< Deuteronomy 14 >
1 You are the children of the Lord your God: you shall not make any baldness between you eyes for the dead.
Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
2 For you are a holy people to the Lord your God, and the Lord your God has chosen you to be a peculiar people to himself of all the nations on the face of the earth.
kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
3 You shall not eat any abominable thing.
Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
4 These [are] the beasts which you shall eat; the calf of the herd, and lamb of the sheep, and kid of the goats;
Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
5 the stag, and doe, and pygarg, and wild goat, and camelopard.
kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
6 Every beast that divides the hoofs, and makes claws of two divisions, and that chews the cud amongst beasts, these you shall eat.
Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
7 And these you shall not eat of them that chew the cud, and of those that divide the hoofs, and make distinct claws; the camel, and the hare, and the rabbit; because they chew the cud, and do not divide the hoof, these are unclean to you.
Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
8 And as for the swine, because he divides the hoof, and makes claws of the hoof, yet he chews not the cud, he is unclean to you; you shall not eat of their flesh, you shall not touch their dead bodies.
Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
9 And these you shall eat of all that are in the water, you shall eat all that have fins and scales.
Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
10 And all that have not fins and scales you shall not eat; they are unclean to you.
Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
11 You shall eat every clean bird.
Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
12 And these of them you shall not eat; the eagle, and the ossifrage, and the sea-eagle,
Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
13 and the vulture, and the kite and the like to it,
kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
15 and the sparrow, and the owl, and the cormorant,
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
16 and the heron, and the swan, and the stork,
bundi, mumbi, bundi mkubwa,
17 and the cormorant, and the hawk, and its like, and the hoopoe, and the raven,
mwari, nderi, mnandi,
18 and the pelican, and the diver and the like to it, and the red-bill and the bat.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
19 All winged animals that creep are unclean to you; you shall not eat of them.
Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
20 You shall eat every clean bird.
Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
21 You shall eat nothing that dies of itself; it shall be given to the sojourner in your cities and he shall eat it, or you shall sell it to a stranger, because you are a holy people to the Lord your God. You shall not boil a lamb in his mother's milk.
Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
22 You shall tithe a tenth of all the produce of your seed, the fruit of your field year by year.
Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
23 And you shall eat it in the place which the Lord your God shall choose to have his name called there; you shall bring the tithe of your corn and of your wine, and of your oil, the firstborn of your herd and of your flock, that you may learn to fear the Lord your God always.
Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
24 And if the journey be too far for you, and you are not able to bring them, because the place [is] far from you which the Lord your God shall choose to have his name called there, because the Lord your God will bless you;
Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
25 then you shall sell them for money, and you shall take the money in your hands, and you shall go to the place which the Lord your God shall choose.
basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
26 And you shall give the money for whatever your soul shall desire, for oxen or for sheep, or for wine, or [you shall lay it out] on strong drink, or on whatever your soul may desire, and you shall eat there before the Lord your God, and you shall rejoice and your house,
Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
27 and the Levite that is in your cities, because he has not a portion or inheritance with you.
Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
28 After three years you shall bring out all the tithes of your fruits, in that year you shall lay it up in your cities.
Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
29 And the Levite shall come, because he has no part or lot with you, and the stranger, and the orphan, and the widow which is in your cities; and they shall eat and be filled, that the Lord your God may bless you in all the works which you shall do.
ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.