< Proverbs 26 >

1 As dew in harvest, and as rain in summer, so honour is not [seemly] for a fool.
Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2 As birds and sparrows fly, so a curse shall not come upon any one without a cause.
Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3 As a whip for a horse, and a goad for an ass, so [is] a rod for a simple nation.
Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4 Answer not a fool according to his folly, lest you become like him.
Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5 Yet answer a fool according to his folly, lest he seem wise in his own conceit.
Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6 He that sends a message by a foolish messenger procures for himself a reproach from his own ways.
Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7 [As well] take away the motion of the legs, as transgression from the mouth of fools.
Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8 He that binds up a stone in a sling, is like one that gives glory to a fool.
Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9 Thorns grow in the hand of a drunkard, and servitude in the hand of fools.
Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10 All the flesh of fools endures much hardship; for their fury is brought to nothing.
Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
11 As when a dog goes to his own vomit, and becomes abominable, so is fool who returns in his wickedness to his own sin. [There is a shame that brings sin: and there is a shame [that is] glory and grace.]
Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
12 I have seen a man who seemed to himself to be wise; but a fool had more hope than he.
Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
13 A sluggard when sent on a journey says, [There is] a lion in the ways, and [there are] murderers in the streets.
Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
14 As a door turns on the hinge, so does a sluggard on his bed.
Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
15 A sluggard having hid his hand in his bosom, will not be able to bring it up to his mouth.
Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
16 A sluggard seems to himself wiser than one who most satisfactorily brings back a message.
Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
17 As he that lays hold of a dog's tail, so is he that makes himself the champion of another's cause.
Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
18 As those who need correction put forth [fair] words to men, and he that first falls in with the proposal will be overthrown;
Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
19 so are all that lay wait for their own friends, and when they are discovered, say, I did it in jest.
ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20 With much wood fire increases; but where there is not a double-minded man, strife ceases.
Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
21 A hearth for coals, and wood for fire; and railing man for the tumult of strife.
Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
22 The words of cunning knaves are soft; but they strike [even] to the inmost parts of the bowels.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
23 Silver dishonestly given is to be considered as a potsherd: smooth lips cover a grievous heart.
Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
24 A weeping enemy promises all things with his lips, but in his heart he contrives deceit.
Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
25 Though [your] enemy entreat you with a loud voice, consent not: for there are seven abominations in his heart.
Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
26 He that hides enmity frames deceit: but being easily discerned, exposes his own sins in the public assemblies.
Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
27 He that digs a pit for his neighbour shall fall into it: and he that rolls a stone, rolls it upon himself.
Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
28 A lying tongue hates the truth; and an unguarded mouth causes tumults.
Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.

< Proverbs 26 >