< Proverbs 28 >
1 The evil man goes running away when no man is after him, but the upright are without fear, like the lion.
Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 Because of the sin of the land, its troubles are increased; but by a man of wisdom and knowledge they will be put out like a fire.
Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 A man of wealth who is cruel to the poor is like a violent rain causing destruction of food.
Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 Those who have no respect for the law give praise to the evil-doer; but such as keep the law are against him.
Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 Evil men have no knowledge of what is right; but those who go after the Lord have knowledge of all things.
Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 Better is the poor man whose ways are upright, than the man of wealth whose ways are not straight.
Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
7 He who keeps the law is a wise son, but he who keeps company with feasters puts shame on his father.
Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8 He who makes his wealth greater by taking interest, only gets it together for him who has pity on the poor.
Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
9 As for the man whose ear is turned away from hearing the law, even his prayer is disgusting.
Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 Anyone causing the upright to go wandering in an evil way, will himself go down into the hole he has made; but the upright will have good things for their heritage.
Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
11 The man of wealth seems to himself to be wise, but the poor man who has sense has a low opinion of him.
Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
12 When the upright do well, there is great glory; but when evil-doers are lifted up, men do not let themselves be seen.
Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
13 He who keeps his sins secret will not do well; but one who is open about them, and gives them up, will get mercy.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
14 Happy is the man in whom is the fear of the Lord at all times; but he whose heart is hard will come into trouble.
Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
15 Like a loud-voiced lion and a wandering bear, is an evil ruler over a poor people.
Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
16 The prince who has no sense is a cruel ruler; but he who has no desire to get profit for himself will have long life.
Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
17 One who has been the cause of a man's death will go in flight to the underworld: let no man give him help.
Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
18 He whose ways are upright will be safe, but sudden will be the fall of him whose ways are twisted.
Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
19 By ploughing his land a man will have bread in full measure; but he who goes after good-for-nothing persons will be poor enough.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
20 A man of good faith will have great blessing, but one attempting to get wealth quickly will not go free from punishment.
Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
21 It is not good to have respect for a man's position: for a man will do wrong for a bit of bread.
Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
22 He who is ever desiring wealth goes running after money, and does not see that need will come on him.
Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
23 He who says words of protest to a man will later have more approval than one who says smooth words with his tongue.
Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
24 He who takes from his father or his mother what is theirs by right, and says, It is no sin; is the same as a taker of life.
Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
25 He who is ever desiring profit is a cause of fighting; but he who puts his faith in the Lord will be made fat.
Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
26 He whose faith is in himself is foolish; but everyone walking wisely will be kept safe.
Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
27 He who gives to the poor will never be in need, but great curses will be on him who gives no attention to them.
Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
28 When evil-doers are lifted up, men take cover; but when destruction overtakes them, the upright are increased.
Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.