< Job 31 >

1 I made a covenant with mine eyes, and I will not think upon a virgin.
Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
2 Now what portion has God given from above? and is there an inheritance [given] of the Mighty One from the highest?
Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
3 Alas! destruction to the unrighteous, and rejection to them that do iniquity.
Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
4 Will he not see my way, and number all my steps?
Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
5 But if I had gone with scorners, and if too my foot has hasted to deceit:
Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
6 (for I am weighed in a just balance, and the Lord knows my innocence: )
na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
7 if my foot has turned aside out of the way, or if mine heart has followed mine eye, and if too I have touched gifts with my hands;
Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
8 then let me sow, and let others eat; and let me be uprooted on the earth.
na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
9 If my heart has gone forth after another man's wife, and if I laid wait at her doors;
Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
10 then let my wife also please another, and let my children be brought low.
na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
11 For the rage of anger is not to be controlled, [in the case] of defiling [another] man's wife.
Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
12 For it is a fire burning on every side, and whoever it attacks, it utterly destroys.
Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
13 And if too I despised the judgement of my servant or [my] handmaid, when they pleaded with me;
Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
14 what then shall I do if the Lord should try me? and if also he should at all visit me, can I make an answer?
kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
15 Were not they too formed as I also was formed in the womb? yes, we were formed in the same womb.
Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
16 But the helpless missed not whatever need they had, and I did not cause the eye of the widow to fail.
kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
17 And if too I ate my morsel alone, and did not impart [of it] to the orphan;
au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
18 (for I nourished [them] as a father from my youth and guided [them] from my mother's womb.)
kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
19 And if too I overlooked the naked as he was perishing, and did not clothe him;
ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
20 and if the poor did not bless me, and their shoulders were [not] warmed with the fleece of my lambs;
ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
21 if I lifted my hand against an orphan, trusting that my strength was far superior [to his]:
ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
22 let them my shoulder start from the blade-bone, and my arm be crushed off from the elbow.
Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
23 For the fear of the Lord constrained me, and I can’t bear up by reason of his burden.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
24 If I made gold my treasure, and if too I trusted the precious stone;
Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
25 and if too I rejoiced when my wealth was abundant, and if too I laid my hand on innumerable [treasures]:
na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
26 (do we not see the shining sun eclipsed, and the moon waning? for they have not [power to continue]: )
Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
27 and if my heart was secretly deceived, and if I have laid my hand upon my mouth and kissed it:
na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
28 let this also then be reckoned to me as the greatest iniquity: for I [should] have lied against the Lord Most High.
hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
29 And if too I was glad at the fall of mine enemies, and mine heart said, Aha!
Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
30 let then mine ear hear my curse, and let me be a byword amongst my people in my affliction.
Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
31 And if too my handmaids have often said, Oh that we might be satisfied with his flesh; (whereas I was very kind:
Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
32 for the stranger did not lodge without, and my door was opened to every one that came: )
(hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
33 or if too having sinned unintentionally, I hid my sin;
Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
34 (for I did not stand in awe of a great multitude, so as not to declare boldly before them: ) and if too I permitted a poor man to go out of my door with an empty bosom:
kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
35 (Oh that I had a hearer, ) and if I had not feared the hand of the Lord; and [as to] the written charge which I had against any one,
Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
36 I would place [it] as a chaplet on my shoulders, and read it.
Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
37 And if I did not read it and return it, having taken nothing from the debtor:
Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
38 If at any time the land groaned against me, and if its furrows mourned together;
Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
39 and if I ate its strength alone without price, and if I too grieved the heart of the owner of the soil, by taking [anything] from [him]:
ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
40 then let the nettle come up to me instead of wheat, and a bramble instead of barley. And Job ceased speaking.
ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.

< Job 31 >