< Chronicles I 6 >
1 The sons of Levi: Gedson, Caath, and Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 And the sons of Caath; Ambram, and Issaar, Chebron, and Oziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 And the sons of Ambram; Aaron, and Moses, and Mariam: and the sons of Aaron; Nadab, and Abiud, Eleazar, and Ithamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Eleazar begot Phinees, Phinees begot Abisu;
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 Abisu begot Bokki, and Bokki begot Ozi;
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 Ozi begot Zaraia, Zaraia begot Mariel;
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 and Mariel begot Amaria, and Amaria begot Achitob;
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 and Achitob begot Sadoc, and Sadoc begot Achimaas;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 and Achimaas begot Azarias, and Azarias begot Joanan;
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 and Joanan begot Azarias: he ministered as priest in the house which Solomon built in Jerusalem.
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 And Azarias begot Amaria, and Amaria begot Achitob;
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 and Achitob begot Sadoc, and Sadoc begot Salom;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 and Salom begot Chelcias, and Chelcias begot Azarias;
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 and Azarias begot Saraia, and Saraias begot Josadac.
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 And Josadac went into captivity with Juda and Jerusalem under Nabuchodonosor.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 The sons of Levi: Gedson, Caath, and Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 And these [are] the names of the sons of Gedson; Lobeni, and Semei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 The sons of Caath; Ambram, and Issaar, Chebron, and Oziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 The sons of Merari; Mooli and Musi: and these [are] the families of Levi, according to their families.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 To Gedson—to Lobeni his son—[were born] Jeth his son, Zammath his son,
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Joab his son, Addi his son, Zara his son, Jethri his son.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 The sons of Caath; Aminadab his son, Core his son, Aser his son;
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Helcana his son, Abisaph his son, Aser his son:
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Thaath his son, Uriel his son, Ozia his son, Saul his son.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 And the sons of Helcana; Amessi, and Achimoth.
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 Helcana his son, Suphi his son, Cainaath his son;
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Eliab his son, Jeroboam his son, Helcana his son.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 The sons of Samuel; the firstborn Sani, and Abia.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 The sons of Merari; Mooli, Lobeni his son, Semei his son, Oza his son;
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 Samaa his son, Angia his son, Asaias his son.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 And these [were the men] whom David set over the service of the singers in the house of the Lord when the ark was at rest.
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 And they ministered in front of the tabernacle of witness [playing] on instruments, until Solomon built the house of the Lord in Jerusalem; and they stood according to their order for their services.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 And these [were the men] that stood, and their sons, of the sons of Caath: Aeman the psalm singer, son of Joel, the son of Samuel,
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 the son of Helcana, the son of Jeroboam, the son of Eliel, the son of Thoas,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 the son of Suph, the son of Helcana, the son of Maath, the son of Amathi,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 the son of Helcana, the son of Joel, the son of Azarias, the son of Japhanias,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 the son of Thaath, the son of Aser, the son of Abiasaph, the son of Core,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 the son of Isaar, the son of Caath, the son of Levi, the son of Israel.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 And his brother Asaph, who stood at his right hand; Asaph the son of Barachias, the son of Samaa,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 the son of Michael, the son of Baasia, the son of Melchia,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 the son of Athani, the son of Zaarai,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 the son of Adai, the son of Aetham, the son of Zammam, the son of Semei,
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 the son of Jeeth, the son of Gedson, the son of Levi.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 And the sons of Merari their brethren on the left hand: Aetham the son of Kisa, the son of Abai, the son of Maloch,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 the son of Amessias, the son of Bani, the son of Semer,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 the son of Mooli, the son of Musi, the son of Merari, the son of Levi.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 And their brethren according to the houses of their fathers, [were] the Levites who were appointed to all the work of ministration of the tabernacle of the house of God.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 And Aaron and his sons [were] to burn incense on the altar of whole burnt offerings, and on the altar of incense, for all the ministry [in] the holy of holies, and to make atonement for Israel, according to all things that Moses the servant of the Lord commanded.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 And these [are] the sons of Aaron; Eleazar his son, Phinees his son, Abisu his son,
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Bokki his son, Ozi his son, Saraia his son,
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Mariel his son, Amaria his son, Achitob his son,
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Sadoc his son, Achimaas his son.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 And these [are] their residences in their villages, in their coasts, to the sons of Aaron, to their family the Caathites: for they had the lot.
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 And they gave them Chebron in the land of Juda, and its suburbs round about it.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 But the fields of the city, and its villages, they gave to Chaleb the son of Jephonne.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 And to the sons of Aaron they gave the cities of refuge, [even] Chebron, and Lobna and her suburbs round about, and Selna and her suburbs, and Esthamo and her suburbs,
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
58 and Jethar and her suburbs, and Dabir and her suburbs,
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 and Asan and her suburbs, and Baethsamys and her suburbs:
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 and of the tribe of Benjamin Gabai and her suburbs, and Galemath and her suburbs, and Anathoth and her suburbs: all their cities [were] thirteen cities according to their families.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 And to the sons of Caath that were left of their families, [there were given] out of the tribe, [namely], out of the half-tribe of Manasse, by lot, ten cities.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 And to the sons of Gedson according to their families [there were given] thirteen cities of the tribe of Issachar, of the tribe of Aser, of the tribe of Nephthali, of the tribe of Manasse in Basan.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 And to the sons of Merari according to their families [there were given], by lot, twelve cities of the tribe of Ruben, of the tribe of Gad, [and] of the tribe of Zabulon.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 So the children of Israel gave to the Levites the cities and their suburbs.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 And they gave by lot out of the tribe of the children of Juda, and out of the tribe of the children of Symeon, and out of the tribe of the children of Benjamin, these cities which they call by name.
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 And [to the members] of the families of the sons of Caath there were also given the cities of their borders out of the tribe of Ephraim.
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 And they gave them the cities of refuge, Sychem and her suburbs in mount Ephraim, and Gazer and her suburbs,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
68 and Jecmaan and her suburbs, and Baethoron and her suburbs,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 and Aelon and her suburbs, and Gethremmon and her suburbs:
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 and of the half-tribe of Manasse Anar and her suburbs, and Jemblaan and her suburbs, to the sons of Caath that were left, according to [each several] family.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 To the sons of Gedson from the families of the half-tribe of Manasse [they gave] Golan of Basan and her suburbs, and Aseroth and her suburbs.
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 And out of the tribe of Issachar, Kedes and her suburbs, and Deberi and her suburbs, and Dabor and her suburbs,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 and Ramoth, and Aenan and her suburbs.
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 And of the tribe of Aser; Maasal and her suburbs, and Abdon and her suburbs,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 and Acac and her suburbs, and Roob and her suburbs.
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 And of the tribe of Nephthali; Kedes in Galilee and her suburbs, and Chamoth and her suburbs, and Kariathaim and her suburbs.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 To the sons of Merari that were left, [they gave] out of the tribe of Zabulon Remmon and her suburbs, and Thabor and her suburbs:
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 out of [the country] beyond Jordan; Jericho westward of Jordan: out of the tribe of Ruben; Bosor in the wilderness and her suburbs, and Jasa and her suburbs,
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 and Kadmoth and her suburbs, and Maephla and her suburbs.
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 Out of the tribe of Gad; Rammoth Galaad and her suburbs, and Maanaim and her suburbs,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 and Esebon and her suburbs, and Jazer and her suburbs.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.