< Psalms 46 >
1 To the chief music-maker. Of the sons of Korah; put to Alamoth. A Song. God is our harbour and our strength, a very present help in trouble.
Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
2 For this cause we will have no fear, even though the earth is changed, and though the mountains are moved in the heart of the sea;
Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
3 Though its waters are sounding and troubled, and though the mountains are shaking with their violent motion. (Selah)
hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
4 There is a river whose streams make glad the resting-place of God, the holy place of the tents of the Most High.
Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
5 God has taken his place in her; she will not be moved: he will come to her help at the dawn of morning.
Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
6 The nations were angry, the kingdoms were moved; at the sound of his voice the earth became like wax.
Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
7 The Lord of armies is with us; the God of Jacob is our high tower. (Selah)
Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
8 Come, see the works of the Lord, the destruction which he has made in the earth.
Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
9 He puts an end to wars over all the earth; by him the bow is broken, and the spear cut in two, and the carriage burned in the fire.
Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
10 Be at peace in the knowledge that I am God: I will be lifted up among the nations, I will be honoured through all the earth.
Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
11 The Lord of armies is with us; the God of Jacob is our high tower. (Selah)
Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah