< Proverbs 12 >

1 He that loves instruction loves sense, but he that hates reproofs is a fool.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 He that has found favour with the Lord [is made] better; but a transgressor shall be passed over in silence.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 A man shall not prosper by wickedness; but the roots of the righteous shall not be taken up.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 A virtuous woman is a crown to her husband; but as a worm in wood, so a bad woman destroys her husband.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 The thoughts of the righteous [are true] judgements; but ungodly men devise deceits.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 The words of ungodly men are crafty; but the mouth of the upright shall deliver them.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 When the ungodly is overthrown, he vanishes away; but the houses of the just remain.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 The mouth of an understanding [man] is praised by a man; but he that is dull of heart is had in derision.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Better is a man in dishonour serving himself, than one honouring himself and lacking bread.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 A righteous man has pity for the lives of his cattle; but the bowels of the ungodly are unmerciful.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 He that tills his own land shall be satisfied with bread; but they that pursue vanities are void of understanding. He that enjoys himself in banquets of wine, shall leave dishonour in his own strong holds.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 The desires of the ungodly are evil; but the roots of the godly are firmly set.
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 For the sin of [his] lips a sinner falls into snare; but a righteous man escapes from them. He whose looks are gentle shall be pitied, but he that contends in the gates will afflict souls.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 The soul of a man shall be filled with good from the fruits of his mouth; and the recompence of his lips shall be given to him.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 The ways of fools are right in their own eyes; but a wise man hearkens to counsels.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 A fool declares his wrath the same day; but a prudent man hides his own disgrace.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 A righteous man declares the open truth; but an unjust witness is deceitful.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 Some wound as they speak, [like] swords; but the tongues of the wise heal.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 True lips establish testimony; but a hasty witness has an unjust tongue.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 [There is] deceit in the heart of him that imagines evil; but they that love peace shall rejoice.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 No injustice will please a just man; but the ungodly will be filled with mischief.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 Lying lips are a abomination to the Lord; but he that deals faithfully is accepted with him.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 An understanding man is a throne of wisdom; but the heart of fools shall meet with curses.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 The hand of chosen men shall easily obtain rule; but the deceitful shall be for a prey.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 A terrible word troubles the heart of a righteous man; but a good message rejoices him.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 A just arbitrator shall be his own friend; but mischief shall pursue sinners; and the way of ungodly men shall lead them astray.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 A deceitful man shall catch no game; but a blameless man is a precious possession.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 In the ways of righteousness is life; but the ways of those that remember injuries [lead] to death.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Proverbs 12 >