< Proverbs 27 >

1 Boast not of to-morrow; for thou knowest not what the next day shall bring forth.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
2 Let thy neighbour, and not thine own mouth, praise thee; a stranger, and not thine own lips.
Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
3 A stone is heavy, and sand cumbersome; but a fool's wrath is heavier than both.
Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
4 Wrath is merciless, and anger sharp: but envy can bear nothing.
Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
5 Open reproofs are better than secret love.
Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
6 The wounds of a friend are more to be trusted than the spontaneous kisses of an enemy.
Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
7 A full soul scorns honeycombs; but to a hungry soul even bitter things appear sweet.
Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
8 As when a bird flies down from its own nest, so a man is brought into bondage whenever he estranges himself from his own place.
Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
9 The heart delights in ointments and wines and perfumes: but the soul is broken by calamities.
Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
10 Thine own friend, and thy father's friend, forsake not; and when thou art in distress go not into thy brother's house: better is a friend [that is] near than a brother living far off.
Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
11 Son, be wise, that thy heart may rejoice; and remove thou from thyself reproachful words.
Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
12 A wise man, when evils are approaching, hides himself; but fools pass on, and will be punished.
Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
13 Take away the man's garment, (for a scorner has passed by) whoever lays waste another's goods.
vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
14 Whosoever shall bless a friend in the morning with a loud voice, shall seem to differ nothing from one who curses [him].
Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
15 On a stormy day drops [of rain] drive a man out of his house; so also does a railing woman [drive a man] out of his own house.
Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
16 The north wind is sharp, but it is called by name propitious.
kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
17 Iron sharpens iron; and a man sharpens his friend's countenance.
Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
18 He that plants a fig-tree shall eat the fruits of it: so he that waits on his own master shall be honoured.
Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
19 As faces are not like [other] faces, so neither are the thoughts of men.
Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
20 Hell and destruction are not filled; so also are the eyes of men insatiable. [He that fixes his eye is an abomination to the Lord; and the uninstructed do not restrain their tongue.] (Sheol h7585)
Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
21 Fire is the trial for silver and gold; and a man is tried by the mouth of them that praise him. The heart of the transgressor seeks after mischiefs; but an upright heart seeks knowledge.
Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
22 Though thou scourge a fool, disgracing him in the midst of the council, thou wilt [still] in no wise remove his folly from him.
Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
23 Do thou thoroughly know the number of thy flock, and pay attention to thine herds.
Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
24 For a man [has] not strength and power for ever; neither does he transmit it from generation to generation.
maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
25 Take care of the herbage in the field, and thou shalt cut grass, and gather the mountain hay;
Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
26 that thou mayest have [wool of] sheep for clothing: pay attention to the land, that thou mayest have lambs.
Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
27 [My] son, thou hast from me words very useful for thy life, and for the life of thy servants.
Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.

< Proverbs 27 >