< Genesis 22 >
1 And it came to pass after these things that God tempted Abraam, and said to him, Abraam, Abraam; and he said, Lo! I [am here].
Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!” Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”
2 And he said, Take thy son, the beloved one, whom thou hast loved—Isaac, and go into the high land, and offer him there for a whole-burnt-offering on one of the mountains which I will tell thee of.
Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
3 And Abraam rose up in the morning and saddled his ass, and he took with him two servants, and Isaac his son, and having split wood for a whole-burnt-offering, he arose and departed, and came to the place of which God spoke to him,
Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia.
4 on the third day; and Abraam having lifted up his eyes, saw the place afar off.
Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali.
5 And Abraam said to his servants, Sit ye here with the ass, and I and the lad will proceed thus far, and having worshipped we will return to you.
Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”
6 And Abraam took the wood of the whole-burnt-offering, and laid it on Isaac his son, and he took into his hands both the fire and the knife, and the two went together.
Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja,
7 And Isaac said to Abraam his father, Father. And he said, What is it, son? And he said, Behold the fire and the wood, where is the sheep for a whole-burnt-offering?
Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!” Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.” Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
8 And Abraam said, God will provide himself a sheep for a whole-burnt-offering, [my] son. And both having gone together,
Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.
9 came to the place which God spoke of to him; and there Abraam built the altar, and laid the wood on it, and having bound the feet of Isaac his son together, he laid him on the altar upon the wood.
Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni.
10 And Abraam stretched forth his hand to take the knife to slay his son.
Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe.
11 And an angel of the Lord called him out of heaven, and said, Abraam, Abraam. And he said, Behold, I [am here].
Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!” Akajibu, “Mimi hapa.”
12 And he said, Lay not thine hand upon the child, neither do anything to him, for now I know that thou fearest God, and for my sake thou hast not spared thy beloved son.
Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”
13 And Abraam lifted up his eyes and beheld, and lo! a ram caught by his horns in a plant of Sabec; and Abraam went and took the ram, and offered him up for a whole-burnt-offering in the place of Isaac his son.
Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
14 And Abraam called the name of that place, The Lord hath seen; that they might say to-day, In the mount the Lord was seen.
Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”
15 And an angel of the Lord called Abraam the second time out of heaven, saying, I have sworn by myself, says the Lord, because thou hast done this thing, and on my account hast not spared thy beloved son,
Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
16 surely blessing I will bless thee, and multiplying I will multiply thy seed as the stars of heaven, and as the sand which is by the shore of the sea, and thy seed shall inherit the cities of their enemies.
akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
17 And in thy seed shall all the nations of the earth be blessed, because thou hast hearkened to my voice.
hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
18 And Abraam returned to his servants, and they arose and went together to the well of the oath; and Abraam dwelt at the well of the oath.
na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
19 And it came to pass after these things, that it was reported to Abraam, saying, Behold, Melcha herself too has born sons to Nachor thy brother,
Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
20 Uz the first-born, and Baux his brother, and Camuel the father of the Syrians, and Chazad, and
Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana:
21 Azav and Phaldes, and Jeldaph, and Bathuel, and Bathuel begot Rebecca;
Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu),
22 these are eight sons, which Melcha bore to Nachor the brother of Abraam.
Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.”
23 And his concubine whose name was Rheuma, she also bore Tabec, and Taam, and Tochos, and Mocha.
Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane.
Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.