< Jeremias 23 >
1 Woe to the shepherds that destroy and scatter the sheep of their pasture!
“Ole wao wachungaji ambao huangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu-hii ndiyo ahadi ya Bwana.”
2 Therefore thus says the Lord against them that tend my people; You have scattered my sheep, and driven them out, and you have not visited them: behold, I [will] take vengeance upon you according to your evil practices.
Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi juu ya wachungaji ambao wanawachunga watu wake, “Ninyi mnawatawanya kundi langu na kuwafukuza. Hamuwajali hata kidogo. Tambueni hili! Mimi nitawalipiza uovu wa matendo yenu-hili ni tamko la Bwana.
3 And I will gather in the remnant of my people in every land, whither I have driven them out, and will set them in their pasture; and they shall increase and be multiplied.
Mimi mwenyewe nitakusanya mabaki ya kondoo wangu kutoka nchi zote nilizowafukuza, nami nitawarejesha kwenye eneo la malisho, ambako watazaa na kuongezeka.
4 And I will raise up shepherds to them, who shall feed them: and they shall fear no more, nor be alarmed, says the Lord.
Ndipo nitawainua wachungaji juu yao ambao watawachunga hivyo hawataogopa tena au kupotezwa. Hakuna hata mmoja atakayepotea-hili ni tamko la Bwana.
5 Behold, the days come, says the Lord, when I will raise up to David a righteous branch, and a king shall reign and understand, and shall execute judgement and righteousness on the earth.
Angalia, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-nitakapomuinulia Daudi tawi la haki. Atatawala kama mfalme; atatenda kwa busara na kusababisha hukumu na haki katika nchi.
6 In his days both Juda shall be saved, and Israel shall dwell securely: and this is his name, which the Lord shall call him, Josedec amongst the prophets.
Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli wataishi kwa usalama. Na jina lake atakayeitwa Bwana ni haki yetu.
7 Therefore, behold, the days come, says the Lord, when they shall no more say, The Lord lives, who brought up the house of Israel out of the land of Egypt;
Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-hawatasema tena, 'Kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya Misri.'
8 but The Lord lives, who has gathered the whole seed of Israel from the north land, and from all the countries whither he [had] driven them out, and has restored them into their own land.
Badala yake watasema, 'Kama Bwana aishivyo, ambaye aliwaleta na ambaye aliwaongoza wana wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote walizofukuzwa.' Nao watakaa katika nchi yao wenyewe.”
9 My heart is broken within me; all my bones are shaken: I am become as a broken-down man, and as a man overcome with wine, because of the Lord, and because of the excellence of his glory.
Kuhusu manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu, na mifupa yangu yote imetetemeka. Nimekuwa kama mlevi, kama mtu ambaye ameshindwa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
10 For because of these things the land mourns; the pastures of the wilderness are dried up; and their course is become evil, and so [also] their strength.
Kwa maana nchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya hayo nchi imeuka. Milima katika jangwa imekauka. Njia hizi za manabii ni mbaya; nguvu zao hazitumiwi kwa namna sahihi.
11 For priest and prophet are defiled; and I have seen their iniquities in my house.
Kwa maana manabii na makuhani wote wamekufuru. Nimeona uovu wao ndani ya nyumba yangu! - hili ndilo tamko la Bwana;
12 Therefore let their way be to them slippery and dark: and they shall be tripped up and fall in it: for I will bring evils upon them, in the year of their visitation.
kwa hiyo njia yao itakuwa kama mahali pa kupumzika katika giza. Watasukumwa chini. Wao wataanguka ndani yake. Kwa maana nitawatuma mabaya juu yao katika mwaka wa adhabu yao; hili ndilo tamko la Bwana.
13 And in the prophets of Samaria I have seen lawless deeds; they prophesied by Baal, and led my people Israel astray.
kwa maana nimeona uchungu kati ya manabii huko Samaria. Walitabiri kwa Baali na wakawaongoza watu wangu Israeli kwenye njia sahihi.
14 Also in the prophets of Jerusalem I have seen horrible things: as they committed adultery, and walked in lies, and strengthened the hands of many, that they should not return each from his evil way: they are all become to me as Sodom, and the inhabitants thereof as Gomorrha.
