< 1 Corinthians 3 >
1 And so, brothers, I was not able to speak to you as if to those who are spiritual, but rather as if to those who are carnal. For you are like infants in Christ.
Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2 I gave you milk to drink, not solid food. For you were not yet able. And indeed, even now, you are not able; for you are still carnal.
Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3 And since there is still envy and contention among you, are you not carnal, and are you not walking according to man?
Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4 For if one says, “Certainly, I am of Paul,” while another says, “I am of Apollo,” are you not men? But what is Apollo, and what is Paul?
Mmoja wenu anaposema, “Mimi ni wa Paulo”, na mwingine, “Mimi ni wa Apolo”, je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5 We are only the ministers of him in whom you have believed, just as the Lord has granted to each of you.
Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6 I planted, Apollo watered, but God provided the growth.
Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7 And so, neither he who plants, nor he who waters, is anything, but only God, who provides the growth.
Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8 Now he who plants, and he who waters, are one. But each shall receive his proper reward, according to his labors.
Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9 For we are God’s assistants. You are God’s cultivation; you are God’s construction.
Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10 According to the grace of God, which has been given to me, I have laid the foundation like a wise architect. But another builds upon it. So then, let each one be careful how he builds upon it.
Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11 For no one is able to lay any other foundation, in place of that which has been laid, which is Christ Jesus.
Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12 But if anyone builds upon this foundation, whether gold, silver, precious stones, wood, hay, or stubble,
Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13 each one’s work shall be made manifest. For the day of the Lord shall declare it, because it will be revealed by fire. And this fire will test each one’s work, as to what kind it is.
Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14 If anyone’s work, which he has built upon it, remains, then he will receive a reward.
Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15 If anyone’s work is burned up, he will suffer its loss, but he himself will still be saved, but only as through fire.
lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16 Do you not know that you are the Temple of God, and that the Spirit of God lives within you?
Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17 But if anyone violates the Temple of God, God will destroy him. For the Temple of God is holy, and you are that Temple.
Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18 Let no one deceive himself. If anyone among you seems to be wise in this age, let him become foolish, so that he may be truly wise. (aiōn )
Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli. (aiōn )
19 For the wisdom of this world is foolishness with God. And so it has been written: “I will catch the wise in their own astuteness.”
Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: “Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao.”
20 And again: “The Lord knows the thoughts of the wise, that they are vain.”
Na tena: “Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai.”
21 And so, let no one glory in men.
Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22 For all is yours: whether Paul, or Apollo, or Cephas, or the world, or life, or death, or the present, or the future. Yes, all is yours.
Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23 But you are Christ’s, and Christ is God’s.
Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.