< 2 Samuel 12 >

1 Then the Lord sent Nathan to David. And when he had come to him, he said to him: “Two men were in one city: one wealthy, and the other poor.
Kisha Yahwe akamtuma Nathani kwa Daudi. Akaja kwake na kusema, “Kulikuwa na watu wawili katika mji. Mmoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa masikini.
2 The wealthy man had very many sheep and oxen.
Yule tajiri alikuwa na kundi la ng'ombe na kondoo wengi sana,
3 But the poor man had nothing at all, except one little sheep, which he had bought and nourished. And she had grown up before him, together with his children, eating from his bread, and drinking from his cup, and sleeping in his bosom. And she was like a daughter to him.
lakini maskini hakuwa na chochote isipokuwa mwanakondoo, aliyekuwa amemnunua na kumlisha na kumlea. Akakua pamoja naye na pamoja na watoto wake. Yule mwanakondoo hata alikula naye na kunywa kutoka katika kikombe chake, naye akalala katika mikono yake na alikuwa kama binti kwake.
4 But when a certain traveler had come to the wealthy man, neglecting to take from his own sheep and oxen, so that he might present a feast for that traveler, who had come to him, he took the sheep of the poor man, and he prepared a meal for the man who had come to him.”
Siku moja tajiri akapata mgeni, lakini yeye hakuwa tiyari kuchukua mnyama kutoka katika kundi lake la ng'ombe au kundi la kondoo ili kumwandalia chakula. Badala yake alichukua mwanakondoo wa masikini na akampika kwa ajili ya mgeni wake.
5 Then David’s indignation was enraged exceedingly against that man, and he said to Nathan: “As the Lord lives, the man who has done this is a son of death.
Hasira ya Daudi ikawaka dhidi ya tajiri yule, naye akamwambia Nathani kwa hasira, “Kama Yahwe aishivyo, mtu aliyelitenda jambo hili anastahili kufa.
6 He shall restore the sheep fourfold, because he did this word, and he did not take pity.”
Ni lazima alipe mwanakondoo mara nne zaidi kwa ajili ya kile alichokifanya, na kwa sababu hakuwa na huruma kwa mtu maskini.
7 But Nathan said to David: “You are that man. Thus says the Lord, the God of Israel: ‘I anointed you as king over Israel, and I rescued you from the hand of Saul.
Ndipo Nathani akamwambia Daudi, “Wewe ndiye yule mtu! Yahweh, Mungu wa Israeli, asema, 'Nilikutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli, na nilikuokoa kutoka katika mkono wa Sauli.
8 And I gave the house of your lord to you, and the wives of your lord into your bosom. And I gave the house of Israel and of Judah to you. And as if these things were small, I shall add much greater things to you.
Nikakupa nyumba ya bwana wako, na wake zake mikononi mwako. Nilikupa pia nyumba ya Israeli na Yuda. Na ikiwa hayo yalikuwa kidogo zaidi kwako, ningeweza kukuongezea mengine zaidi.
9 Therefore, why have you despised the word of the Lord, so that you did evil in my sight? You have struck down Uriah the Hittite with the sword. And you have taken his wife as a wife for yourself. And you have put him to death with the sword of the sons of Ammon.
Hivyo basi kwa nini umedharau maagizo ya Yahwe, hata ukafanya yaliyo maovu mbele zake? Umeua Uria Mhiti kwa upanga na umechukua mkewe kuwa mke wako. Uliua kwa upanga wa jeshi la Amoni.
10 For this reason, the sword shall not withdraw from your house, even perpetually, because you have despised me, and you have taken the wife of Uriah the Hittite, so that she may be your wife.’
Hivyo basi upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa kuwa umenidharau na umemchukua mke wa Uria mhiti kuwa mke wako.'
11 And so, thus says the Lord: ‘Behold, I will raise up over you an evil from your own house. And I will take your wives away before your eyes, and I will give them to your neighbor. And he will sleep with your wives in the sight of this sun.
Yahwe asema, 'Tazama, nitaleta maafa dhidi yako kutoka katika nyumba yako mwenyewe. Nitachukua wake zako, mbele ya macho yako na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako wakati wa mchana.
12 For you acted secretly. But I will do this word in the sight of all of Israel, and in the sight of the sun.’”
Kwa maana wewe ulitenda dhambi hii sirini, lakini mimi nitatenda jambo hili wakati wa mchana mbele za Israeli wote.
13 And David said to Nathan, “I have sinned against the Lord.” And Nathan said to David: “The Lord has also taken away your sin. You shall not die.
Ndipo Daudi alipomwambia Nathani, “Nimemtenda dhambi Yahwe.” Nathani akamjibu Daudi, “Yahwe naye ameiachilia dhambi yako. Hautakufa.
14 Yet truly, because you have given occasion to the enemies of the Lord to blaspheme, because of this word, the son who was born to you: dying he shall die.”
Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umemdharau Yahwe, mtoto aliyezaliwa kwako hakika atakufa.”
15 And Nathan returned to his own house. And the Lord struck the little one, whom the wife of Uriah had borne to David, and he was despaired of.
Kisha Nathani akaondoka na kwenda kwake. Yahwe akampiga mtoto ambaye mke wa Uria alimzaa kwa Daudi, naye akaugua sana.
16 And David begged the Lord on behalf of the little one. And David fasted strictly, and entering alone, he lay upon the ground.
Kisha Daudi akamwomba Mungu kwa ajili ya kijana. Daudi akafunga naye akaingia ndani na kulala usiku wote juu ya sakafu.
