< Psalms 68 >

1 To the chief music-maker. Of David. A Psalm. A Song. Let God be seen, and let his haters be put to flight; let those who are against him be turned back before him.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 Let them be like smoke before the driving wind; as wax turning soft before the fire, so let them come to an end before the power of God.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 But let the upright be glad; let them have delight before God; let them be full of joy.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Make songs to God, make songs of praise to his name; make a way for him who comes through the waste lands; his name is Jah; be glad before him.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 A father to those who have no father, a judge of the widows, is God in his holy place.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 Those who are without friends, God puts in families; he makes free those who are in chains; but those who are turned away from him are given a dry land.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 O God, when you went out before your people, wandering through the waste land; (Selah)
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 The earth was shaking and the heavens were streaming, because God was present; even Sinai itself was moved before God, the God of Israel.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 You, O God, did freely send the rain, giving strength to the weariness of your heritage.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 Those whose resting-place was there, even the poor, were comforted by your good things, O God.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 The Lord gives the word; great is the number of the women who make it public.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 Kings of armies quickly go in flight: and the women in the houses make a division of their goods.
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 Will you take your rest among the flocks? like the wings of a dove covered with silver, and its feathers with yellow gold.
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 When the Most High put the kings to flight, it was as white as snow in Salmon.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 A hill of God is the hill of Bashan; a hill with high tops is the hill of Bashan.
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 Why are you looking with envy, you high hills, on the hill desired by God as his resting-place? truly, God will make it his house for ever.
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 The war-carriage of God is among Israel's thousands; the Lord has come from Sinai to the holy place.
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 You have gone up on high, taking your prisoners with you; you have taken offerings from men; the Lord God has taken his place on the seat of his power.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 Praise be to the Lord, who is our support day by day, even the God of our salvation. (Selah)
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 Our God is for us a God of salvation; his are the ways out of death.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 The heads of the haters of God will be crushed; even the head of him who still goes on in his evil ways.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 The Lord said, I will make them come back from Bashan, and from the deep parts of the sea;
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 So that your foot may be red with blood, and the tongues of your dogs with the same.
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 We see your going, O God: even the going of my God, my King, into the holy place.
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 The makers of songs go before, the players of music come after, among the young girls playing on brass instruments.
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 Give praise to God in the great meeting; even the Lord, you who come from the fountain of Israel.
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 There is little Benjamin ruling them, the chiefs of Judah and their army, the rulers of Zebulun and the rulers of Naphtali.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 O God, send out your strength; the strength, O God, with which you have done great things for us,
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 Out of your Temple in Jerusalem.
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Say sharp words to the beast among the water-plants, the band of strong ones, with the lords of the peoples, put an end to the people whose delight is in war.
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Kings will give you offerings, they will come out of Egypt; from Pathros will come offerings of silver; Ethiopia will be stretching out her hands to God.
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Make songs to God, you kingdoms of the earth; O make songs of praise to the Lord; (Selah)
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 To him who goes or the clouds of heaven, the heaven which was from earliest times; he sends out his voice of power.
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 Make clear that strength is God's: he is lifted up over Israel, and his power is in the clouds.
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 O God, you are to be feared in your holy place: the God of Israel gives strength and power to his people. Praise be to God.
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Psalms 68 >