< Proverbs 25 >
1 These are more wise sayings of Solomon, copied out by the men of Hezekiah, king of Judah.
Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
2 It is the glory of God to keep a thing secret: but the glory of kings is to have it searched out.
Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
3 The heaven is high and the earth is deep, and the hearts of kings may not be searched out.
Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
4 Take away the waste from silver, and a vessel will come out for the silver-worker.
Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
5 Take away evil-doers from before the king, and the seat of his power will be made strong in righteousness.
Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
6 Do not take glory for yourself before the king, and do not put yourself in the place of the great:
Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
7 For it is better to have it said to you, Come up here; than for you to be put down in a lower place before the ruler.
Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
8 Do not be quick to go to law about what you have seen, for what will you do in the end, when your neighbour has put you to shame?
Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
9 Have a talk with your neighbour himself about your cause, but do not give away the secret of another:
Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
10 Or your hearer may say evil of you, and your shame will not be turned away.
au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
11 A word at the right time is like apples of gold in a network of silver.
Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
12 Like a nose-ring of gold and an ornament of the best gold, is a wise man who says sharp words to an ear ready to give attention.
Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
13 As the cold of snow in the time of grain-cutting, so is a true servant to those who send him; for he gives new life to the soul of his master.
Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
14 As clouds and wind without rain, so is one who takes credit for an offering he has not given.
Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
15 A judge is moved by one who for a long time undergoes wrongs without protest, and by a soft tongue even bone is broken.
Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
16 If you have honey, take only as much as is enough for you; for fear that, being full of it, you may not be able to keep it down.
Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
17 Let not your foot be frequently in your neighbour's house, or he may get tired of you, and his feeling be turned to hate.
Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
18 One who gives false witness against his neighbour is a hammer and a sword and a sharp arrow.
Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
19 Putting one's faith in a false man in time of trouble is like a broken tooth and a shaking foot.
Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
20 Like one who takes off clothing in cold weather and like acid on a wound, is he who makes melody to a sad heart.
Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
21 If your hater is in need of food, give him bread; and if he is in need of drink, give him water:
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
22 For so you will put coals of fire on his head, and the Lord will give you your reward.
maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
23 As the north wind gives birth to rain, so is an angry face caused by a tongue saying evil secretly.
Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
24 It is better to be living in an angle of the house-top, than with a bitter-tongued woman in a wide house.
Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
25 As cold water to a tired soul, so is good news from a far country.
Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Like a troubled fountain and a dirty spring, is an upright man who has to give way before evil-doers.
Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
27 It is not good to take much honey: so he who is not looking for honour will be honoured.
Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
28 He whose spirit is uncontrolled is like an unwalled town which has been broken into.
Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.