends her hand and grasps him by his private parts,
Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri,
12 then you shall cut off her hand. Neither shall you weep over her with any mercy.
huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.
13 You shall not have differing weights, greater and lesser, in your bag.
Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi.
14 Neither shall there be in your house a greater and a lesser measure.
Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo.
15 You shall have a just and a true weight, and your measure shall be equal and true, so that you may live for a long time upon the land, which the Lord your God will give to you.
Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
16 For the Lord your God abominates him who does these things, and he loathes all injustice.
Kwa maana Bwana Mungu wako humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.
17 Remember what Amalek did to you, along the way, when you were departing from Egypt:
Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri.
18 how he met you and cut down the stragglers of the troops, who were sitting down, exhausted, when you were consumed by hunger and hardship, and how he did not fear God.
Wakati mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.
19 Therefore, when the Lord your God will give you rest, and you will have subdued all the surrounding nations, in the land which he has promised to you, you shall delete his name from under heaven. Take care not to forget this.”
Bwana Mungu wako atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi akupayo kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!