< Numbers 2 >

1 And the Lord said to Moses and Aaron,
Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
2 The children of Israel are to put up their tents in the order of their families, by the flags of their fathers' houses, facing the Tent of meeting on every side.
“Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
3 Those whose tents are on the east side, looking to the dawn, will be round the flag of the children of Judah, with Nahshon, the son of Amminadab, as their chief.
Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
4 The number of his army was seventy-four thousand, six hundred.
Kundi lake lina watu 74,600.
5 And nearest to him will be the tribe of Issachar, with Nethanel, the son of Zuar, as their chief.
Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
6 The number of his army was fifty-four thousand, four hundred.
Kundi lake lina watu 54,400.
7 After him, the tribe of Zebulun, with Eliab, the son of Helon, as their chief.
Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
8 The number of his army was fifty-seven thousand, four hundred.
Kundi lake lina watu 57,400.
9 The number of all the armies of Judah was a hundred and eighty-six thousand, four hundred. They go forward first.
Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
10 On the south side is the flag of the children of Reuben, in the order of their armies, with Elizur, the son of Shedeur, as their chief.
Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
11 The number of his army was forty-six thousand, five hundred.
Kundi lake lina watu 46,500.
12 And nearest to him, the tribe of Simeon, with Shelumiel, the son of Zurishaddai, as their chief.
Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
13 The number of his army was fifty-nine thousand, three hundred.
Kundi lake lina watu 59,300.
14 Then the tribe of Gad, with Eliasaph, son of Reuel, as their chief.
Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
15 The number of his army was forty-five thousand, six hundred and fifty.
Kundi lake lina watu 45,650.
16 The number of all the armies of Reuben together came to a hundred and fifty-one thousand, four hundred and fifty. They go forward second.
Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
17 Then the Tent of meeting is to go forward, with the tents of the Levites, in the middle of the armies; in the same order as their tents are placed, they are to go forward, every man under his flag.
Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
18 On the west side will be the flag of the children of Ephraim, with Elishama, the son of Ammihud, as their chief.
Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
19 The number of his army was forty thousand, five hundred.
Kundi lake lina watu 40,500.
20 And by him the tribe of Manasseh with Gamaliel, the son of Pedahzur, as their chief.
Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
21 The number of his army was thirty-two thousand, two hundred.
Kundi lake lina watu 32,200.
22 Then the tribe of Benjamin, with Abidan, the son of Gideoni, as their chief.
Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
23 The number of his army was thirty-five thousand, four hundred.
Kundi lake lina watu 35,400.
24 The number of all the armies of Ephraim was a hundred and eight thousand, one hundred. They go forward third.
Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
25 On the north side will be the flag of the children of Dan, with Ahiezer, the son of Ammishaddai, as their chief.
Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
26 The number of his army was sixty-two thousand, seven hundred.
Kundi lake lina watu 62,700.
27 Nearest to him will be the tribe of Asher, with Pagiel, the son of Ochran, as their chief.
Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
28 The number of his army was forty-one thousand, five hundred;
Kundi lake lina watu 41,500.
29 Then the tribe of Naphtali, with Ahira, the son of Enan, as their chief.
Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
30 The number of his army was fifty-three thousand, four hundred.
Kundi lake lina watu 53,400.
31 The number of all the armies in the tents of Dan was a hundred and fifty-seven thousand, six hundred. They will go forward last, by their flags.
Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
32 These are all who were numbered of the children of Israel, in the order of their fathers' families: all the armies in their tents together came to six hundred and three thousand, five hundred and fifty.
Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
33 But the Levites were not numbered among the children of Israel, as the Lord said to Moses.
Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
34 So the children of Israel did as the Lord said to Moses, so they put up their tents by their flags, and they went forward in the same order, by their families, and by their fathers' houses.
Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.

< Numbers 2 >