< Numbers 32 >

1 Now the children of Reuben and the children of Gad had a great number of cattle: and when they saw that the land of Jazer and the land of Gilead was a good place for cattle;
Sasa wana wa uzao wa Reubeni na wa Gadi walikuwa na idadi kubwa ya wanyama. Waliiona ardhi ya Jazeri na Gileadi, kuwa ni ardhi nzuri kwa mifugo.
2 The children of Gad and the children of Reuben came and said to Moses and to Eleazar the priest and to the chiefs of the meeting,
Kwa hiyo wana wa Gadi na wa Reubeni wakaja kumwambia Musa, na Eliazari kuhani, na viongozi wa watu. Wakasema,
3 Ataroth, and Dibon, and Jazer, and Nimrah, and Heshbon, and Elealeh, and Sebam, and Nebo, and Beon,
“Hii ndiyo orodha ya maeneo ambayo tumeyatembelea: Diboni, Jazeri, Nimraha, Heshibonni, Ellealehi, Sebamu, Nebo, na Beoni.
4 The land which the Lord gave into the hands of the children of Israel, is a land for cattle, and your servants have cattle.
Haya ni maeneo ambayo BWANA aliyachukua mbele ya watu wa Israeli, na maeneo mazuri kwa ajili ya mifugo. Sisi watumishi wako tuna mifugo mingi sana.
5 And they said, With your approval, let this land be given to your servants as their heritage: do not take us over Jordan.
Wakasema kuwa, “Kama tutapata kibali mbele ya macho yako, tunaomba ardhi hii tupewe, sisi watumishi wako, kuwa urithi. Usituvushe ng'ambo ya Yorodani.”
6 And Moses said to the children of Gad and the children of Reuben, Are your brothers to go to the war, while you take your rest here?
Musa akawajibu wale wana wa auzao wa Gadi na Reubeni, “Je, mngependa ndugu zenu waende vitani wakati ninyi mkikaa hapa?
7 Why would you take from the children of Israel the desire to go over into the land which the Lord has given them?
Kwa nini kuwafish moyo watu wa Israeli wasivuke kwenda kwenye nchi ambayo BWANA amewapa?
8 So did your fathers, when I sent them from Kadesh-barnea to see the land.
Baba zenu walifanya hivyo nilipowatuma kutoka Kadeshi Banea kwenda kuipeleleza ile nchi.
9 For when they went up to the valley of Eshcol, and saw the land, they took from the children of Israel the desire to go into the land which the Lord had given them.
Walienda mpaka kwenye bonde la Eskoli. Waliiona ile ardhi kisha wakawafisha moyo watu wa Israeli kwa hiyo wakagoma kuingia kwenye nchi ambayo BWANA alikuwa amewapa.
10 And at that time the Lord was moved to wrath, and made an oath, saying,
Siku hiyo hasira ya BWANA iliwaka. Akaapa akisema,
11 Truly, not one of the men of twenty years old and over who came out of Egypt will see the land which I gave by oath to Abraham, Isaac, and Jacob; because they have not been true to me with all their heart;
'Kwa hakika hakuna mtu aliyetoka Misri, kuanzia wa umri wa miaka ishirini na zaidi ambao wataiona nchi ambao niliwaapia Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwa sababu hawakunifuata mimi kwa ukamilifu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi, na Yoshua mwana wa Nuni.
12 But only Caleb, the son of Jephunneh the Kenizzite, and Joshua, the son of Nun: because they have been true to the Lord.
Ni Kalebu na Joshua tu ndio walionifuata kwa ukamilifu.'
13 Then the Lord was angry with Israel, and he made them wanderers in the waste land for forty years? till all that generation who had done evil in the eyes of the Lord was dead.
Kwa hiyo hasira za BWANA ziliwaka juu ya Israei. Akawafanya wazunguke zunguke jangwani kwa miaka arobaini mpaka kile kizazi kilichofanya maovu mbele za macho yake kilipoteketea.
14 And now you have come to take the place of your fathers, another generation of sinners, increasing the wrath of the Lord against Israel.
Tazama, mmetokea katika nafasi za baba zenu, kama watu wengine wenye dhambi zaidi, ili kuongeza hasira ya BWANA kwa Israeli.
15 For if you are turned away from him, he will send them wandering again in the waste land; and you will be the cause of the destruction of all this people.
Kama hamtamfuata, ataiacha Israeli jangwani na mtakuwa mmewateketeza watu hawa wote.
16 Then they came to him, and said, We will make safe places for our cattle here, and towns for our little ones;
Kwa hiyo wakaja karibu na Musa wakamwambia, “Turuhusu tujenga hapa uzio kwa ajili ya ng'ombe zetu na miji hapa kwa ajili ya familia zetu.
17 But we ourselves will be ready armed to go before the children of Israel till we have taken them to their place: but our little ones will be safe in the walled towns against the people of the land.
Hata hivyo, sisi wenyewe tutajipanga kijeshi kwenda na jeshi la Israeli mpaka tumewaongoza kupata maeneo yao. Lakini familia zetu zitakuwa kwenye miji ya maboma kwa ssbabu ya watu wengine ambao bado wanaishi katika nchi hii.
18 We will not come back to our houses till every one of the children of Israel has come into his heritage.
Hatutarudi kwenye familia zetu mpaka kila mmoja watu wa Israeli apate urithi wake.
19 For we will not have our heritage with them on the other side of Jordan and forward; because our heritage has come to us on this side of Jordan to the east.
Sisi hatutachukua urithi wa ardhi pamoja nao kule ng'ambo ya Yorodani, kwa sababu urithi wetu uko hapa upande wa mashariki mwa Yorodani.”
20 Then Moses said to them, If you will do this, arming yourselves to go before the Lord to the war,
Kwa hiyo Musa akawajibu, “Kama mtafanya mnachokisema, kama mtajipanga wenyewe mbele za BWANA kwenda vitani,
21 Every armed man of you going across Jordan before the Lord till he has overcome and sent in flight all who are against him,
basi kila mmoja wa wanajeshi wenu lazima avuke Yorodani mbele za BWANA, mpaka atakapowafukuza maadui zake kutoka mbele zake
22 And the land is under the rule of the Lord: then after that you may come back, having done no wrong to the Lord and to Israel; and this land will be yours for your heritage before the Lord.
na nchi itawaliwe na Israeli mbele zake. Kisha mtaweza kurudi. Hamtakuwa na hatia mbele za BWANA na mbele ya Israeli. Hii nchi itakuwa miliki yenu mbele za BWANA.
23 But if you do not do this, then you are sinners against the Lord; and you may be certain that your sin will have its reward.
Bali kama hamtafnya hivyo, tazama, mtakuwa mmefanya dhambi mbele ya BWANA. Mwe na hakika kuwa dhambi yenu itaonekana
24 So get to work building your towns for your little ones, and safe places for your sheep; and do as you have said.
wazi. Jengeni miji kwa ajili ya familia zenu na mazizi kwa ajili ya kondoo zenu; kisha fanyeni kile mlichokisema.”
25 And the children of Gad and the children of Reuben said to Moses, Your servants will do as my lord says.
Wale wana wa Gadi na Reubeni wakamwambia Musa, wakisema, “Watumishi wako wtafanya kama vile wewe, bwana wetu, unavyotuamuru.
26 Our little ones, our wives, and our flocks, and all our cattle, will be there in the towns of Gilead;
Watoto wetu, wake zetu, makundi yetu, na wanyama wetu wote watakaa huko kwenye miji ya Gileadi.
27 But your servants will go over, every man armed for war, before the Lord to the fight, as my lord says.
Hata hivyo, sisi watumishi wako, tutavuka kwenda ng'ambo mbele za BWANA kupigana, kila mtu ambaye yuko tayari kwa vita, kama vile wewe, bwana wetu, unavyosema.”
28 So Moses gave orders about them to Eleazar the priest and to Joshua, the son of Nun, and to the heads of families of the tribes of the children of Israel.
