< Psalms 142 >

1 [A Psalm] of instruction for David, when he was in the cave, —a Prayer. I cried to the Lord with my voice; with my voice I made supplication to the Lord.
Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
2 I will pour out before him my supplication: I will declare before him mine affliction.
Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
3 When my spirit was fainting within me, then thou knewest my paths; in the very way wherein I was walking, they hid a snare for me.
Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
4 I looked on [my] right hand, and behold, for there was none that noticed me; refuge failed me; and there was none that cared for my soul.
Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
5 I cried unto thee, O Lord, and said, Thou art my hope, my portion in the land of the living.
Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 Attend to my supplication, for I am brought very low; deliver me from them that persecute me; for they are stronger than I.
Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
7 Bring my soul out of prison, that I may give thanks to thy name, O Lord; the righteous shall wait for me, until thou recompense me.
Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”

< Psalms 142 >