< Job 38 >

1 And after Elius had ceased from speaking, the Lord spoke to Job through the whirlwind and clouds, [saying],
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Who is this that hides counsel from me, and confines words in [his] heart, and thinks to conceal [them] from me?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Gird thy loins like a man; and I will ask thee, and do thou answer me.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Where wast thou when I founded the earth? tell me now, if thou hast knowledge,
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 who set the measures of it, if thou knowest? or who stretched a line upon it?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 On what are its rings fastened? and who is he that laid the corner-stone upon it?
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 When the stars were made, all my angels praised me with a loud voice.
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 And I shut up the sea with gates, when it rushed out, coming forth out its mother's womb.
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 And I made a cloud its clothing, and swathed it in mist.
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 And I set bounds to it, surrounding it with bars and gates.
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 And I said to it, Hitherto shalt thou come, but thou shalt not go beyond, but thy waves shall be confined within thee.
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Or did I order the morning light in thy time; and [did] the morning star [then first] see his appointed place;
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 to lay hold of the extremities of the earth, to cast out the ungodly out of it?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Or didst thou take clay of the ground, and form a living creature, and set it with the power of speech upon the earth?
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 And hast thou removed light from the ungodly, and crushed the arm of the proud?
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Or hast thou gone to the source of the sea, and walked in the tracks of the deep?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 And do the gates of death open to thee for fear; and did the porters of hell quake when they saw thee? (questioned)
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 And hast thou been instructed in the breadth of the [whole earth] under heaven? tell me now, what is the extent of it?
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 And in what kind of a land does the light dwell? and of what kind is the place of darkness?
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 If thou couldest bring me to their [utmost] boundaries, and if also thou knowest their paths;
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 I know then that thou wert born at that time, and the number of thy years is great.
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 But hast thou gone to the treasures of snow? and hast thou seen the treasures of hail?
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 And is there a store [of them], for thee against the time of [thine] enemies, for the day of wars and battle?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 And whence proceeds the frost? or [whence] is the south wind dispersed over the [whole world] under heaven?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 And who prepared a course for the violent rain, and a way for the thunders;
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 to rain upon the land where [there is] no man, the wilderness, where there is not a man in it; so as to feed the untrodden and uninhabited [land],
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 and cause it to send forth a crop of green herbs?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Who is the rain's father? and who has generated the drops of dew?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 And out of whose womb comes the ice? and who has produced the frost in the sky,
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 which descends like flowing water? who has terrified the face of the ungodly?
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 And dost thou understand the band of Pleias, and hast thou opened the barrier of Orion?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Or wilt thou reveal Mazuroth in his season, and the evening star with his rays? Wilt thou guide them?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 And knowest thou the changes of heaven, or the events which take place together under heaven?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 And wilt thou call a cloud with thy voice, and will it obey thee with a violent shower of much rain?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 And wilt thou send lightnings, and they shall go? and shall they say to thee, What is [thy pleasure]?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 And who has given to women skill in weaving, or knowledge of embroidery?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 And who is he that numbers the clouds in wisdom, and has bowed the heaven [down] to the earth?
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 For it is spread out as dusty earth, and I have cemented it as one hewn stone to another.
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 And wilt thou hunt a prey for the lions? and satisfy the desires of the serpents?
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 For they fear in their lairs, and lying in wait couch in the woods.
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 And who has prepared food for the raven? for its young ones wander and cry to the Lord, in search of food.
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >