< Deuteronomy 17 >

1 You shall not sacrifice to the Lord your God a calf or a sheep, in which there is a blemish, [or] any evil thing; for it is an abomination to the Lord your God.
Haupaswi kumtolea dhabihu Yahwe Mungu wako ng'ombe au kondoo aliye na kasoro au kitu chochote kibaya, kwa kuwa hiyo itakuwa chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
2 And if there should be found in any one of your cities, which the Lord your God gives you, a man or a woman who shall do that which is evil before the Lord your God, so as to transgress his covenant,
Kama kunapatikana miongoni mwenu, ndani ya malango ya mji wowote ambao Yahwe Mungu wenu anawapatia, mwanaume yoyote au mwanamke ambaye anafanya uovu mbele ya Yahwe Mungu wenu kuiharibu agano lake -
3 and they should go and serve other gods, and worship them, the sun, or the moon, or any of the host of heaven, which he commanded you not to do,
yoyote ambaye ameenda na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, wala jua, mwezi, au kati ya jeshi la mbinguni- hakuna chochote nimekuamuru,
4 and it be told you, and you shall have enquired diligently, and, behold, the thing really took place, this abomination has been done in Israel;
na kama ungeambiwa kuhusu hiki, au kama una mifugo- basi unapaswa kufanya uchunguzi wa makini. Kama ni kweli na hakika kwamba chukizo kama hilo limefanyika Israeli-
5 then shall you bring out that man, or that woman, and you shall stone them with stones, and they shall die.
-basi utamleta huyo mwanaume au mwanamke, aliyefanya uovu huu, katika malango ya mji, kwamba mwanaume kabisa au mwanamke, na umponde huyo mtu mpaka kufa.
6 He shall die on the testimony of two or three witnesses; a man who is put to death shall not be put to death for one witness.
Kwa kinywa cha mashahidi wawili, au mashahidi watatu, itakuwa yeye anayepaswa kuuwawa; lakini kwa kinywa cha shahidi mmoja peke hatauwawa.
7 And the hand of the witnesses shall be upon him amongst the first to put him to death, and the hand of the people at the last; so shall you remove the evil one from amongst yourselves.
Mkono wa mashahidi unapaswa kuwa wa kwanza kumuuwa, na badae mkono wa watu wote; na mtamuondoa muovu miongoni mwenu.
8 And if a matter shall be too hard for you in judgement, between blood and blood, and between cause and cause, and between stroke and stroke, and between contradiction and contradiction, matters of judgement in your cities;
Kama jambo linatokea ambalo ni gumu kwenu kufanya maamuzi- pengine swali la mauaji au kifo cha ajali, haki ya mtu mmoja na haki ya mtu mwingine, au swali moja la aina ya kuzulu kufanyika, au aina nyingine ya jambo-mambo ya utata ndani ya malango yenu, basi utapaswa kwenda kwenye eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kama patakatifu pake.
9 then you shall arise and go up to the place which the Lord your God shall choose, and you shall come to the priests the Levites, and to the judge who shall be in those days, and they shall search out [the matter] and report the judgement to you.
Utapaswa kwenda kwa makuhani, wazao wa Lawi, na kwa mwamuzi atakayetumika kwa wakati huo; mtatafuta ushauri wao, na watawapa ninyi maamuzi.
10 And you shall act according to the thing which they shall report to you out of the place which the Lord your God shall choose, and you shall observe to do all whatever shall have been by law appointed to you.
Mnapaswa kufuata sheria mliyopewa, katika eneo Yahwe atachagua kama patakatifu pake. Mtakuwa makini kufanya kila kitu ambacho wanawaelekeza kufanya.
11 You shall do according to the law and to the judgement which they shall declare to you: you shall not swerve to the right hand or to the left from any sentence which they shall report to you.
Fuata sheria wanayowafundisha, na kufanya kulingana na maamuzi wanawapa. Msigeuke kutoka kwa kile wanawambia, kwa kulia au kushoto.
12 And the man whoever shall act in haughtiness, so as not to listen to the priest who stands to minister in the name of the Lord your God, or the judge who shall preside in those days, that man shall die, and you shall remove the evil one out of Israel.
Yeyote anayefanya kwa kiburi, kwa kutomsikiliza kuhani anayesimama kutumika mbele ya Yahwe Mungu wako, au kwa kutomsikiliza mwamuzi- huyu mtu atakufa; mtaweka mbali uovu kutoka Israeli.
13 And all the people shall hear and fear, and shall no more commit impiety.
Watu wote wanapaswa kusikia na kuogopa, na kutofanya kwa kiburi tena.
14 And when you shall enter into the land which the Lord your God gives you, and shall inherit it and dwell in it, and shall say, I will set a ruler over me, as also the other nations round about me;
Wakati mlipokuja kwenye nchi ambayo Yahwe Mungu anawapa, na wakati mnamiliki na kuanza kuishi ndani yake, na halafu unasema, 'Nitajiwekea mfalme juu yangu, kama mataifa yote yanayonizunguka mimi,'
15 you shall surely set over you the ruler whom the Lord God shall choose: of your brethren you shall set over you a ruler; you shall not have power to set over you a stranger, because he is not your brother.
basi unapaswa kwa hakika kujiwekea mfalme juu yako mtu yeyote ambaye Yahwe atachagua. Unapaswa kujiweka kama mfalme juu yako mtu yeyote kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Haupaswi kuweka mgeni, ambaye si ndugu yenu, juu yenu.
16 For he shall not multiply to himself horses, and he shall by no means turn the people back to Egypt, lest he should multiply to himself horses; for the Lord said, You shall not any more turn back by that way.
Lakini hapaswi kuzidisha farasi kwa ajili yake, wala kusababisha watu kurudi Misri ili kwamba aweze kuzidisha farasi, kwa kuwa Yahwe alikwisha sema kwako, 'Unapaswa kuanzia sasa usirudi njia hiyo tena.'
17 And he shall not multiply to himself wives, lest his heart turn away; and he shall not greatly multiply to himself silver and gold.
Na hapaswi kuzidisha wake kwa ajili yake, ili kwamba moyo wake usigeuke kotoka kwa Yahwe; wala hapaswi sana kuzidisha kwa ajili yake fedha au dhahabu.
18 And when he shall be established in his government, then shall he write for himself this repetition of the law into a book by the hands of the priests the Levites;
Wakati aketipo kwenye kiti cha enzi cha ufalme wake, anapaswa kuandika kwenye kitabu kwa ajili yake nakala ya sheria hii, kutoka kwenye sheria ambayo iko mbele ya makuhani, ambao ni Walawi.
19 and it shall be with him, and he shall read in it all the days of his life, that he may learn to fear the Lord your God, and to keep all these commandments, and to observe these ordinances:
Kitabu kinapaswa kuwa na yeye, na anapaswa kusoma ndani yake kwa siku zake zote, ili kwamba aweze kujifunza kumheshimu Yahwe Mungu wako, ili kwamba ashike maneno yote ya sheria hii na amri hizi, kuzishika.
20 that his heart be not lifted up above his brethren, that he depart not from the commandments on the right hand or on the left; that he and his sons may reign long in his dominion amongst the children of Israel.
Anapaswa kufanya hivi ili kwamba moyo wake usiinuliwe zaidi ya ndugu zake, na ili kwamba asigeuke mbali na amri, kwa kulia au kwa kushoto' kwa kusudi kwamba aweze kuzidisha siku zake katika ufalme wake, yeye na watoto wake, miongoni mwa Israel.

< Deuteronomy 17 >