< Esias 43 >
1 And now thus saith the Lord God that made thee, O Jacob, and formed thee, O Israel, Fear not: for I have redeemed thee, I have called thee [by] thy name; thou art mine.
Lakini sasa hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyekuumba, ee Yakobo, yeye aliyekuhuluku, ee Israeli: “Usiogope kwa maana nimekukomboa, nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu.
2 And if thou pass through water, I am with thee; and the rivers shall not overflow thee: and if thou go through fire, thou shalt not be burned; the flame shall not burn thee.
Unapopita kwenye maji makuu, nitakuwa pamoja nawe, unapopita katika mito ya maji, hayatakugharikisha. Utakapopita katika moto, hutaungua, miali ya moto haitakuunguza.
3 For I am the Lord thy God, the Holy One of Israel, that saves thee: I have made Egypt and Ethiopia thy ransom, and [given] Soene for thee.
Kwa kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Ninaitoa Misri kuwa fidia yako, Kushi na Seba badala yako.
4 Since thou becamest precious in my sight, thou hast become glorious, and I have loved thee: and I will give men for thee, and princes for thy life.
Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu, nami kwa kuwa ninakupenda, nitatoa watu badala yako na mataifa badala ya maisha yako.
5 Fear not; for I am with thee: I will bring thy seed from the east, and will gather thee from the west.
Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe, nitawaleta watoto wako kutoka mashariki, na kukukusanya kutoka magharibi.
6 I will say to the north, Bring; and to the south, Keep not back; bring my sons from the [land] afar off, and my daughters from the ends of the earth;
Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’ nayo kusini, ‘Usiwazuie.’ Walete wana wangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka miisho ya dunia:
7 [even] all who are called by my name: for I have prepared him for my glory, and I have formed him, and have made him:
kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu, niliyemuumba kwa utukufu wangu, niliyemhuluku na kumfanya.”
8 and I have brought forth the blind people; for [their] eyes are alike blind, and they that have ears are deaf.
Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni, wenye masikio lakini hawasikii.
9 All the nations are gathered together, and princes shall be gathered out of them: who will declare these things? or who will declare to you things from the beginning? let them bring forth their witnesses, and be justified; and let them hear, and declare the truth.
Mataifa yote yanakutanika pamoja, na makabila yanakusanyika. Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya, na kututangazia mambo yaliyopita? Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi, ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.”
10 Be ye my witnesses, and I [too am] a witness, saith the Lord God, and my servant whom I have chosen: that ye may know, and believe, and understand that I am [he]: before me there was no other God, and after me there shall be none.
“Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “na mtumishi wangu niliyemchagua, ili mpate kunijua na kuniamini, na kutambua kwamba Mimi ndiye. Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa, wala hatakuwepo mwingine baada yangu.
11 I am God; and beside me there is no Saviour.
Mimi, naam mimi, ndimi Bwana, zaidi yangu hakuna mwokozi.
12 I have declared, and have saved; I have reproached, and there was no strange [god] among you: ye are my witnesses, and I am the Lord God,
Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza: Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu. Ninyi ni mashahidi wangu,” asema Bwana, “kwamba Mimi ndimi Mungu.
13 even from the beginning; and there is none that can deliver out of my hands: I will work, and who shall turn it back?
Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye. Hakuna hata mmoja awezaye kuokoa kutoka mkononi wangu. Mimi ninapotenda, ni nani awezaye kutangua?”
14 Thus saith the Lord God that redeems you, the Holy One of Israel; for your sakes I will send to Babylon, and I will stir up all that flee, and the Chaldeans shall be bound in ships.
Hili ndilo Bwana asemalo, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa ajili yenu nitatumana Babeli na kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi, katika meli walizozionea fahari.
15 I am the Lord God, your Holy One, who have appointed for Israel your king.
Mimi ndimi Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wako, Muumba wa Israeli, Mfalme wako.”
16 Thus saith the Lord, who makes a way in the sea, and a path in the mighty water;
Hili ndilo asemalo Bwana, yeye aliyefanya njia baharini, mahali pa kupita kwenye maji mengi,
17 who brought forth chariots and horse, and a mighty multitude: but they have lain down, and shall not rise: they are extinct, as quenched flax.
aliyeyakokota magari ya vita na farasi, jeshi pamoja na askari wa msaada, nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe, wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi:
18 Remember ye not the former things, and consider not the ancient things.
“Msiyakumbuke mambo yaliyopita, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
19 Behold, I [will] do new things, which shall presently spring forth, and ye shall know them: and I will make a way in the wilderness, and rivers in the dry land.
Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame.
20 the beasts of the field shall bless me, the owls and young ostriches; for I have given water in the wilderness, and rivers in the dry land, to give drink to my chosen race,
Wanyama wa mwituni wataniheshimu, mbweha na bundi, kwa sababu ninawapatia maji jangwani, na vijito katika nchi kame, ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua,
21 my people whom I have preserved to tell forth my praises.
watu wale niliowaumba kwa ajili yangu, ili wapate kutangaza sifa zangu.
22 I have not now called thee, O Jacob; neither have I made thee weary, O Israel.
“Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo, hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli.
23 Thou hast not brought me the sheep of thy whole-burnt-offering; neither hast thou glorified me with thy sacrifices. I have not caused thee to serve with sacrifices, neither have I wearied thee with frankincense.
Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa dhabihu zako. Sikukulemea kwa sadaka za nafaka wala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba.
24 Neither hast thou purchased for me victims for silver, neither have I desired the fat of thy sacrifices: but thou didst stand before me in thy sins, and in thine iniquities.
Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato, wala hukunipa kwa ukarimu mafuta ya wanyama wa dhabihu zako. Lakini umenilemea kwa dhambi zako, na kunitaabisha kwa makosa yako.
25 I, [even] I, am he that blots out thy transgressions for mine own sake, and thy sins; and I will not remember [them].
“Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako, kwa ajili yangu mwenyewe, wala sizikumbuki dhambi zako tena.
26 But do thou remember, and let us plead [together]: do thou first confess thy transgressions, that thou mayest be justified.
Tafakari mambo yaliyopita, njoo na tuhojiane, leta shauri lako uweze kupewa haki yako.
27 Your fathers first, and your princes have transgressed against me.
Baba yako wa kwanza alitenda dhambi, wasemaji wako wameasi dhidi yangu.
28 And the princes have defiled my sanctuaries: so I gave Jacob [to enemies] to destroy, and Israel to reproach.
Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako, nami nitamtoa Yakobo aangamizwe, na Israeli adhihakiwe.