< 1 Kings 18 >

1 After many days, the word of the Lord came to Elijah, in the third year, saying, “Go and show yourself to Ahab, so that I may grant rain upon the face of the earth.”
Kwa hiyo baada ya siku nyingi neno la BWANA likamjia Eliya, katika mwaka wa tatu wa ukame, likisema, “Nenda ukajionyeshe mwenyewe kwa Ahabu nami nitainyeshea ardhi mvua.”
2 Therefore, Elijah went to show himself to Ahab. For there was a severe famine in Samaria.
Eliya akaenda kujionyesha mwenyewe kwa Ahabu; sasa njaa ilikuwa kali sana kule Samaria.
3 And Ahab called Obadiah, the manager of his household. Now Obadiah feared the Lord greatly.
Ahabu akamwita Obadia, aliyekuwa mkuu wa ikulu. Obadia alimheshimu sana BWANA,
4 For when Jezebel was killing the prophets of the Lord, he took one hundred prophets, and concealed them, fifty and fifty, in caves. And he fed them with bread and water.
kwa kuwa wakati Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa BWANA, Obadia alichukua manabii mia akawaficha katika makundi ya hamsini hamsini katika pango na akawalisha kwa mikate na maji.
5 Then Ahab said to Obadiah, “Go into the land, to all fountains of water, and to all the valleys, for perhaps we will be able to find plants, and save the horses and mules, so that the beasts of burden may not perish entirely.”
Ahabu akamwambia Obadia, “Pita katika nchi yote na katika chemichemi zote za maji na vijito. Yamkini tunaweza kupata maji na nyasi ili tuwaokoa hawa farasi na nyumbu, ili tusiwakose wanyama wote.”
6 And they divided the regions among themselves, so that they might travel through them. Ahab went one way alone, and Obadiah went another way by himself.
Kwa hiyo wakaigawa nchi kati yao ili wapite kati yake wakitafuta maji. Ahabu akaenda njia yake mwenyewe na Obadia naye akaenda njia yake.
7 And while Obadiah was on the way, Elijah met him. And when he had recognized him, he fell on his face, and he said, “Are you not my lord Elijah?”
Wakati Obadia akiwa njiani, akakutana na Eliya pasipo kutegemea. Obadia akamtambua na akalala kifudifudi chini. Akamwambia, “Ndiye wewe, bwana wangu Eliya?”
8 And he responded to him: “I am. Go and tell your lord that Elijah is here.”
Naye Eliya akamjibu, Ni mimi. Nenda umwambie bwana wako, 'Tazama, Eliya yuko hapa.'”
9 And he said: “How have I sinned that you would deliver me, your servant, into the hand of Ahab, so that he would put me to death?
Obadia akamjibu. “Nimekoseaje, kwamba umtoe mtumishi wako katika mkono wa Ahabu ili aniue?
10 As the Lord your God lives, there is no nation or kingdom to which my lord has not sent, seeking you. And when all responded, ‘He is not here,’ he swore each kingdom and nation to an oath, because you were not found at all.
Kama BWANA Mungu wako aishivyo, hakuna taifa wala ufalme ambapo bwana wangu hajatuma watu kukutafuta. Kila taifa au ufalme unaposema, “Eliya hayuko hapa,' Ahabu hufanya waape ni kweli hawajakuona.
11 And now, you say to me, ‘Go and tell your lord that Elijah is here.’
Na sasa wewe unasema, 'Nenda, ukamwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa.'
12 And when I will have departed from you, the Spirit of the Lord will transport you to a place that I do not know. And entering, I will report to Ahab. And he, not finding you, will put me to death. Yet your servant has feared the Lord from his infancy.
Mara tu baada ya kukuacha Roho wa BWANA atakuchukua na kukupeleka mahali ambapo sitapajua. Kisha nikienda na kumwambia Ahabu, na asipokuona, ataniua. Bado, mimi, mtumishi wako, nimekuwa nikimwabudu BWANA kutoka ujana wangu.
13 Has it not been revealed to you, my lord, what I did when Jezebel was killing the prophets of the Lord: how I hid one hundred men from the prophets of the Lord, fifty and fifty, in caves, and how I fed them with bread and water?
