< Joshua 12 >
1 And these [are] the kings of the land, whom the children of Israel slew, and inherited their land beyond Jordan from the east, from the valley of Arnon to the mount of Aermon, and all the land of Araba on the east.
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Seon king of the Amorites, who dwelt in Esebon, ruling from Arnon, which is in the valley, on the side of the valley, and half of Galaad as far as Jaboc, the borders of the children of Ammon.
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 And Araba as far as the sea of Chenereth eastward, and as far as the sea of Araba; the salt sea eastward [by] the way to Asimoth, from Thaeman under Asedoth Phasga.
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 And Og king of Basan, who dwelt in Astaroth and in Edrain, was left of the giants
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 ruling from mount Aermon and from Secchai, and [over] all the land of Basan to the borders of Gergesi, and Machi, and the half of Galaad of the borders of Seon king of Esebon.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moses the servant of the Lord and the children of Israel smote them; and Moses gave them by way of inheritance to Ruben, and Gad, and to the half tribe of Manasse.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 And these [are] the kings of the Amorites, whom Joshua and the children of Israel slew beyond Jordan by the sea of Balagad in the plain of Libanus, and as far as the mountain of Chelcha, as men go up to Seir: and Joshua gave it to the tribes of Israel to inherit according to their portion;
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 in the mountain, and in the plain, and in Araba, and in Asedoth, and in the wilderness, and Nageb; the Chettite, and the Amorite, and the Chananite, and the Pherezite, and the Evite, and the Jebusite.
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 The king of Jericho, and the king of Gai, which is near Baethel;
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 the king of Jerusalem, the king of Chebron,
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 the king of Jerimuth, the king of Lachis;
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 the king of Aelam, the king of Gazer;
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 the king of Dabir, the king of Gader:
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 the king of Hermath, the king of Ader;
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 the king of Lebna, the king of Odollam,
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 the king of Taphut, the king of Opher,
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 the king of Ophec of Aroc,
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 the king of Symoon, the king of Mambroth, the king of Aziph,
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 the king of Cades, the king of Zachac,
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 the king of Maredoth, the king of Jecom of Chermel,
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 the king of Odollam [belonging to] Phennealdor, the king of Gei of Galilee:
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 the king of Thersa: all these [were] twenty-nine kings.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.