< Proverbs 28 >

1 The ungodly [man] flees when no one pursues: but the righteous is confident as a lion.
Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
2 By reason of the sins of ungodly men quarrels arise; but a wise man will quell them.
Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
3 A bold man oppresses the poor by ungodly deeds. As an impetuous and profitable rain,
Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
4 so they that forsake the law praise ungodliness; but they that love the law fortify themselves with a wall.
Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
5 Evil men will not understand judgement: but they that seek the Lord will understand everything.
Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
6 A poor man walking in truth is better than a rich liar.
Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
7 A wise son keeps the law: but he that keeps up debauchery dishonours his father.
Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
8 He that increases his wealth by usuries and [unjust] gains, gathers it for him that pities the poor.
Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
9 He that turns away his ear from hearing the law, even he has made his prayer abominable.
Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 He that causes upright men to err in an evil way, himself shall fall into destruction: transgressor also shall pass by prosperity, but shall not enter into it.
Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
11 A rich man is wise in his own conceit; but an intelligent poor man will condemn him.
Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
12 By reason of the help of righteous men great glory arises: but in the places of the ungodly men are caught.
Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
13 He that covers his own ungodliness shall not prosper: but he that blames [himself] shall be loved.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
14 Blessed is the man who religiously fears always: but the hard of heart shall fall into mischiefs.
Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
15 A hungry lion and a thirsty wolf [is he], who, being poor, rules over a poor nation.
Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
16 A king in need of revenues is a great oppressor: but he that hates injustice shall live a long time.
Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
17 He that becomes surety for a man charged with murder shall be an exile, and not in safety. Chasten your son, and he shall love you, and give honour to your soul: he shall not obey a sinful nation.
Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
18 He that walks justly is assisted: but he that walks in crooked ways shall be entangled [therein].
Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
19 He that tills his own land shall be satisfied with bread: but he that follows idleness shall have plenty of poverty.
Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
20 A man worthy of credit shall be much blessed: but the wicked shall not be unpunished.
Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
21 He that reverences not the persons of the just is not good: such a one will sell a man for a morsel of bread.
Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
22 An envious man makes haste to be rich, and knows not that the merciful man will have the mastery over him.
Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
23 He that reproves a man's ways shall have more favour than he that flatters with the tongue.
Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
24 He that casts off father or mother, and thinks he sins not; the same is partaker with an ungodly man.
Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
25 An unbelieving man judges rashly: but he that trusts in the Lord will act carefully.
Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
26 He that trusts to a bold heart, such an one is a fool: but he that walks in wisdom shall be safe.
Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
27 He that gives to the poor shall not be in lack: but he that turns away his eye [from him] shall be in great distress.
Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
28 In the places of ungodly [men] the righteous mourn: but in their destruction the righteous shall be multiplied.
Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.

< Proverbs 28 >