< Daniel 12 >

1 “But at that time Michael will rise up, the great leader, who stands up for the sons of your people. And a time will come, such as has not been from the time that nations began, even until that time. And, at that time, your people will be saved, all who will be found written in the book.
“Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
2 And many of those who sleep in the dust of the earth will awaken: some to everlasting life, and others to a reproach that they will always see.
Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
3 But those who have taught will shine like the brightness of the firmament, and those who instruct many towards justice, like the stars for unending eternity.
Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
4 But you, Daniel, close the message and seal the book, until the established time. Many will pass through, and knowledge will be increased.”
Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
5 And I, Daniel, looked, and behold, similarly two others stood up, one over here, on the bank of the river, and the other over there, on the other bank of the river.
Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
6 And I said to the man, who was clothed in linen, who stood over the waters of the river, “How long will it be until the end of these wonders?”
Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
7 And I heard the man, who was clothed in linen, who stood over the waters of the river, when he had lifted his right hand and his left hand up to heaven, and had sworn by He who lives forever, that it would be for a time, and times, and half a time. And when the dispersion of the hand of the holy people is completed, all these things will be completed.
Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
8 And I heard and did not understand. And I said, “My lord, what will be after these things?”
Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
9 And he said, “Go, Daniel, for the words are closed and sealed until the predetermined time.
Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
10 Many will be chosen and purified, and, as if by fire, they will be tested, and the impious will act impiously, and none of the impious will understand, yet the teachers will understand.
Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
11 And from the time when the continual sacrifice will be taken away and the abomination of desolation will be set up, there will be one thousand two hundred ninety days.
“Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
12 Blessed is he who waits and reaches until one thousand three hundred thirty-five days.
Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
13 But you, go, until the predetermined time, and you will rest and will stand in your allotted place at the end of days.
“Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”

< Daniel 12 >