< Psalms 80 >

1 For the end, for alternate [strains], a testimony for Asaph, a Psalm concerning the Assyrian. Attend, O Shepherd of Israel, who guide Joseph like a flock; you who sit upon the cherubs, manifest yourself;
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 before Ephraim and Benjamin and Manasse, stir up your power, and come to deliver us.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Turn us, O God, and cause your face to shine; and we shall be delivered.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 O Lord God of hosts, how long are you angry with the prayer of your servant?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 You will feed us with bread of tears; and will cause us to drink tears by measure.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 You has made us a strife to our neighbours; and our enemies have mocked at us.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Turn us, O Lord God of hosts, and cause your face to shine; and we shall be saved. (Pause)
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 You have transplanted a vine out of Egypt: you have cast out the heathen, and planted it.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 You made a way before it, and did cause its roots to strike, and the land was filled [with it].
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Its shadow covered the mountains, and its shoots [equalled] the goodly cedars.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 It sent forth its branches to the sea, and its shoots to the river.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Therefore have you broken down its hedge, while all that pass by the way pluck it?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 The boar out of the wood has laid it waste, and the wild beast has devoured it.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 O God of hosts, turn, we pray you: look on [us] from heaven, and behold and visit this vine;
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 and restore that which your right hand has planted: and look on the son of man whom you did strengthen for yourself.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 [It is] burnt with fire and dug up: they shall perish at the rebuke of your presence.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Let your hand be upon the man of your right hand, and upon the son of man whom you did strengthen for yourself.
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 So will we not depart from you: you shall quicken us, and we will call upon your name.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Turn us, O Lord God of hosts, and make your face to shine; and we shall be saved.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Psalms 80 >