< 1 Chronicles 7 >

1 Now the sons of Issachar were Tola and Puah, Jashub and Shimron, four.
Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
2 The sons of Tola: Uzzi, and Rephaiah, and Jeriel, and Jahmai, and Ibsam, and Shemuel, leaders according to the houses of their kindred. From the stock of Tola, there were numbered, in the days of David, twenty-two thousand six hundred very strong men.
Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
3 The sons of Uzzi: Izrahiah, from whom were born: Michael, and Obadiah, and Joel, and Isshiah; all five were leaders.
Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
4 And with them, by their families and peoples, there were thirty-six thousand very strong men, girded for battle. And they had many wives and children.
Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
5 Also, their brothers, throughout all the kindred of Issachar, were numbered as eighty-seven thousand, very fit for battle.
Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
6 The sons of Benjamin: Bela, and Becher, and Jediael, three.
Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
7 The sons of Bela: Ezbon, and Uzzi, and Uzziel, and Jerimoth and Iri, five leaders of families, also very fit for battle; and their number was twenty-two thousand thirty-four.
Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
8 Now the sons of Becher: Zemirah, and Joash, and Eliezer, and Elioenai, and Omri, and Jeremoth, and Abijah, and Anathoth, and Alemeth: all these were sons of Becher.
Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
9 And they were numbered according to their families, by the leaders of their kindred, very strong in warfare, twenty thousand and two hundred.
Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
10 And the sons of Jediael: Bilhan, and the sons of Bilhan: Jeush, and Benjamin, and Ehud, and Chenaanah, and Zethan, and Tarshish, and Ahishahar.
Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
11 All these were sons of Jediael, the leaders of their kindred, very strong men, seventeen thousand and two hundred, going forth to battle.
Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
12 Also, Shuppim and Huppim, the sons of Ir; and Hushim, sons of Aher.
Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
13 Then the sons of Naphtali: Jahziel, and Guni, and Jezer, and Shallum, sons of Bilhah.
Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
14 Also, the son of Manasseh: Asriel. And his concubine, a Syrian, bore Machir, the father of Gilead.
Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
15 Now Machir took wives for his sons, Huppim and Shuppim. And he had a sister named Maacah; but the name of the second was Zelophehad, and daughters were born to Zelophehad.
Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
16 And Maacah, the wife of Machir, bore a son, and she called his name Peresh. And the name of his brother was Sheresh. And his sons were Ulam and Rakem.
Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
17 Then the son of Ulam: Bedan. These are the sons of Gilead, the son of Machir, the son of Manasseh.
Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
18 And his sister, Regina, bore Ishhod, and Abiezer, and Mahlah.
Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
19 Now the sons of Shemida were Ahian, and Shechem, and Likhi and Aniam.
Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
20 And the sons of Ephraim: Shuthelah, Bered his son, Tahath his son, Eleadah his son, Tahath his son, whose son was Zabad,
Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
21 and his son was Shuthelah, and his son was Ezer, and also Elead. But the men indigenous to Gath killed them, because they had descended to invade their possessions.
Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
22 And so their father, Ephraim, mourned for many days; and his brothers arrived, so that they might console him.
Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
23 And he entered to his wife; she conceived and bore a son. And he called his name Beriah, because he rose up during a time of evil for his house.
Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
24 Now his daughter was Sheerah, who built lower and upper Beth-horon, and also Uzzen-sheerah.
Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
25 And Rephah was his son, and Resheph, and Telah, from whom was born Tahan,
Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
26 who conceived Ladan. And his son was Ammihud, who conceived Elishama,
Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
27 from whom was born Nun, who had Joshua as a son.
Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
28 Now their possessions and habitations were: Bethel with her daughters, and toward the east, Naaran, and toward the western region, Gezer and her daughters, as well as Shechem with her daughters, as far as Ayyah with her daughters;
Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
29 also, beside the sons of Manasseh, Bethshean and her daughters, Taanach and her daughters, Megiddo and her daughters, Dor and her daughters. In these places, there lived the sons of Joseph, the son of Israel.
Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
30 The sons of Asher: Imnah, and Ishvah, and Ishvi, and Beriah, and Serah their sister.
Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
31 And the sons of Beriah: Heber, and Malchiel, the same is the father of Birzaith.
Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
32 Now Heber conceived Japhlet, and Shomer, and Hotham, and their sister Shua.
Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
33 The sons of Japhlet: Pasach, and Bimhal, and Ashvath; these are the sons of Japhlet.
Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
34 Then the sons of Shomer: Ahi, and Rohgah, and Jehubbah, and Aram.
Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
35 And the sons of Helem, his brother: Zophah, and Imna, and Shelesh, and Amal.
Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
36 The sons of Zophah: Suah, Harnepher, and Shual, and Beri, and Imrah,
Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
37 Bezer, and Hod, and Shamma, and Shilshah, and Ithran, and Beera.
Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
38 The sons of Jether: Jephunneh, and Pispa, and Ara.
Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
39 Then the sons of Ulla: Arah, and Hanniel, and Rizia.
Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
40 All these were sons of Asher, the leaders of families, elect and very strong rulers among rulers. And the number of those who were of an age that was fit for warfare was twenty-six thousand.
Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.

< 1 Chronicles 7 >