< Psalms 76 >
1 For the end, amongst the Hymns, a Psalm for Asaph; a Song for the Assyrian. God is known in Judea: his name is great in Israel.
Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
2 And his place has been in peace, and his dwelling-place in Sion.
Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
3 There he broke the power of the bows, the shield, and the sword, and the battle. (Pause)
Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
4 You do wonderfully shine forth from the everlasting mountains.
Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
5 All the simple ones in heart were troubled; all the men of wealth have slept their sleep, and have found nothing in their hands.
Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
6 At your rebuke, O God of Jacob, the riders on horses slumbered.
Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
7 You are terrible; and who shall withstand you, because of your anger?
Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
8 You did cause judgement to be heard from heaven; the earth feared, and was still,
Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
9 when God arose to judgement, to save all the meek in heart. (Pause)
wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
10 For the inward thought of man shall give thanks to you: and the memorial of his inward thought shall keep a feast to you.
Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
11 Vow, and pay [your vows] to the Lord our God; all that are round about him shall bring gifts, [even] to him that is terrible,
Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
12 and that takes away the spirits of princes; to him that is terrible amongst the kings of the earth.
Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.