< 2 Chronicles 26 >

1 Then all the people of Judah appointed his son, Uzziah, who was sixteen years old, as king in place of his father, Amaziah.
Watu wote wa Yuda wakamchukua Uzia, ambaye alikuwa na aumri wa mika kumi na sita, na wakamfanya mfalme katika nafasi ya baba yake Amazia.
2 He built up Eloth, and he restored it to the dominion of Judah. After this, the king slept with his fathers.
Ndiye aliuyeijenga tena Elathi na kuurejesha kwa Yuda. Baada ya hapo mfalme akalala pamoja na babu zake.
3 Uzziah was sixteen years old when he had begun to reign. And he reigned for fifty-two years in Jerusalem. The name of his mother was Jecoliah, from Jerusalem.
Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala. Akatawala miaka ishirini na mabili katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Yekolia; alikuwa wa Yerusalemu.
4 And he did what was right in the eyes of the Lord, in accord with all that his father, Amaziah, had done.
Akafanya yaliyokuwa sahihi katika macho ya Yahwe, akiufuata mfano wa baba yake, katika kila jamabo.
5 And he sought the Lord, during the days of Zechariah, who understood and saw God. And while he was seeking the Lord, he directed him in all things.
Alijitoa kumtafuta Mungu katiaka siku za Zekaria, ambaye alimpa maelekezo kwa ajili ya kumtii Mungu. Kadri alivyomtafuta Yaahwe, Mungu alimfanikisha.
6 Indeed, he went out and fought against the Philistines. And he destroyed the wall of Gath, and the wall of Jabneh, and the wall of Ashdod. Also, he built towns in Ashdod, and among the Philistines.
Uzia akaenda na kupigana zidi ya Wafilisti. Akaubomoa ukuta wa mji wa Gathi, Yabne, na Ashdodi; akajenga miji katika nchi ya Ashdodi na miongoni mwa Wafilisti.
7 And God helped him against the Philistines, and against the Arabians, who were living in Gurbaal, and against the Ammonites.
Mungu aakaamsaidia zidi ya Wafilist, zidi ya Waarabu waliokuwa wakiishi Gur - baali, na zidi ya Wameuni.
8 And the Ammonites weighed out gifts to Uzziah. And his name became widely known, even to the entrance of Egypt, because of his frequent victories.
Waamoni wakalipa kodi kwa Uzia, na umaarufu wake ukaenea, hata kufika maingilio ya Misiri, kwa sababu alikuwa ameanza kuwa maarufu.
9 And Uzziah built towers in Jerusalem, above the gate of the corner, and above the gate of the valley, and others on the same side of the wall, and he fortified them.
Zaidi ya hayo, Uzia akajenga minara katika Yerusalemu katika kona ya Lango, kwenye Lango la Bonde, na pa kwenye kona ya ukuta, na akavizungushia ngome.
10 Then he also constructed towers in the wilderness, and dug many cisterns, because he had much cattle, both in the plains and in the starkness of the wilderness. Also, he had vineyards and dressers of vines in the mountains and at Carmel. Certainly, he was a man devoted to agriculture.
Akajenga minara ya ulinzi katika nyika na akachimba mabwawa, kwa maana alikuwa na ng'ombe wengi, katika visiwa vya chini na katika nchi tambarare. Alikuwa na wakulima na wapandaji wa zabibu katika mwinuko wa nchi na katika mashamba yenye rutuba, kwa maana alipenda kulima.
11 Now the army of his warriors, who would go forth to battle, was under the hand of Jeiel, the scribe, and Maaseiah, the teacher, and under the hand of Hananiah, who was among the king’s commanders.
Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi la wanaume wa kupigana vita ambao walienda vitani katika makundi ambayo idadi yake ilikuwa imehesabiwa na Yeieli, mwandishi. na Maaseya, afisa, chini ya mamlaka ya Hanania, mmoja wa maamri jeshi wa mfalme.
12 And the entire number of the leaders, by the families of strong men, was two thousand six hundred.
Jumla ya wakuu wa nyumba za mababu, watu wa kupigana vita, walikuwa 2, 600.
13 And the entire army under them was three hundred and seven thousand five hundred, who were fit for war, and who fought on behalf of the king against the adversaries.
Chini ya mkono wao kulikuwa na jeshi la watu 307, 500 ambao walifanya vita kwa nguvu ili kumsaidia mfalme idi ya maadui.
14 Also, Uzziah prepared for them, that is, for the entire army, shields, and spears, and helmets, and breastplates, and bows, as well as slings for the casting of stones.