Na miongoni mwa manabii huko Yerusalemu nimeona mambo ya kutisha: wanafanya uzinzi na huenda kwa udanganyifu. Wanaimarisha mikono ya waovu; hakuna mtu anarejea na kuacha uovu wake. Wote wamekuwa kama Sodoma kwangu na wenyeji wake kama Gomora!”
15 Therefore thus says the Lord; Behold, I will feed them with pain, and give them bitter water to drink: for from the prophets of Jerusalem has defilement gone forth [into] all the land.
Kwa hiyo, Bwana wa majeshi asema hivi juu ya manabii, “Tazameni, nitawafanya wale magugu na kunywa maji yenye sumu, kwa maana kufuru imetoka kwa manabii wa Yerusalemu na kuingia katika nchi yote.”
16 Thus says the Lord Almighty, Listen not to the words of the prophets: for they frame a vain vision for themselves; they speak from their own heart, and not from the mouth of the Lord.
Bwana wa majeshi asema hivi, “Usisikilize maneno ya manabii wanaokuhubiri. Wamekudanganya! Wanatangaza maono kutoka kwenye mawazo yao wenyewe, si kwa kinywa cha Bwana.
17 They say to them that reject the word of the Lord, There shall be peace to you; and to all that walk after their own lusts, and to everyone that walks in the error of his heart, they have said, No evil shall come upon you.
Wanasema daima kwa wale wanaonidharau mimi, 'Bwana asema kutakuwa na amani kwako.' Na kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake anasema, 'mabaya hayatakuja kwenu.'
18 For who has stood in the counsel of the Lord, and seen his word? who has listened, and heard?
Lakini nani amesimama katika mkutano wa baraza la Bwana? Ni nani anayeona na kusikia neno lake? Ni nani anayezingatia maneno yake na kusikiliza?
19 Behold, [there is] an earthquake from the Lord, and anger proceeds to a convulsion, it shall come violently upon the ungodly.
Tazama, kuna dhoruba inayotoka kwa Bwana! Hasira yake inatoka, na dhoruba inazunguka. Inazunguka vichwa vya waovu.
20 And the Lord's wrath shall return no more, until he have accomplished it, and until he have established it, according to the purpose of his heart: at the end of the days they shall understand it.
Hasira za Bwana hazitarejea mpaka zitakapotimiza nia ya moyo wake. Katika siku za mwisho, utaelewa.
21 I sent not the prophets, yet they ran: neither spoke I to them, yet they prophesied.
Sikuwatuma manabii hawa. Wao tu walionekana. Sikuwahubiri jambo lolote kwao, lakini bado wanatabiri.
22 But if they had stood in my counsel, and if they had listened to my words, then would they have turned my people from their evil practices.
Kwa kuwa kama walisimama katika mkutano wangu wa baraza, wangeweza kuwasababisha watu wangu kusikia neno langu; wangewafanya wapate kuacha maneno yao mabaya na mazoea mabaya.
23 I am a God near at hand, says the Lord, and not a God afar off.
Mimi ni Mungu aliye karibu-hili ni tamko la Bwana-mimi sio Mungu aliye mbali?
24 Shall any one hide himself in secret places, and I not see him? Do I not fill heaven and earth? says the Lord.
Je, kuna mtu yeyote anayejificha mahali penye siri ili nisiweze kumwona? -Hili ndilo tamko la Bwana-Je mbingu na nchi hazikujawa nami? -hili Ndilo tamko la Bwana.
25 I have heard what the prophets say, what they prophesy in my name, saying falsely, I have seen a night vision.
Nimesikia yale waliyosema manabii, wale waliokuwa wanatabiri uongo kwa jina langu. Wakisema, 'Nilikuwa na ndoto!
26 How long shall [these things] be in the heart of the prophets that prophesy lies, when they prophesy the purposes of their own heart?
Nilikuwa na ndoto!' Je, hii itaendelea mpaka lini, manabii wanaotabiri uongo kutoka kwa akili zao, na wanasema nini kutokana na udanganyifu mioyoni mwao?
27 who devise that [men] may forget my law by their dreams, which they have told every one to his neighbour, as their fathers forgot my name in [the worship of] Baal.
Wana mpango wa kuwafanya watu wangu kusahau jina langu kwa ndoto ambazo wanazoripoti, kila mmoja kwa jirani yake, kama vile babu zao walivyosahau jina langu kwa ajili ya jina la Baali.
28 The prophet who has a dream, let him tell his dream; and [he] in whom is my word [spoken] to him, let him tell my word truly: what is the chaff to the corn? so are my words, says the Lord.
Nabii aliye na ndoto, aseme ndoto hiyo. Lakini yule ambaye nimemwambia kitu fulani, basi aseme neno langu kwa kweli. Je, majani yanahusiana na nafaka? - hili ni tamko la Bwana-
29 Behold, are not my words as fire? says the Lord; and as an axe cutting the rock?
Na neno langu si kama moto? -Hili ni tamko la Bwana-na kama mwamba wenye kupiga nyundo?
30 Behold, I am therefore against the prophets, says the Lord God, that steal my words every one from his neighbour.
Tazameni, ninapingana na nabii-hii ndiyo ahadi ya Bwana-yeyote anayeiba maneno kutoka kwa mtu mwingine na anasema yanatoka kwangu.
31 Behold, I am against the prophets that put forth prophecies of mere words, and slumber their sleep.
Tazama, ninapingana na manabii-hili ndilo tamko la Bwana-ambao hutumia lugha zao kutabiri maneno.
32 Therefore, behold, I am against the prophets that prophesy false dreams, and have not told them [truly], and have caused my people to err by their lies, and by their errors; yet I sent them not, and commanded them not; therefore, they shall not profit this people at all.
Tazameni, ninapingana na manabii wanaoota ndoto-hii ndiyo ahadi ya Bwana-na kisha kuwahubiri na kwa njia hii kuwadanganya watu wangu kwa udanganyifu wao na kujivunia. Mimi ni juu yao, kwa kuwa sikuwatuma wala kuwapa amri. Kwa hivyo hawatawasaidia watu hawa - hili ndilo tamko la Bwana.
33 And if this people, or the priest, or the prophet, should ask, What is the burden of the Lord? then you shall say to them, You are the burden, and I will dash you down, says the Lord.
Watu hawa au nabii au kuhani wakakuuliza, 'Je, ni nini tamko la Bwana?' basi lazima uwaambie, 'Ni tamko gani? Kwa maana nimekuacha wewe-hili ndilo tamko la Bwana.
34 [As for] the prophet, and the priests, and the people, who shall say, The burden of the Lord, I will even take vengeance on that man, and on his house.
Kwa habari ya manabii, makuhani, na watu wanaosema, 'Hili ndilo tamko la Bwana,' nitamuadhibu mtu huyo na nyumba yake.
35 Thus shall you say every one to his neighbour, and every one to his brother, What has the Lord answered? and, what has the Lord said?
Endelea kusema, kila mtu kwa jirani yake na kila mtu kwa ndugu yake, 'Bwana alijibu nini?' na 'Bwana alitangaza nini?'
36 And do you name no more the burden of the Lord; for his own word shall be a man's burden.
Lakini usizungumze tena juu ya tamko la Bwana, kwa kuwa kila tamko kutoka kwa kila mtu limekuwa ujumbe wake mwenyewe, na umepotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana wa majeshi, Mungu wetu.
37 But therefore, [say you], has the Lord our God spoken?
Utamuuliza nabii hivi, 'Bwana alikujibu nini? Je, Bwana alisema nini? Kisha unasema tamko kutoka kwa Bwana;
38 Therefore thus says the Lord our God; Because you have spoken this word, The burden of the Lord, and I sent to you, saying, you shall not say, The burden of the Lord;
lakini Bwana asema hivi, Sema hivi, “Hili ni tamko la Bwana” ingawa nimekuagiza na kusema, “Usiseme: Hili ni tamko kutoka kwa Bwana.”
39 therefore, behold, I [will] seize, and dash down you and the city which I gave to you and your fathers.
Kwa hiyo, angalia, nitawachukua na kukutupa mbali na mimi, pamoja na jiji ambalo nilikupa wewe na baba zako.
40 And I will bring upon you an everlasting reproach, and everlasting disgrace, which shall not be forgotten.
Ndipo nitaweka aibu ya milele na fedheha juu yenu ambayo haitasahauliwa.'”