< Deuteronomy 14 >

1 “Be sons of the Lord your God. You shall not cut yourselves, nor make yourselves bald, because of the dead.
Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
2 For you are a holy people, for the Lord your God. And he chose you, so that you may be a people particularly his, out of all the nations on earth.
kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
3 You shall not eat the things that are unclean.
Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
4 These are the animals which you ought to eat: the ox, and the sheep, and the goat,
Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
5 the stag and the roe deer, the gazelle, the wild goat, the addax, the antelope, the giraffe.
kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
6 Every beast which has a hoof divided into two parts and which also chews the cud, you shall eat.
Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
7 But those which chew over again, but do not have a divided hoof, you must not eat, such as the camel, the hare, and the hyrax. Since these chew the cud, but do not have a divided the hoof, they shall be unclean to you.
Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
8 The pig also, since it has a divided hoof, but does not chew over again, shall be unclean. Their flesh shall not be eaten, and you shall not touch their carcasses.
Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
9 These you shall eat out of all that dwells in the waters: whatever has fins and scales, you shall eat.
Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
10 Whatever is without fins and scales, you shall not eat, for these are unclean.
Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
11 All the clean birds, you shall eat.
Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
12 You shall not eat those that are unclean: such as the eagle, and the griffin, and the osprey,
Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
13 the crane, and the vulture, and the kite, according to their kind,
kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
14 and any kind of raven,
kunguru wa aina yoyote,
15 and the ostrich, and the owl, and the gull, and the hawk, according to their kind,
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
16 the heron, and the swan, and the ibis,
bundi, mumbi, bundi mkubwa,
17 and the sea bird, the marsh hen, and the night raven,
mwari, nderi, mnandi,
18 the pelican and the plover, each in their kind, likewise the crested hoopoe and the bat.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
19 And anything which crawls and also has little wings shall be unclean, and shall not be eaten.
Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
20 All that is clean, you shall eat.
Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
21 But whatever has died of itself, you shall not eat from it. Give it to the sojourner, who is within your gates, so that he may eat, or sell it to him. For you are the holy people of the Lord your God. You shall not boil a young goat in the milk of his mother.
Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
22 Each year, you shall separate the tithes out of all your crops which spring forth from the earth.
Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
23 And you shall eat these in the sight of the Lord your God, in the place which he will choose, so that his name may be invoked there: the tenth part of your grain and wine and oil, and the firstborn from the herds and your sheep. So may you learn to fear the Lord your God at all times.
Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
24 But when the way and the place which the Lord your God will have chosen is further away, and he will have blessed you, so that you are not able to carry all these things to it,
Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
25 you shall sell them all, so as to turn them into money, and you shall carry it in your hand, and you shall set out for the place which the Lord will choose.
basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
26 And you shall buy with the same money whatever pleases you, either from the herds or from the sheep, and also wine and liquor, and all that your soul desires. And you shall eat in the sight of the Lord your God, and you shall feast: you and your household.
Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
27 As for the Levite, who is within your gates, take care that you do not abandon him, for he has no other portion within your possession.
Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
28 In the third year, you shall separate another tenth part of all the things which spring forth for you at that time, and you shall store it within your gates.
Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
29 And the Levite, who has no other portion or possession with you, and the sojourner as well as the orphan and the widow who are within your gates, shall approach and eat and be satisfied, so that the Lord your God may bless you in all the works of your hands which you shall do.”
ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.

< Deuteronomy 14 >