Kwa hiyo Musa akawapa maelekezo yayowahusu kwa Eliazari kuhani, kwa Joshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa koo kufuata jamaa zao katika makabila ya wana wa Israeli.
29 And Moses said to them, If the children of Gad and the children of Reuben go with you over Jordan, every man armed for the fight before the Lord, and all the land is given into your hands, then let them have the land of Gilead for a heritage:
Musa akawaambia, “Kama uzao wa Reubeni na Gadi watavuka ng'ambo ya Yorodani pamoja nanyi, kila mwanamume anayetakiwa kuwa vitani mbele za BWANA, na kama nchi mtaitawala mbele zenu, ndipo mtakapowapa eneo la Gileadi kuwa miliki yao.
30 But if they do not go over with you armed, they will have to take their heritage with you in the land of Canaan.
Lakini kama hawatavuka pamoja nanyi wakiwa na silaha zao, basi mtawapa urithi wao katika nchi ya Kanaani.”
31 Then the children of Gad and the children of Reuben said, As the Lord has said to your servants, so will we do.
Kwas hiyo wana wa uzao wa Gadi na wa Reubeni wakamjibu wakisema, Kama vile BWANA alivyosema nasi, sisi watumwa wako, hiki ndicho tutakachokifanya.
32 We will go over armed before the Lord into the land of Canaan, and you will give us our heritage on this side of Jordan.
Tutavuka tukiwa na silaha zetu mbele za BWANA kuingia katika nchi ya Kanaani, lakini urithi wetu utabaki utabaki upande huu wa Yorodani.”
33 So Moses gave to them, even to the children of Gad and the children of Reuben and to the half-tribe of Manasseh, the son of Joseph, the kingdom of Sihon, king of the Amorites and Og, king of Bashan, all the land with its towns and the country round them.
Kwa hiyo uzao wa Gadi na Reubeni, na pia nusu ya kabila la Manase mwana wa Yusufu, Musa akawapa ufalme wa Sihoni, mfalme wa Waamori, na wa Ogi, mafalme wa Bashani, Aliwapa hiyo nchi, na kuwagawia miji yake yote pamoja na mipaka yake, miji yote ya nchi inayowazunguka.
34 And the children of Gad were the builders of Dibon and Ataroth and Aroer;
Wale wa uzao wa Gadi wakaijenga Diboni,
35 And Atroth-shophan and Jazer and Jogbehah;
Atarothi, Aroeri, Atrothi, Jazeri, Jogbehaha, Bethi Nimraha,
36 And Beth-nimrah and Beth-haran: walled towns and shut-in places for sheep.
na Bethi Harani kuwa miji iliyo na maboma na mazizi ya kondoo wao.
37 And the children of Reuben were the builders of Heshbon and Elealeh and Kiriathaim;
Wale wa uzao wa Reubeni wakaijenga Heshiboni. Elealehi, Kiriathaimu,
38 And Nebo and Baal-meon, (their names being changed, ) and Sibmah: and they gave other names to the towns they made.
Nebo, Baali Meoni - baadaye waliyabadili majina yao, na Sibimaha.
39 And the children of Machir, the son of Manasseh, went to Gilead and took it, driving out the Amorites who were living there.
Wale wa uzao wa Machiri mwana wa Manase walienda Gileadi na kuutwaa kutoka kwa Waamori waliokuwa wakiishi humo.
40 And Moses gave Gilead to Machir, the son of Manasseh; and he made it his living-place.
Kisha Musa akaitoa Gileadi kwa Machiri mwana wa Manase, na watu wake wakaishi humo.
41 And Jair, the son of Manasseh, went and took the towns of Gilead, naming them Havvoth-Jair.
Jairi mwana wa Manase alienda kuiteka miji yake na kuiita Havothi Jairi.
42 And Nobah went and took Kenath and its small towns, naming it Nobah, after himself.
Nobaha alienda kuitieka Kenathi na vijiji vyake, na akauita kwa jina lake Nobaha.

< Numbers 32 >