< Deuteronomy 1 >

1 These are the words which Moses spoke to all of Israel, across the Jordan, in the plain of the wilderness opposite the Red Sea, between Paran and Tophel and Laban and Hazeroth, where gold is very plentiful,
Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
2 eleven days from Horeb, by way of Mount Seir as far as Kadesh-barnea.
(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
3 In the fortieth year, on the eleventh month, on the first day of the month, Moses told the sons of Israel all that the Lord had instructed him. And so he spoke to them,
Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
4 after he had struck down Sihon, the king of the Amorites, who lived at Heshbon, and Og, the king of Bashan, who resided at Ashtaroth and at Edrei,
Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
5 across the Jordan in the land of Moab. And so, Moses began to explain the law, and to say:
Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
6 “The Lord our God spoke to us at Horeb, saying: ‘You have remained long enough on this mountain.
Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
7 Turn back and go to the mountain of the Amorites, and to the other places which are near it: the plains as well as the mountainous regions, and the low-lying places opposite the south and along the shore of the sea, the land of the Canaanites, and Lebanon, as far as the great river Euphrates.’
Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
8 ‘Lo,’ he said, ‘I have delivered it to you. Enter and possess that which the Lord swore to your fathers, Abraham, Isaac, and Jacob, that he would give it to them, and to their offspring after them.’
Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
9 And I said to you, at that time:
Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
10 ‘I alone am not able to sustain you. For the Lord, your God, has multiplied you, and you are today like the stars of heaven, very many.
Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
11 May the Lord, the God of your fathers, add to this number many thousands more, and may he bless you, just as he has said.
Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
12 Alone, I do not have the strength to endure your arbitrations and judgments and disputes.
Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
13 Offer, from among you, wise and experienced men, those whose conversation has been proven within your tribes, so that I may appoint them as your rulers.’
Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
14 Then you responded to me: ‘What you intend to do is a good thing.’
Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
15 And so, I took from your tribes men, wise and noble, and I appointed them as rulers, as tribunes and centurions, and as leaders over fifty and over ten, who would teach you each thing.
Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
16 And I instructed them, saying: ‘Listen to them, and judge what is just, whether he is one of your citizens or a sojourner.
Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
17 There shall be no favoritism to any persons. So you shall listen to the little as well as to the great. And you shall not accept anyone’s reputation, for this is the judgment of God. But if anything seems difficult to you, then refer it to me, and I will hear it.’
Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
18 And I instructed you in all that you were obliged to do.
Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
19 Then, setting out from Horeb, we crossed through a terrible and great wasteland, which you saw along the way of the mountain of the Amorite, just as the Lord our God had instructed us. And when we had arrived at Kadesh-barnea,
Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
20 I said to you: ‘You have arrived at the mountain of the Amorite, which the Lord our God will give to us.
Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
21 Gaze upon the land that the Lord your God gives to you. Ascend and possess it, just as the Lord our God has spoken to your fathers. Do not be afraid, and do not become terrified by anything.’
Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
22 And you all approached me and said: ‘Let us send men who may consider the land, and who may report as to the way by which we ought to ascend, and as to which cities we ought to travel.’
Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
23 And since the word was pleasing to me, I sent from among you twelve men, one from each tribe.
Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
24 These, when they had set out and had ascended the mountains, arrived as far as the valley of the cluster of grapes. And having considered the land,
Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
25 having taken from its fruits in order to show its fertility, they brought these to us, and they said: ‘The land that the Lord our God will give to us is good.’
Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
26 Yet you were not willing to go there. Instead, being incredulous to the word of the Lord our God,
Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
27 you murmured in your tents, and you said: ‘The Lord hates us, and therefore he has led us away from the land of Egypt, so that he might deliver us into the hand of the Amorite and destroy us.
Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
28 To where should we ascend? The messengers have terrified our heart by saying: “The multitude is very great, and taller than us. And the cities are great, and the walls extend even to the sky. We have seen the sons of the Anakim there.”’
Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
29 And I said to you: ‘Do not be apprehensive, nor should you fear them.
Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
30 The Lord God himself, who is your leader, will fight on your behalf, just as he did in Egypt in the sight of all.
Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
31 And in the wilderness (as you yourselves saw), the Lord your God carried you, like a man who is accustomed to carrying his little son, along all the way that you walked, until you arrived at this place.’
na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
32 And yet, despite all of this, you did not believe the Lord your God,
Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
33 who went before you on the way, and who marked out the place where you should pitch your tents, showing you the way by fire in the night, and by a pillar of cloud in the day.
ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
34 And when the Lord had heard the voice of your words, becoming angry, he swore and said:
Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
35 ‘None of the men of this wicked generation will see the good land, which I have promised by oath to your fathers,
“Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
36 except Caleb the son of Jephuneh. For he himself will see it, and I will give the land on which he has walked to him and to his sons, because he has followed the Lord.’
isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
37 Neither is his indignation with the people a wonder, since the Lord also became angry with me because of you, and so he said: ‘Neither will you enter into that place.
Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
38 But Joshua, the son of Nun, your minister, shall himself enter on your behalf. Exhort and strengthen this man, and he himself shall divide the land by lot to Israel.
Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
39 Your little ones, about whom you said that they would be led away as captives, and your sons, who to this day are ignorant of the difference between good and evil, they shall enter. And I will give the land to them, and they will possess it.
Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
40 But as for you, turn back and go out to the wilderness, by way of the Red Sea.’
Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
41 And you responded to me: ‘We have sinned against the Lord. We will ascend and fight, just as the Lord our God has instructed.’ And having been equipped with weapons, when you were setting out for the mountain,
Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
42 the Lord said to me: ‘Say to them: Do not ascend and do not fight. For I am not with you. Otherwise, you may fall in the sight of your enemies.’
Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
43 I spoke, and you did not listen. But, opposing the order of the Lord, and swelling with pride, you ascended onto the mountain.
Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
44 And so, having gone forth, the Amorite, who was living in the mountains, came against you and pursued you, just as a swarm of bees would do. And he struck you down from Seir all the way to Hormah.
Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
45 And when you returned and were weeping in the sight of the Lord, he would not hear you, nor was he willing to agree to your voice.
Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
46 Therefore, you camped at Kadesh-barnea for a long time.”
Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.

< Deuteronomy 1 >