< Deuteronomy 20 >
1 “If you go out to battle against your enemies, and you see horsemen and chariots, and that the multitude of your adversary’s army is greater than your own, you shall not fear them. For the Lord your God, who led you away from the land of Egypt, is with you.
Mtakapokwenda vitani kupigana na adui zenu na mkaona farasi na magari ya vita na jeshi kubwa kuliko lenu, msiwaogope, kwa sababu Bwana Mungu wenu aliyewatoa kutoka Misri, atakuwa pamoja nanyi.
2 Then, as the battle now draws near, the priest shall stand before the front ranks, and he shall speak to the people in this manner:
Wakati mtakapokaribia kwenda vitani, kuhani atakuja mbele na kuhutubia jeshi.
3 ‘Listen, O Israel! Today you engage in a battle against your enemies. Do not let your heart be overwhelmed with fear. Do not be apprehensive. Do not yield. You should have no dread of them.
Atasema: “Sikia, ee Israeli, leo unakwenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao.
4 For the Lord your God is in your midst, and he will contend against your enemies on your behalf, so that he may rescue you from peril.’
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi.”
5 Likewise, the officers shall proclaim, throughout every company, in the hearing of the soldiers: ‘What man is there who has built a new house, and has not dedicated it? Let him go and return to his house, lest perhaps he may die in the battle, and another man may dedicate it.
Maafisa wataliambia jeshi: “Je, kuna yeyote aliyejenga nyumba mpya ambayo haijawekwa wakfu? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akaiweka wakfu.
6 What man is there who has planted a vineyard, and has not yet caused it to be common, so that all may eat from it? Let him go, and return to his house, lest perhaps he may die in the battle, and another man may carry out his office.
Je, kuna yeyote aliyepanda shamba la mizabibu na hajaanza kulifurahia? Yeye na arudi nyumbani, au sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akalifurahia.
7 What man is there, who has betrothed a wife, and has not taken her? Let him go, and return to his house, lest perhaps he may die in battle, and another man may take her.’
Je, kuna yeyote aliyeposa mwanamke na hajamwoa? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akamwoa.”
8 After these things have been declared, they shall add the remainder, and shall say to the people: ‘What man is there who is overwhelmed by fear and is fainthearted? Let him go, and return to his house, lest he cause the hearts of his brothers to fear, just as he himself has been thoroughly stricken with fear.’
Kisha maafisa wataongeza haya, “Je, kuna mtu anayeogopa ama kufa moyo? Yeye na arudi nyumbani ili ndugu zake nao wasije wakafa moyo pia.”
9 And when the officers of the army have become silent, and have completed their speech, each one shall prepare his unit to wage war.
Wakati maafisa watakapomaliza kuzungumza na jeshi, watawateua wakuu wa vikosi.
10 When, at any time, you approach a city to fight against it, you shall first offer peace to it.
Wakati mtakapokwenda kushambulia mji, wapeni watu wake masharti ya amani.
11 If they receive it, and open the gates to you, then all the people who are in it shall be saved, and they shall serve you by paying tribute.
Wakikubali na kuwafungulia malango yao, watu wake wote watawatumikia kwa kufanya kazi ngumu na watawatumikia.
12 But if they are not willing to enter into an agreement, and they begin to act against you in warfare, then you shall besiege it.
Ikiwa watakataa kufanya mapatano ya amani na wakiwaingiza katika vita, basi mtauzunguka mji huo kwa vita.
13 And when the Lord your God will have delivered it into your hands, you shall strike down anyone who is in it, of the male gender, with the edge of the sword,
Wakati Bwana Mungu wenu atakapouweka mji huo mkononi mwenu, waueni kwa upanga wanaume wote waliomo ndani yake.
14 but not the women and young children, nor the cattle and the other things that are within the city. And you shall divide all the plunder to the soldiers, and you shall eat the spoils from your enemies, which the Lord your God will give to you.
Kwa upande wa wanawake, watoto, mifugo na kila kitu kingine chochote ndani ya huo mji, mnaweza kuvichukua kama nyara kwa ajili yenu. Nanyi mnaweza kuzitumia hizo nyara ambazo Bwana Mungu wenu amewapa kutoka kwa adui zenu.
15 So shall you do to all the cities which are at a great distance from you, those which are not among the cities that you shall receive as a possession.
Hivi ndivyo mtakavyofanya kwa miji yote ambayo iko mbali nanyi, ambayo haimilikiwi na mataifa ya karibu.
16 But among those cities which shall be given to you, you shall not permit anyone at all to live.
Hata hivyo, katika miji ya mataifa ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi, msiache kitu chochote hai kinachopumua.
17 Instead, you shall put them to death with the edge of the sword, specifically: the Hittite and the Amorite and the Canaanite, the Perizzite and the Hivite and the Jebusite, just as the Lord your God has commanded you.
Waangamizeni kabisa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, kama Bwana Mungu wenu alivyowaamuru.
18 Otherwise, they may teach you to do all the abominations which they have committed for their own gods. And then you would sin against the Lord your God.
La sivyo, watawafundisha kufuata mambo yote ya machukizo wanayofanya wakiabudu miungu yao, nanyi mtatenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu.
19 When you will have besieged a city for a long time, and you will have encircled it with fortifications, so that you may fight against it, you shall not cut down trees from which one is able to eat, neither shall you cause devastation with axes to the surrounding region. For it is a tree, and not a man. It is not able to increase the number of those who are fighting against you.
Wakati mtakapouzunguka mji kwa vita kwa muda mrefu, mkipigana dhidi yake ili kuuteka, msiharibu miti yake kwa kuikata kwa shoka, kwa sababu mtaweza kula matunda yake. Hivyo msiikate. Je, miti hiyo ya mashambani ni watu, hata muizingire?
20 But if there are any trees which are not fruitful, but are wild, and if these are fit for other uses, then cut them down, and make machines, until you have captured the city that is contending against you.”
Hata hivyo, mnaweza kuikata miti ambayo sio miti ya matunda na kuitumia kujenga ngome, mpaka mji ulio katika vita na ninyi utakapoanguka.