< Deuteronomy 27 >

1 And Moses and the elders of Israel commanded, saying, Keep all these commands, all that I command you this day.
Musa na wazee wa Israeli waliwaamuru watu na kusema, “Zishikeni amri zote ninazowaamuru leo.
2 And it shall come to pass in the day when you shall cross over Jordan into the land which the Lord your God gives you, that you shall set up for yourself great stones, and shall plaster them with plaster.
Katika siku mtakapopita juu ya Yordani kwenye nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia, mnapaswa kutengeneza mawe kiasi makubwa na kuyachapa kwa lipu.
3 And you shall write on these stones all the words of this law, as soon as you have crossed Jordan, when you are entered into the land, which the Lord God of your fathers gives you, a land flowing with milk and honey, according as the Lord God of your fathers said to you.
Mnatakiwa kuyaandika juu yake maneno yote ya sheria hii pale mtakapovuka; ili muweze kwenda katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali, kama Yahwe, Mungu wa mababu zenu, alivyowaahidi.
4 And it shall be as soon as you are gone over Jordan, you shall set up these stones, which I command you this day, on mount Gaebal, and you shall plaster them with plaster.
Mtakapovuka juu ya Yordani, yapangane haya mawe ninayowaamuru leo, juu ya mlima wa Ebali, na myapige kwa lipu.
5 And you shall build there an altar to the Lord your God, an altar of stones; you shall not lift up iron upon it.
Hapo mnapaswa kujenga dhabahu kwa Yahwe Mungu wako, dhabahu la mawe; lakini hautakiwi kuinua chombo cha chuma kujenga mawe.
6 Of whole stones shall you build an altar to the Lord your God, and you shall offer upon it whole burnt offerings to the Lord your God.
Unatakiwa kujenga dhabahu ya Yahwe Mungu wako kwa mawe yasiyokuwa na kazi; unatakiwa kutoa dhabihu ya kuteketeza juu yake kwa Yahwe Mungu wako,
7 And you shall there offer a peace-offering; and you shall eat and be filled, and rejoice before the Lord your God.
na utatoa sadaka ya pamoja na utakula pale; utafurahia mbele ya Yahwe Mungu wako.
8 And you shall write upon the stones all this law very plainly.
Utaandika juu ya mawe maneno yote ya sheria hii kwa wazi.
9 And Moses and the priests the Levites spoke to all Israel, saying, Be silent and hear, O Israel; this day you are become a people to the Lord your God.
Musa na makuhani, Walawi, waliongea na Waisraeli wote na kusema, “Nyamazeni na sikilizeni Israel: Leo mmekuwa watu wa Yahwe Mungu wenu.
10 And you shall listen to the voice of the Lord your God, and shall do all his commands, and his ordinances, as many as I command you this day.
Mnapaswa basi kutii sauti ya Yahwe Mungu wenu na kutii amri na sheria zake ambazo ninawaamuru leo.”
11 And Moses charged the people on that day, saying,
Musa aliwaamuru watu siku hiyo hiyo na kusema,
12 These shall stand to bless the people on mount Garizin having gone over Jordan; Symeon, Levi, Judas, Issachar, Joseph, and Benjamin.
“Makabila haya yanapaswa kusimama katika mlima Gerizimu kuwabariki watu baada ya nyinyi kuvuka Yordani; Simeoni, Lawi, Judah, Isakari, Yusufu na Benyamini.
13 And these shall stand for cursing on mount Gaebal; Ruben, Gad, and Aser, Zabulon, Dan, and Nephthali.
Haya ni makabila ambayo lazima yasimame juu yam lima Ebali kutamka laana: Rubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dan na Naftali.
14 And the Levites shall answer and say to all Israel with a loud voice,
Walawi watajibu na kusema kwa wanamume wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15 Cursed [is] the man whoever shall make a graven or molten image, an abomination to the Lord, the work of the hands of craftsmen, and shall put it in a secret place: and all the people shall answer and say, So be it.
“Alaaniwe mwanamume atakayechonga sanamu au kinyago, chukizo kwa Yahwe, kazi ya mikono ya fundi, ambayo ataifanya sirini”. Kisha watu wote wanapaswa kujibu na kusema, ‘Amina’.
16 Cursed is the man that dishonours his father or his mother: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume atakayemuaibisha baba yake au mama yake. Kisha watu wote waseme, 'Amina'.
17 Cursed is he that removes his neighbour's landmarks: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume anayetoa alama ya ardhi.' Kisha watu wote na waseme, 'Amina'.
18 Cursed is he that makes the blind to wander in the way: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume asababishae kipofu kutoka nje ya barabara. Kisha watu wote waseme, ‘Amina’.
19 Cursed is every one that shall pervert the judgement of the stranger, and orphan, and widow: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume atumiaye nguvu kupokonya haki inayomstahili mgeni, yatima, au mjane. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
20 Cursed is he that lies with his father's wife, because he has uncovered his father's skirt: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na mke wa baba yake, kwa sababu atakuwa amechukua haki za baba yake’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
21 Cursed is he that lies with any beast: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na aina yoyote ya mnyama’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
22 Cursed is he that lies with his sister by his father or his mother: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na dada yake, binti wa baba yake, au binti wa mama yake. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
23 Cursed is he that lies with his daughter-in-law: and all the people shall say, So be it. Cursed is he that lies with his wife's sister: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume atakayelala na mama mkwe’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
24 Cursed is he that smites his neighbour secretly: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume atakayemuua jirani yake kwa siri’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
25 Cursed is he whoever shall have taken a bribe to kill an innocent man: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume apokeaye rushwa kumuua mtu asiye na hatia’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
26 Cursed is every man that continues not in all the words of this law to do them: and all the people shall say, So be it.
Alaaniwe mwanamume asiyethibitisha maneno ya sheria hii, ili kwamba ayatii.’ Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.

< Deuteronomy 27 >