Je, haujaambiwa, bwana wangu, nilichokifanya wakati Yezebeli alipowaua manabii wa BWANA, jinsi nilivyowaficha wale manabii mia moja wa BWANA katika makundi ya hamsini kwenye pango na kuwalisha kwa mikate na maji?
14 And now you say: ‘Go and tell your lord that Elijah is here,’ so that he may kill me!”
Na sasa unasema, 'Nenda umwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa,' kwa hiyo ataniua.”
15 And Elijah said, “As the Lord of hosts lives, before whose face I stand, this day I will appear to him.”
Ndipo Eliya alipomjibu, “Kama vile BWANA wa majeshi aishivyo, ambaye mimi ninasimama, Kwa hakika nitajionyeshakwa Ahabu leo.”
16 Therefore, Obadiah went away to meet Ahab, and he reported to him. And Ahab went to meet Elijah.
Kwa hiyo Obadia akaenda kukutana na Ahabu, nakumwambia kile Eliya alichokuwa amemwambia. Ndipo mfalme alipoenda kukutana na Eliya.
17 And when he had seen him, he said, “Are you the one who is disturbing Israel?”
Ahabu alipomwona Eliya, akamwambia, “Je, ni wewe? Wewe mtabishaji wa Israeli!”
18 And he said: “I have not troubled Israel. But it is you, and the house of your father, who have abandoned the commandments of the Lord, and have followed the Baals.
Eliya akamwambia, “Mimi sijaitabisha Israeli, Lakiini wewe na familia ya baba yako ndio watabishaji kwa kuziacha amri za BWANA na kufuata sanamu za Baali.
19 Yet truly now, send and gather to me all of Israel, on Mount Carmel, with the four hundred and fifty prophets of Baal, and the four hundred prophets of the sacred groves, who eat from the table of Jezebel.”
Kwa hiyo sasa, Tuma neno na unikusanyie Israeli yote katika mlima Kameli, pamoja na manabii 450 wa Baali na wale manabii 400 wa Ashera wanaokula kwenye meza ya Yezebeli.”
20 Ahab sent to all the sons of Israel, and he gathered together the prophets on mount Carmel.
Kwa hiyo Ahabu akatuma neno kwa watu wote wa Israeli na akawakusanya manabii wote kwenye mlima Kameli.
21 Then Elijah, drawing near to all the people, said: “How long will you waver between two sides? If the Lord is God, follow him. But if Baal is, then follow him.” And the people did not respond a word to him.
Eliya akaja karibu na watu wote akasema, “Mtaendelea kubadilisha mawazo yenu mpaka lini? Kama BWANA ni Mungu, mfuateni yeye, Lakini kama Baali ni Mungu, basi mfuateni yeye,” Lakini watu hawakumjibu neno.
22 And Elijah said again to the people: “I alone remain as a prophet of the Lord. But the prophets of Baal are four hundred and fifty men.
Kisha Eliya akawaambia wale watu, “Mimi, pekee yangu, ndiye niliyebaki kuwa nabii wa BWANA, lakini manabii wa Baali wako 450.
23 Let two oxen be given to us. And let them choose one ox for themselves, and, cutting it into pieces, let them set it on the wood. But they may not place fire under it. And I will prepare the other ox, and set it on the wood. But I will not place fire under it.
Hebu tutoleeni ng'ombe wawili. Nao wajichagulie ng'ombe mmoja na wamchinje na kumkatakata katika vipnde, na wamweke kwenye kuni, na wasitie moto chini yake. Nami nitamwandaa yule wa pili na kumweke juu ya kuni nami sitatia moto chini yake.
24 Call upon the names of your gods. And I will call on the name of my Lord. And the God who will have heeded with fire, let him be God.” And in response, all the people said, “Excellent proposition.”
Kisha mtaliita jina la mungu wenu, nami nitaliita jina la BWANA, na Mungu atakayejibu kwa moto, huyo ndiye Mungu.” Watu wote wakajibu na kusema, “Hilo ni jambo jema.”
25 Then Elijah said to the prophets of Baal: “Choose for yourselves one ox, and prepare it first. For you are many. And call on the names of your gods, but do not place fire under it.”