Uzia akaandaa kwa ajili yao—kwa ajili ya jeshi lote — ngao, mikuki, chapeo, deraya za majini, nyuta, na mawe ya kurusha.
15 And in Jerusalem, he made various kinds of machines, which he placed in the towers, and at the corners of the walls, so as to shoot arrows and large stones. And his name went forth to far away places, for the Lord was helping him and had strengthened him.
Katka Yerusalemu alijenga mitambo, iliyobuniwa na watu wenye ujuzi, ili iwe juu ya minara na juu ya buruji, kwa ajili ya kurushia mishale na mawe makaubwa. Umaarufu wake ukaenea hadi nchi za mbali, kwa maana alisaidiwa sana hadi alipokuwa na ngavu sana.
16 But when he had become strong, his heart was lifted up, even to his own destruction. And he neglected the Lord his God. And entering into the temple of the Lord, he intended to burn incense upon the altar of incense.
Lakini Uzia alipokuwa amekuwa na nguvu nyingi, moyo wake ulijiinua akatenda kwa uovu; akafanya makosa zidi ya Yahwe, Mungu wake, kwa maana alienda kwenye nyumba ya Yahwe kwa ajili ya kufukiza uvumba juu ya madhabahu ya kufukizia.
17 And entering immediately after him, Azariah the priest, and with him eighty priests of the Lord, very valiant men,
Azaria, kuhani, akamfuata, na pamoja naye makuhanai themanini wa Yahwe, ambao walikuwa watu wenye ujasiri.
18 withstood the king, and they said: “It is not your office, Uzziah, to burn incense to the Lord; rather, it is the office of the priests, that is, of the sons of Aaron, who have been consecrated for this same ministry. Depart from the sanctuary, otherwise you will be in contempt. For this act will not be reputed to you for your glory by the Lord God.”
Walimzuia Uzia, mfalme, na wakasema kwake, “Siyo jukumu lako, Uzia, kumtolea Yahwe uvumba, bali ni kazi ya makuhani, wana wa Haruni, amabao wametengwa kwa ajili ya kutoa sadaka za uvumba. Toka nje ya sehemu takatifu, kwa maana huna uaminifu na hautaheshimiwa na Yahwe Mungu.”
19 And Uzziah, having become angry, while holding in his hand the censer so that he might burn incense, threatened the priests. And immediately a leprosy arose on his forehead, in the sight of the priests, in the house of the Lord, at the altar of incense.
Kisha Uzia akakasirika. Alikuwa ameshikilia chetezo mkononi kwa ajili ya kufukiza uvumba. Wakati alipowaghadhabikia makuhani, ukoma ukatokea juu ya uso wake mbele ya makuhani katika nyumba ya Yahwe, pembeni mwa madhabahu ya uvumba.
20 And when the high priest Azariah, and all the rest of the priests, had gazed upon him, they saw the leprosy on his forehead, and they hurried to expel him. Then too, he himself, becoming terrified, rushed to depart, because immediately he had become aware of the wound of the Lord.
Azaria kuhani mkuu na makuhani wote wakamwanagalia, na, tazama, alikuwa amepatwa ukoma juu ya uso wake. Walimwondoa pale haraka. Kwa hakika, aliharakisha kwenda nje, kwa maana Yahwe alikuwa amempiga.
21 And so, king Uzziah was a leper, even until the day of his death. And he lived in a separate house, being full of leprosy, because of which he had been ejected from the house of the Lord. Then Jotham, his son, directed the house of the king, and he was judging the people of the land.
Uzia, mfalme, alikuwa mwenye ukoma hadi siku ya kufa kwake na aliishi katika nyumba ya kutengwa tangu alipokuwa mwenye ukoma, kwa maan alitengwa na nyumba ya Yahwe. Yothamu, mwanaye, alikuwa mkuu wa anyumba ya mfalme na aliwatawala watu wa nchi.
22 But the rest of the words of Uzziah, the first and the last, were written by the prophet Isaiah, the son of Amoz.
Mambo mengine kuhusu Uzia, mwanzo na mwisho, yako katika kile ambacho Isaya, mwana wa Amozi, nabii, aliandika.
23 And Uzziah slept with his fathers. And they buried him in the field of the royal sepulchers, because he was a leper. And Jotham, his son, reigned in his place.
Kwa hiyo Uzia akalala pamoja na babu zake; walimzka pamoja na babu zake katika uwanja wa maziko wa Mfalme, kwa maana walisema, “Ni mwenye ukoma”. Yothamu, mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake.

< 2 Chronicles 26 >