< 2 Thessalonians 2 >
1 But we ask you, brothers, concerning the advent of our Lord Jesus Christ and of our gathering to him,
Ndugu, kuhusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele zake, tunawasihi,
2 that you not be readily disturbed or terrified in your minds, by any spirit, or word, or epistle, supposedly sent from us, claiming that the day of the Lord is close by.
msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako.
3 Let no one deceive you in any way. For this cannot be, unless the apostasy will have arrived first, and the man of sin will have been revealed, the son of perdition,
Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.
4 who is an adversary to, and who is lifted up above, all that is called God or that is worshipped, so much so that he sits in the temple of God, presenting himself as if he were God.
Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.
5 Do you not recall that, when I was still with you, I told you these things?
Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya?
6 And now you know what it is that holds him back, so that he may be revealed in his own time.
Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia.
7 For the mystery of iniquity is already at work. And only one now holds back, and will continue to hold back, until he is taken from our midst.
Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa.
8 And then that iniquitous one shall be revealed, the one whom the Lord Jesus shall bring to ruin with the spirit of his mouth, and shall destroy at the brightness of his return:
Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa utukufu wa kuja kwake.
9 him whose advent is accompanied by the works of Satan, with every kind of power and signs and false miracles,
Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo,
10 and with every seduction of iniquity, toward those who are perishing because they have not accepted the love of truth, so that they may be saved.
na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.
11 For this reason, God will send to them works of deception, so that they may believe in lies,
Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo,
12 in order that all those who have not believed in the truth, but who have consented to iniquity, may be judged.
na wahukumiwe wote ambao hawakuiamini ile kweli, bali wamefurahia uovu.
13 Yet we must always give thanks to God for you, brothers, beloved of God, because God has chosen you as first-fruits for salvation, by the sanctification of the Spirit and by faith in the truth.
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli.
14 He has also called you into truth through our Gospel, unto the acquisition of the glory of our Lord Jesus Christ.
Kwa kusudi hili Mungu aliwaita kwa njia ya kuhubiri kwetu Injili, ili mpate kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo.
15 And so, brothers, stand firm, and hold to the traditions that you have learned, whether by word or by our epistle.
Hivyo basi, ndugu wapendwa, simameni imara na myashike sana yale mafundisho tuliyowapa ikiwa ni kwa maneno ya kinywa au kwa barua.
16 So may our Lord Jesus Christ himself, and God our Father, who has loved us and who has given us an everlasting consolation and good hope in grace, (aiōnios )
Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios )
17 exhort your hearts and confirm you in every good word and deed.
awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.