< Proverbs 26 >

1 As dew in harvest, and as rain in summer, so honour is not [seemly] for a fool.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 As birds and sparrows fly, so a curse shall not come upon any one without a cause.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 As a whip for a horse, and a goad for an ass, so [is] a rod for a simple nation.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Answer not a fool according to his folly, lest you become like him.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Yet answer a fool according to his folly, lest he seem wise in his own conceit.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 He that sends a message by a foolish messenger procures for himself a reproach from his own ways.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 [As well] take away the motion of the legs, as transgression from the mouth of fools.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 He that binds up a stone in a sling, is like one that gives glory to a fool.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Thorns grow in the hand of a drunkard, and servitude in the hand of fools.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 All the flesh of fools endures much hardship; for their fury is brought to nothing.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 As when a dog goes to his own vomit, and becomes abominable, so is fool who returns in his wickedness to his own sin. [There is a shame that brings sin: and there is a shame [that is] glory and grace.]
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 I have seen a man who seemed to himself to be wise; but a fool had more hope than he.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 A sluggard when sent on a journey says, [There is] a lion in the ways, and [there are] murderers in the streets.
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 As a door turns on the hinge, so does a sluggard on his bed.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 A sluggard having hid his hand in his bosom, will not be able to bring it up to his mouth.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 A sluggard seems to himself wiser than one who most satisfactorily brings back a message.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 As he that lays hold of a dog's tail, so is he that makes himself the champion of another's cause.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 As those who need correction put forth [fair] words to men, and he that first falls in with the proposal will be overthrown;
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 so are all that lay wait for their own friends, and when they are discovered, say, I did it in jest.
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 With much wood fire increases; but where there is not a double-minded man, strife ceases.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 A hearth for coals, and wood for fire; and railing man for the tumult of strife.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 The words of cunning knaves are soft; but they strike [even] to the inmost parts of the bowels.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Silver dishonestly given is to be considered as a potsherd: smooth lips cover a grievous heart.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 A weeping enemy promises all things with his lips, but in his heart he contrives deceit.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Though [your] enemy entreat you with a loud voice, consent not: for there are seven abominations in his heart.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 He that hides enmity frames deceit: but being easily discerned, exposes his own sins in the public assemblies.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 He that digs a pit for his neighbour shall fall into it: and he that rolls a stone, rolls it upon himself.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 A lying tongue hates the truth; and an unguarded mouth causes tumults.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Proverbs 26 >