< 1 Chronicles 14 >
1 Also, Hiram, the king of Tyre, sent messengers to David, and cedar wood, and artisans of walls and of wood, so that they might build a house for him.
Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
2 And David realized that the Lord had confirmed him as king over Israel, and that his kingdom had been lifted up over his people Israel.
Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
3 Also, David took other wives in Jerusalem. And he conceived sons and daughters.
Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
4 And these are the names of those who were born to him in Jerusalem: Shammua and Shobab, Nathan and Solomon,
Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
5 Ibhar, and Elishua, and Elpelet,
Ibihari, Elishua, Elpeleti,
6 as well as Nogah, and Nepheg, and Japhia,
Noga, Nefegi, Yafia,
7 Elishama, and Beeliada, and Eliphelet.
Elishama, Beeliada na Elifeleti.
8 Then, hearing that David had been anointed as king over all of Israel, all the Philistines ascended so that they might seek him. But when David had heard of it, he went out to meet them.
Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
9 Now the Philistines, arriving, spread out in the Valley of the Rephaim.
Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
10 And so David consulted the Lord, saying, “Shall I ascend to the Philistines, and will you deliver them into my hand?” And the Lord said to him, “Ascend, and I will deliver them into your hand.”
Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
11 And when they had ascended to Baal-perazim, David struck them there, and he said: “God has divided my enemies by my hand, just as waters are divided.” And therefore the name of that place was called Baal-perazim.
Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
12 And they left behind their gods in that place, and so David ordered them to be burned.
Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
13 And then, at another time, the Philistines invaded, and they spread out in the valley.
Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
14 And again, David consulted God. And God said to him: “You shall not ascend after them. Draw away from them. And you shall come against them opposite the balsam trees.
hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
15 And when you hear a sound approaching in the tops of the balsam trees, then you shall go forth to war. For God has gone forth before you, so that he may strike down the army of the Philistines.”
Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
16 Therefore, David did just as God had instructed him. And he struck down the army of the Philistines, from Gibeon as far as Gazera.
Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
17 And the name of David became well-known in all the regions. And the Lord placed the fear of him over all the nations.
Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.