17 Then the elders of his house came, urging him to rise up from the ground. And he was not willing, nor would he eat a meal with them.
Wazee wa nyumba yake wakainuka na kusimama kando yake, ili wamwinue kutoka sakafuni. Lakini hakuinuka, na hakula pamoja nao.
18 Then, on the seventh day, it happened that the infant died. And the servants of David were afraid to report to him that the little one had died. For they said: “Behold, when the child was still alive, we were speaking to him, but he would not listen to our voice. How much more will he afflict himself, if we tell him that the boy is dead?”
Ikawa siku ya saba mtoto akafa. Watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia kwamba mtoto amekufa, kwa maana walisema, “Tazama, wakati mtoto alipokuwa hai tuliongea naye, lakini hakuisikiliza sauti yetu. Atakuwaje ikiwa tutamwambia kwamba kijana amekufa?!”
19 But when David had seen his servants whispering, he realized that the infant had died. And he said to his servants, “Is the child dead?” And they responded to him, “He is dead.”
Daudi alipoona kwamba watumishi wake walikuwa wakinong'onezana, Akatambua kwamba mtoto amekufa. Akawauliza, “Je mtoto amekufa?” Wakajibu, “Amekufa.”
20 Therefore, David rose up from the ground. And he washed and anointed himself. And when he had changed his clothing, he entered the house of the Lord, and he worshiped. Then he went to his own house, and he asked them to place bread before him, and he ate.
Kisha Daudi akainuka kutoka sakafuni naye akaoga, akajipaka mafuta, na kubadili mavazi yake. Akaenda katika hema la kukutania na akaabudu pale, kisha akarudu katika kasri lake. Akataka chakula kiletwe, wakamwandalia, naye akala.
21 But his servants said to him: “What is this word that you have done? You fasted and were weeping, on behalf of the infant, while he was still alive. But when the boy was dead, you arose and ate bread.”
Ndipo watumishi wake walipomwambia, “Kwa nini umefanya jambo hili? Ulifunga na kulia kwa ajili ya mtoto wakati alipokuwa hai, lakini mtoto alipokufa, ukainuka na kula.”
22 And he said: “While he was yet alive, I fasted and wept on behalf of the infant. For I said: Who knows if the Lord may perhaps give him to me, and let the infant live?
Daudi akajibu, “Wakati mtoto alipokuwa hai nilifunga na kulia. Nilisema, Ni nani ajuaye kwamba Yahwe angeweza kunihurumia mtoto akaishi au sivyo?
23 But now that he is dead, why should I fast? Would I be able to bring him back anymore? Instead, I will go to him. Yet truly, he will not return to me.”
Lakini sasa amekufa, hivyo nifungie nini? Je naweza kumrudisha tena? Nitakwenda kwake, lakini yeye hawezi kunirudia.”
24 And David consoled his wife Bathsheba. And entering to her, he slept with her. And she bore a son, and he called his name Solomon, and the Lord loved him.
Daudi akamfariji Bethsheba mkewe, akaingia kwake, na akalala naye. Baadaye akazaa mtoto wa kiume, naye akaitwa Selemani. Yahwe akampenda
25 And he sent, by the hand of Nathan the prophet, and he called his name, Beloved of the Lord, because the Lord loved him.
naye akatuma neno kupitia nabii Nathani kumwita Yedidia, kwa sababu Yahwe alimpenda.
26 And then Joab fought against Rabbah of the sons of Ammon, and he fought outside the royal city.
Basi Yoabu akapigana na Raba, mji wa kifalme wa watu wa Amoni, naye akaiteka ngome yake.
27 And Joab sent messengers to David, saying: “I have struggled against Rabbah, and so the City of Waters will soon be seized.
Hivyo Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi na kusema, “Nimepigana na Raba, nami nimeshikilia sehemu inayosambaza maji ya mji.
28 Now therefore, gather the remaining portion of the people together, and besiege the city and take it. Otherwise, when the city will have been laid waste by me, the victory will be ascribed to my name.”
Kwa hiyo sasa likusanye jeshi lililosalia uhuzingire mji na kuuteka, kwa maana ikiwa nitauteka, utaitwa kwa jina langu.”
29 And so David gathered together all the people, and he set out against Rabbah. And after he had fought, he seized it.
Hivyo Daudi akalikusanya jeshi lote na kwenda Raba; akapigana nao na kuuteka.
30 And he took the crown of their king from his head. The weight of it was a talent of gold, having the most precious gems. And it was placed upon the head of David. Moreover, he carried away the spoils of the city, which were very many.
Daudi akachukua taji ya dhahabu kutoka katika kichwa cha mfalme wao iliyokuwa na uzito wa talanta, na ilikuwa na jiwe la thamani ndani yake. Taji ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Kisha akachukua nyara za mji kwa wingi.
31 Also, bringing forth its people, he sawed them, and he drove over them with iron wagons, and he divided them with knives, and he dragged them through brick kilns. So he did to all the citizens of the sons of Ammon. And David returned, with the entire army, to Jerusalem.
Akawatoa watu waliokuwa mjini naye akawalazimisha kufanya kazi kwa misumeno, sululu na shoka; lakini pia akawalazimisha kutengeneza matofali. Daudi akailazimisha miji yote ya watu wa Amoni kufanya kazi hiyo. Kisha Daudi na jeshi lote wakarudi Yerusalemu

< 2 Samuel 12 >