< Psalms 52 >
1 For the end, [a Psalm] of instruction by David, when Doec the Idumean came and told Saul, and said to him, David is gone to the house of Abimelech. Why do you, O mighty man, boast of iniquity in [your] mischief? All the day
Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
2 your tongue has devised unrighteousness; like a sharpened razor you have wrought deceit.
Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
3 You have loved wickedness more than goodness; unrighteousness better than to speak righteousness. (Pause)
Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
4 You has loved all words of destruction, [and] a deceitful tongue.
Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
5 Therefore may God destroy you for ever, may he pluck you up and utterly remove you from [your] dwelling, and your root from the land of the living. (Pause)
Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
6 And the righteous shall see, and fear, and shall laugh at him, and say,
Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
7 Behold the man who made not God his help; but trusted in the abundance of his wealth, and strengthened himself in his vanity.
“Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
8 But I am as a fruitful olive in the house of God: I have trusted in the mercy of God for ever, even for evermore.
Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
9 I will give thanks to you for ever, for you have done [it]: and I will wait on your name; for [it is] good before the saints.
Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.