< Psalms 1 >
1 Happy is the man who does not go in the company of sinners, or take his place in the way of evil-doers, or in the seat of those who do not give honour to the Lord.
Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
2 But whose delight is in the law of the Lord, and whose mind is on his law day and night.
Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
3 He will be like a tree planted by the rivers of water, which gives its fruit at the right time, whose leaves will ever be green; and he will do well in all his undertakings.
Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
4 The evil-doers are not so; but are like the dust from the grain, which the wind takes away.
Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 For this cause there will be no mercy for sinners when they are judged, and the evil-doers will have no place among the upright,
Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 Because the Lord sees the way of the upright, but the end of the sinner is destruction.
Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.