< 2 Timothy 4 >

1 I testify before God, and before Jesus Christ, who shall judge the living and the dead through his return and his kingdom:
Ninakupa agizo hili lenye uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, atakaye wahukumu walio hai na wafu, na kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake:
2 that you should preach the word urgently, in season and out of season: reprove, entreat, rebuke, with all patience and doctrine.
Hubiri Neno. Uwe tayari kwa wakati ufaao na usiofaa. Waambie watu dhambi zao, kemea, himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho.
3 For there shall be a time when they will not endure sound doctrine, but instead, according to their own desires, they will gather to themselves teachers, with itching ears,
Kwa maana wakati utakuja ambao watu hawatachukuliana na mafundisho ya kweli. Badala yake, watajitafutia walimu wa kufundisha kulingana na tamaa zao. kwa njia hii masikio yao yatakuwa yametekenywa.
4 and certainly, they will turn their hearing away from the truth, and they will be turned toward fables.
Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli, na kugeukia hadithi.
5 But as for you, truly, be vigilant, laboring in all things. Do the work of an Evangelist, fulfilling your ministry. Show self-restraint.
Lakini wewe uwe mwaminifu katika mambo yote, vumilia magumu, fanya kazi ya mwinjilisti; timiza huduma yako.
6 For I am already being worn away, and the time of my dissolution presses close.
Kwa maana mimi tayari nimekwisha kumiminwa. Muda wa kuondoka kwangu umewadia.
7 I have fought the good fight. I have completed the course. I have preserved the faith.
Nimeshindana katika haki, Mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda.
8 As for the remainder, a crown of justice has been reserved for me, one which the Lord, the just judge, will render to me in that day, and not only to me, but also to those who look forward to his return.
Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu, ambayo Bwana, anayehukumu kwa haki, atanipa siku ile. Na siyo kwangu tu bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.
9 Hurry to return to me soon.
Jitahidi kuja kwagu haraka.
10 For Demas has abandoned me, out of love for this age, and he has departed for Thessalonica. Crescens has gone to Galatia; Titus to Dalmatia. (aiōn g165)
Kwa kuwa Dema ameniacha. Anaupenda ulimwengu wa sasa na amekwenda Thesalonike, Kreseni alikwenda Galatia, na Tito alikwenda Dalmatia. (aiōn g165)
11 Luke alone is with me. Take Mark and bring him with you; for he is useful to me in the ministry.
Luka tu ndiye yuko pamoja nami. Umchukue Marko uje naye kwani yeye ni muhimu kwangu katika huduma.
12 But Tychicus I have sent to Ephesus.
Nimemtuma Tikiko Efeso.
13 When you return, bring with you the supplies that I left with Carpus at Troas, and the books, but especially the parchments.
Lile joho ambalo nililiacha Troa kwa Karpo, utakapokuja lilete, pamoja na vile vitabu hasa vile vya ngozi.
14 Alexander the coppersmith has shown me much evil; the Lord will repay him according to his works.
Alekizanda mfua chuma alinitendea maovu mengi. Bwana atamlipa kulingana na matendo yake.
15 And you should also avoid him; for he has strongly resisted our words.
Nawe pia jihadhari naye, kwani aliyapinga sana maneno yetu.
16 At my first defense, no one stood by me, but everyone abandoned me. May it not be counted against them!
Katika utetezi wangu wa kwanza, hakuna mtu yeyote aliyesimama pamoja nami, badala yake, kila mmoja aliniacha. Mungu asiwahesabie hatia.
17 But the Lord stood with me and strengthened me, so that through me the preaching would be accomplished, and so that all the Gentiles would hear. And I was freed from the mouth of the lion.
Lakini Bwana alisimama pamoja nami, akanitia nguvu ili kwamba kupitia kwangu, neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia. Niliokolewa katika kinywa cha Simba.
18 The Lord has freed me from every evil work, and he will accomplish salvation by his heavenly kingdom. To him be glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
Bwana ataniepusha na matendo yote maovu na kuniokoa kwa ajili ya ufalme wake wa mbinguni. Utukufu uwe kwake milele na milele. Amen (aiōn g165)
19 Greet Prisca, and Aquila, and the household of Onesiphorus.
Msalimie Priska, Akila na nyumba ya Onesiforo.
20 Erastus remained at Corinth. And Trophimus I left sick at Miletus.
Erasto alibaki huko Korintho, lakini Trifimo nilimuacha Mileto akiwa mgonjwa.
21 Hurry to arrive before winter. Eubulus, and Pudens, and Linus, and Claudia, and all the brothers greet you.
Fanya hima uje kabla ya kipindi cha baridi. Eubulo anakusalimu, pia Pude, Lino, Claudia na ndugu wote.
22 May the Lord Jesus Christ be with your spirit. May grace be with you. Amen.
Mungu awe pamoja na roho yako, Neema iwe nawe.

< 2 Timothy 4 >