< 1 Samuel 27 >
1 And David said in his heart: “At some time, I will one day fall into the hands of Saul. Is it not better if I flee, and be saved in the land of the Philistines, so that Saul may despair and cease to seek me in all the parts of Israel? Therefore, I will flee away from his hands.”
Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
2 And David rose up and went away, he and the six hundred men who were with him, to Achish, the son of Maoch, the king of Gath.
Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
3 And David lived with Achish at Gath, he and his men: each man with his household, and David with his two wives, Ahinoam, the Jezreelite, and Abigail, the wife of Nabal of Carmel.
Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
4 And it was reported to Saul that David had fled to Gath. And so, he did not continue to seek him.
Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
5 And David said to Achish: “If I have found favor in your eyes, let a place be given to me in one of the cities of this region, so that I may live there. For why should your servant stay in the city of the king with you?”
Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
6 And so, Achish gave Ziklag to him on that day. And for this reason, Ziklag belongs to the kings of Judah, even to this day.
Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
7 Now the number of days that David lived in the region of the Philistines was four months.
Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
8 And David and his men went up and took plunder from Geshuri, and from Girzi, and from the Amalekites. For in the land long ago, these were the inhabitants of the area, going from Shur as far as the land of Egypt.
Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
9 And David struck the entire land. Neither did he leave alive man or woman. And he took away the sheep, and the oxen, and the donkeys, and the camels, and the garments. And he returned and went to Achish.
Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
10 Then Achish said to him, “Whom did you go out against today?” And David responded, “Against the south of Judah, and against the south of Jerahmeel, and against the south of Keni.”
Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
11 Neither man nor woman was left alive by David. Neither did he lead back any of them to Gath, saying, “Lest perhaps they may speak against us.” David did these things. And this was his decision during all the days that he lived in the region of the Philistines.
Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
12 Therefore, Achish trusted David, saying: “He has worked much harm against his people Israel. And so, he will be a servant to me forever.”
Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”