< Judges 10 >

1 Now after Abimelech, Tola, the son of Puah, the son of Dodo, a man of Issachar, became the saviour of Israel; he was living in Shamir in the hill-country of Ephraim.
Baada ya Abimeleki, Tola, mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, aliyekaa Shamiri, katika mlima wa Efraimu, akaondoka ili kuwaokoa Israeli.
2 He was judge over Israel for twenty-three years; and at his death his body was put to rest in the earth in Shamir.
Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na mitatu. Alikufa na kuzikwa Shamiri.
3 And after him came Jair the Gileadite, who was judge over Israel for twenty-two years.
Alifuatiwa na Yairi Mgileadi. Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na miwili.
4 And he had thirty sons, who went on thirty young asses; and they had thirty towns in the land of Gilead, which are named Havvoth-Jair to this day.
Alikuwa na wana thelathini waliokuwa wakipanda kwenye punda thelathini, na walikuwa na miji thelathini, ambayo inaitwa Hawoth Yairi hata leo, iliyo katika nchi ya Gileadi.
5 And at the death of Jair his body was put to rest in the earth in Kamon.
Yairi alikufa na kuzikwa Kamoni.
6 And again the children of Israel did evil in the eyes of the Lord, worshipping the Baals and Astartes, and the gods of Aram and the gods of Zidon and the gods of Moab and the gods of the children of Ammon and the gods of the Philistines; they gave up the Lord and were servants to him no longer.
Watu wa Israeli waliendelea kutenda maovu mbele za Bwana, wakaabudu Mabaali, Maashtoreti, miungu ya Aramu, miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu, miungu ya wana wa Amoni, na miungu ya Wafilisti. Wakamsahau Bwana na hawakamsujudia tena.
7 And the wrath of the Lord was burning against Israel, and he gave them up into the hands of the Philistines and into the hands of the children of Ammon.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mikononi mwa Wafilisti na katika mikono ya wana wa Amoni.
8 And that year the children of Israel were crushed under their yoke; for eighteen years all the children of Israel on the other side of Jordan, in the land of the Amorites which is in Gilead, were cruelly crushed down.
Wakawaangamiza na kuwadhulumu watu wa Israeli mwaka huo, na kwa muda wa miaka kumi na nane waliwafukuza watu wote wa Israeli waliokuwa ng'ambo ya Yordani katika nchi ya Waamori, iliyoko Gileadi.
9 And the children of Ammon went over Jordan, to make war against Judah and Benjamin and the house of Ephraim; and Israel was in great trouble.
Nao wana wa Amoni wakavuka Yordani, wakapigana na Yuda, na Benyamini, na nyumba ya Efraimu; Israeli akasumbuliwa sana.
10 Then the children of Israel, crying out to the Lord, said, Great is our sin against you, for we have given up our God and have been servants to the Baals.
Ndipo wana wa Israeli wakamwita Bwana, wakisema, “Tumekukosea, kwa sababu tumemwacha Mungu wetu, tukaabudu Mabaali.”
11 And the Lord said to the children of Israel, Were not the Egyptians and the Amorites and the children of Ammon and the Philistines
Bwana akawaambia wana wa Israeli, “Je, sikuwatoa ninyi kutoka kwa Wamisri, na Waamori, na Waamoni, na Wafilisti,
12 And the Zidonians and Amalek and Midian crushing you down, and in answer to your cry did I not give you salvation from their hands?
na pia kwa Wasidoni? Waamaleki na Wamaoni walipowakandamiza; mliniita, nami nikawaokoa kutoka katika nguvu zao.
13 But, for all this, you have given me up and have been servants to other gods: so I will be your saviour no longer.
Lakini ninyi mliniacha tena na kuabudu miungu mingine. Kwa hiyo, sitawaokoa tena.
14 Go, send up your cry for help to the gods of your selection; let them be your saviours in the time of your trouble.
Nendeni mkaiite miungu mnayoiabudu. Ili iwaokoe wakati wa shida.
15 And the children of Israel said to the Lord, We are sinners; do to us whatever seems good to you: only give us salvation this day.
Wana wa Israeli wakamwambia Bwana, Tumefanya dhambi. Tufanyie chochote kinachoonekana kuwa kizuri kwako. Tafadhali, tuokoe leo.
16 So they put away the strange gods from among them, and became the Lord's servants; and his soul was angry because of the sorrows of Israel.
Wakaiacha miungu ya kigeni waliyokuwa nayo, nao wakamwabudu Bwana. Naye akawa na subira juu ya taabu ya Israeli.
17 Then the children of Ammon came together and put their army in position in Gilead. And the children of Israel came together and put their army in position in Mizpah.
Ndipo Waamoni wakakusanyika, wakaweka kambi Gileadi. Waisraeli walikutana na kuweka kambi yao huko Mispa.
18 And the people of Israel said to one another, Who will be the first to make an attack on the children of Ammon? We will make him head over all Gilead.
Viongozi wa watu wa Gileadi wakaambiana, 'Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni? Yeye atakuwa kiongozi juu ya wote wanaoishi Gileadi.

< Judges 10 >