< Psalms 85 >

1 For the end, a Psalm for the sons of Core. O Lord, thou has taken pleasure in thy land: thou hast turned back the captivity of Jacob.
Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
2 Thou hast forgiven thy people their transgressions; thou has covered all their sins. (Pause)
Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
3 Thou has caused all thy wrath to cease: thou hast turned from thy fierce anger.
Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
4 Turn us, O God of our salvation, and turn thy anger away from us.
Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
5 Wouldest thou be angry with us for ever? or wilt thou continue thy wrath from generation to generation?
Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
6 O God, thou wilt turn and quicken us; and thy people shall rejoice in thee.
Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
7 Shew us thy mercy, O Lord, and grant us thy salvation.
Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
8 I will hear what the Lord God will say concerning me: for he shall speak peace to his people, and to his saints, and to those that turn their heart toward him.
Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
9 Moreover his salvation is near them that fear him; that glory may dwell in our land.
Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
10 Mercy and truth are met together: righteousness and peace have kissed [each other].
Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
11 Truth has sprung out of the earth; and righteousness has looked down from heaven.
Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
12 For the Lord will give goodness; and our land shall yield her fruit.
Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
13 Righteousness shall go before him; and shall set his steps in the way.
Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.

< Psalms 85 >