Kwa Eliya akawaambia manabii wa Baali, “Chagueni ng'ombe mmoja kwa ajili yenu na mwe wa kwanza kumwamdaa, kwa kuwa ninyi ni wengi, Kisha liiteni jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
26 And when they had taken an ox, which he had given to them, they prepared it. And they called on the name of Baal, from morning even until midday, saying, “O Baal, heed us.” And there was no voice, nor did anyone respond. And so they leaped upon the altar that they had made.
Nao wakamchukua yule ng'ombe waliokuwa wamepewa na wakamwandaa, na ndipo walipoliita jina la Baali kuanzia asubuhi hadi adhuhuri, wakisema, “Baali, tusikie.” Lakini hapakuwepo na Sauti, na wala hakuna aliyejibu. Wakachezacheza kuizunguka madhabahu waliyotengeneza.
27 And when it was now midday, Elijah ridiculed them, saying: “Cry out with a louder voice. For he is a god, and perhaps he is talking, or at an inn, or on a journey, or certainly he may be asleep, and must be awakened.”
Ilipofika adhuhuri Eliya akawakejeli akisema, “Mwiteni kwa nguvu! Huyo ni mungu! labda anawaza kitu, au amepumzika, au yuko safarini, au pengine amelala sharti aamshwe.”
28 Then they cried out with a loud voice, and they cut themselves, in accord with their ritual, with knives and lancets, until they were entirely covered in blood.
Kwa hiyo wakamwita kwa nguvu, wakajikatakata kama kawaida yao ilivyokuwa, kwa upanga na nyembe, mpaka damu ikawachuruzika.
29 Then, after midday had passed, and they were prophesying, the time had arrived when the sacrifice is usually offered. And there was no voice heard, neither did anyone heed or respond to the praying.
Ikawa wakati wa adhuhuri ulipopita, na bado walikuwa wakiendelea kutabiri mpaka wakati wa jioni wa kutoa dhabihu, lakini hapakuwepo na sauti wala mtu wa kuwajibu; wala hapakuwepo na yeyote wa kujibu wala wa kuangalia.
30 Elijah said to all the people, “Draw near to me.” And as the people were drawing near to him, he repaired the altar of the Lord, which had been torn down.
Kisha Eliya akawaambia watu wote, “Nisogeleeni,” na watu wote wakamsogelea. Naye akatengeneza ile madhabahu ya BWANA ambayo ilikuwa imeharibika.
31 And he took twelve stones, in accord with the number of the tribes of the sons of Jacob, to whom the word of the Lord came, saying, “Israel shall be your name.”
Eliya akachukua mawe kumi na mawili, kila jiwe moja liliwakilisha kabila moja la wana wa Yakobo - ni kupitia Yakobo kwamba neno la BWANA lilikuja, likisema, “Jina lako litakuwa Israel.”
32 And he built from the stones an altar to the name of the Lord. And he made a trench for water, like two furrows of plowed land, all around the altar.
Kwa kutumia hayo mawe aliijenga ile madhabahu kwa jina la BWANA na akachimba mfereji kuizunguka ile madhabahu kubwa kiasi cha kubeba lita kumi na tano za maji.
33 And he arranged the wood, and he cut the ox into pieces, and he placed it on the wood.
Kisha akaweka kuni kwa ajili ya moto na akamkatakata yule ng'ombe katika vipande vipande na akaweka vile vipande juu ya kuni. Na akasema, “Vijazeni maji hivyo vyombo na yamwageni kwenye hiyo sadaka ya kueketezwa na juu ya hizo kuni.”
34 And he said, “Fill four containers with water, and pour it over the holocaust, and over the wood.” And again, he said, “Do this a second time.” And when they had done it a second time, he said, “Do it also a third time.” And they did so a third time.
Akasema tena fanyeni hivyo mara ya pili,” nao wakafanya kwa mara ya pili. kisha akasema, “Fanyeni mara ya tatu,” nao wakafanya kwa mara ya tatu.
35 And the water was running down around the altar, and the pit of the trench was filled with water.
Maji yakaizunguka ile madhabahu na kuujaza ule mfereji.
