< Psalms 113 >

1 Alleluia. Praise the Lord, ye servants [of his], praise, the name of the Lord.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Let the name of the Lord be blessed, from this present time and for ever.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 From the rising of the sun to his setting, the name of the Lord is to be praised.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 The Lord is high above all the nations; his glory is above the heavens.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Who is as the Lord our God? who dwells in the high places,
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 and [yet] looks upon the low things in heaven, and on the earth:
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 who lifts up the poor from the earth, and raises up the needy from the dunghill;
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 to set him with princes, [even] with the princes of his people:
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 who settles the barren [woman] in a house, [as] a mother rejoicing over children.
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Psalms 113 >