< Psalms 34 >

1 Of David. When he made a change in his behaviour before Abimelech, who sent him away, and he went. I will be blessing the Lord at all times; his praise will be ever in my mouth.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 My soul will say great things of the Lord: the poor in spirit will have knowledge of it and be glad.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 O give praise to the Lord with me; let us be witnesses together of his great name.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 I was searching for the Lord, and he gave ear to my voice, and made me free from all my fears.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Let your eyes be turned to him and you will have light, and your faces will not be shamed.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 This poor man's cry came before the Lord, and he gave him salvation from all his troubles.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 The angel of the Lord is ever watching over those who have fear of him, to keep them safe.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 By experience you will see that the Lord is good; happy is the man who has faith in him.
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Keep yourselves in the fear of the Lord, all you his saints; for those who do so will have no need of anything.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 The young lions are in need and have no food; but those who are looking to the Lord will have every good thing.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Come, children, give attention to me; I will be your teacher in the fear of the Lord.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 What man has a love of life, and a desire that his days may be increased so that he may see good?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Keep your tongue from evil, and your lips from words of deceit.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Be turned from evil, and do good; make a search for peace, desiring it with all your heart.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 The eyes of the Lord are on the upright, and his ears are open to their cry.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 The face of the Lord is against those who do evil, to take away the memory of them from the earth.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 The cry of the upright comes before the Lord, and he takes them out of all their troubles.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 The Lord is near the broken-hearted; he is the saviour of those whose spirits are crushed down.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Great are the troubles of the upright: but the Lord takes him safely out of them all.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 He keeps all his bones: not one of them is broken.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Evil will put an end to the sinner, and those who are haters of righteousness will come to destruction.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 The Lord will be the saviour of the souls of his servants, and no one who has faith in him will be put to shame.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psalms 34 >