< Osee 8 >

1 [He shall come] into their midst as the land, as an eagle against the house of the Lord, because they have transgressed my covenant, and have sinned against my law.
“Weka tarumbeta katika midomo yako! Tai anakuja juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja agano langu na waliasi dhidi ya sheria yangu.
2 They shall soon cry out to me, [saying], O God, we know you.
Wananililia,'Mungu wangu, sisi katika Israeli tunakujua.'
3 For Israel has turned away from good things; they have pursued an enemy.
Lakini Israeli amekataa mema, na adui atamfuata.
4 They have made kings for themselves, but not by me: they have ruled, but they did not make it known to me: [of] their silver and their gold they have made images to themselves, that they might be destroyed.
Wameweka wafalme, lakini sio kwa shauri langu. Wamewafanya wakuu, lakini sikuwa na habari. Kwa fedha zao na dhahabu wamejifanyia sanamu wenyewe, ili wakatiliwe mbali.”
5 Cast off your calf, O Samaria; mine anger is kindled against them: how long will they be unable to purge themselves in Israel?
“Ndama yako imekataliwa, Samaria. Hasira yangu inawaka juu ya watu hawa. Kwa muda gani watakuwa na hatia?
6 Whereas the workman made it, and it is not God; therefore your calf, Samaria, was a deceiver:
Kwa maana sanamu hii ilitoka Israeli; fundi aliifanya; si Mungu! Ndama ya Samaria itavunjwa vipande vipande.
7 for they sowed blighted [seed], and their destruction shall await them, a sheaf of corn that avails not to make meal; and even if it should produce it, strangers shall devour it.
Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga. Mbegu zilizosimama hazina vichwa; haitoi unga. Ikiwa itakomaa, wageni watakula.
8 Israel is swallowed up: now is he become amongst the nations as a worthless vessel.
Israeli imemezwa; sasa wanalala kati ya mataifa kama kitu kisicho na maana.
9 For they have gone up to the Assyrians: Ephraim has been strengthened against himself; they loved gifts.
Kwa maana walikwenda Ashuru kama punda wa mwitu pekee. Efraimu ameajiri wapenzi kwa ajili yake mwenyewe.
10 Therefore shall they be delivered to the nations: now I will receive them, and they shall cease a little to anoint a king and princes.
Hata ingawa wameajiri wapenzi kati ya mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wao wataanza kupotea kwa sababu ya unyanyasaji wa mfalme wa wakuu.
11 Because Ephraim has multiplied altars, [his] beloved altars are become sins to him.
Kwa maana Efraimu imeongeza madhabahu kwa sadaka za dhambi, lakini zimekuwa madhabahu kwa kufanya dhambi.
12 I will write down a multitude [of commands] for him; but his statutes are accounted strange things, [even] the beloved altars.
Niliweza kuandika sheria yangu kwao mara elfu kumi, lakini wangeiona kama kitu cha ajabu kwao.
13 For if they should offer a sacrifice, and eat flesh, the lord will not accept them: now will he remember their iniquities, and will take vengeance on their sins: they have returned to Egypt, and they shall eat unclean things amongst the Assyrians.
Kwa ajili ya dhabihu za sadaka zangu, hutoa nyama na kuila, lakini mimi, Bwana, siwakubali. Sasa nitafikiri juu ya uovu wao na kuadhibu dhambi zao. Watarudi Misri.
14 And Israel has forgotten him that made him, and they have built fanes, and Juda has multiplied walled cities: but I will send fire on his cities, and it shall devour their foundations.
Israeli amenisahau mimi, Muumba wake, na amejenga majumba. Yuda ameimarisha miji mingi, lakini nitatuma moto juu ya miji yake; itaharibu ngome zake.

< Osee 8 >