36 And when it was now time for the holocaust to be offered, the prophet Elijah, drawing near, said: “O Lord, God of Abraham, and Isaac, and Israel, reveal this day that you are the God of Israel, and that I am your servant, and that I have acted, in all these things, in accord with your precept.
Ikawa wakati wa kutoa dhabihu ya jioni, nabii Eliya akasogea na akasema, “BWANA, Mungu wa Abrahamu, na wa Isaka, na wa Israeli, na ijulikane leo kwamba wewe ndiye Mungu wa Israeli, na kwamba mimi ni mtumishi wako, na kwamba nimeyafanya mambo haya yote kwa jina lako.
37 Heed me, O Lord, heed me, so that this people may learn that you are the Lord God, and that you have converted their heart again.”
Nisikie, BWANA, nisike, ili hawa watu wajue kuwa wewe, BWANA, ndiye Mungu, na kwamba umeirudisha mioyo yao kwako tena.”
38 Then the fire of the Lord fell down and devoured the holocaust, and the wood, and the stones, and even the dust, and it absorbed the water that was in the trench.
Ndipo moto wa BWANA ukashuka ukairamba ile sadaka, pamoja na zile kuni, mawe na mavumbi, na kuyaramba yale maji yaliyokuwa kwenye ule mfereji.
39 And when all the people had seen it, they fell upon their face, and they said: “The Lord himself is God! The Lord himself is God!”
watu wote walipoona haya, wakalala kifudifudi chini wakasema, “BWANA, ndiye Mungu! BWANA ndiye Mungu!
40 And Elijah said to them, “Apprehend the prophets of Baal, and do not let even one of them escape.” And when they had apprehended them, Elijah led them down to the torrent Kishon, and he put them to death there.
Kwa hiyo Eliya akawaambia, “Wakamateni manabii wa Baali. Msimwache hata mmoja wao atoroke.” Kwa hiyo wakawakamata, na Eliya akawaleta manabii wa Baali chini kwenye kijito cha Kishoni na akawaua huko.
41 And Elijah said to Ahab “Ascend; eat and drink. For there is the sound of an abundance of rain.”
Eliya akamwambia Ahabu, “Inuka, ule na kunywa, kwa kuwa kuna sauti ya mvua kubwa.”
42 Ahab ascended, so that he might eat and drink. But Elijah ascended to the top of Carmel, and bending down to the ground, he placed his face between his knees.
Kwa hiyo Ahabu akaenda akala na knywa. Kisha Eliya akaenda juu ya mlima Kameli, akasudu chini na akaweka uso wake katikati ya magoti.
43 And he said to his servant, “Ascend, and gaze out toward the sea.” And when he had ascended, and had contemplated, he said, “There is nothing.” And again, he said to him, “Return seven times.”
Akamwambia mtumishi wake, “Nenda sasa, utazame upande wa bahari.” mtumishi wake akaenda na akasema, “Hakuna kitu,” Eliya akamwambia, “Nenda tena, mpaka mara saba.”
44 And at the seventh time, behold, a little cloud ascended from the sea like the footstep of a man. And he said: “Ascend, and say to Ahab, ‘Yoke your chariot, and descend; otherwise, the rain may prevent you.’”
Ile mara ya saba mtumishi wake akasema, “Tazama, kuna wingu linapanda kutoka baharini, ni dogo kama mkono wa mtu.” Eliya akamjibu, Nenda ukamwambie Ahabu, 'Andaa gari lako na ushuke kabla mvua haijakuzuia.'”
45 And as he was turning himself this way and that, behold, the heavens were darkened, and there were clouds and wind, and a great rainstorm occurred. And so Ahab, going up, went away to Jezreel.
Ikatokea baada ya muda mfupi mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, na kulikuwa na mvua kubwa. Ahabu akapanda gari akaenda zake Yezreeli,
46 And the hand of the Lord was upon Elijah. And cinching his waist, he ran before Ahab, until he arrived at Jezreel.
lakini mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Eliya. Akalikaza vazi lake kwa mshipi wake na akakimbia mbele ya Ahabu kwenye lango la Yezreeli.

< 1 Kings 18 >